< Job 40 >

1 Moreover Yhwh answered Job, and said,
Bwana akamwambia Ayubu:
2 Shall he that contendeth with the Almighty instruct him? he that reproveth God, let him answer it.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Then Job answered Yhwh, and said,
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Behold, I am vile; what shall I answer thee? I will lay mine hand upon my mouth.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Once have I spoken; but I will not answer: yea, twice; but I will proceed no further.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Then answered Yhwh unto Job out of the whirlwind, and said,
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Gird up thy loins now like a man: I will demand of thee, and declare thou unto me.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Wilt thou also disannul my judgment? wilt thou condemn me, that thou mayest be righteous?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Hast thou an arm like God? or canst thou thunder with a voice like him?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Deck thyself now with majesty and excellency; and array thyself with glory and beauty.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Cast abroad the rage of thy wrath: and behold every one that is proud, and abase him.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Look on every one that is proud, and bring him low; and tread down the wicked in their place.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Hide them in the dust together; and bind their faces in secret.
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Then will I also confess unto thee that thine own right hand can save thee.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Behold now behemoth, which I made with thee; he eateth grass as an ox.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Lo now, his strength is in his loins, and his force is in the navel of his belly.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 He moveth his tail like a cedar: the sinews of his stones are wrapped together.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 His bones are as strong pieces of brass; his bones are like bars of iron.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 He is the chief of the ways of God: he that made him can make his sword to approach unto him.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Surely the mountains bring him forth food, where all the beasts of the field play.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 He lieth under the shady trees, in the covert of the reed, and fens.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 The shady trees cover him with their shadow; the willows of the brook compass him about.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Behold, he drinketh up a river, and hasteth not: he trusteth that he can draw up Jordan into his mouth.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 He taketh it with his eyes: his nose pierceth through snares.
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< Job 40 >