< Job 36 >

1 Elihu also proceeded, and said,
Elihu aliendelea na kusema,
2 Suffer me a little, and I will shew thee that I have yet to speak on God’s behalf.
“Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
3 I will fetch my knowledge from afar, and will ascribe righteousness to my Maker.
Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
4 For truly my words shall not be false: he that is perfect in knowledge is with thee.
Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
5 Behold, God is mighty, and despiseth not any: he is mighty in strength and wisdom.
Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
6 He preserveth not the life of the wicked: but giveth right to the poor.
Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
7 He withdraweth not his eyes from the righteous: but with kings are they on the throne; yea, he doth establish them for ever, and they are exalted.
Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
8 And if they be bound in fetters, and be holden in cords of affliction;
Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
9 Then he sheweth them their work, and their transgressions that they have exceeded.
kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
10 He openeth also their ear to discipline, and commandeth that they return from iniquity.
Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
11 If they obey and serve him, they shall spend their days in prosperity, and their years in pleasures.
Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
12 But if they obey not, they shall perish by the sword, and they shall die without knowledge.
Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
13 But the hypocrites in heart heap up wrath: they cry not when he bindeth them.
Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
14 They die in youth, and their life is among the unclean.
Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
15 He delivereth the poor in his affliction, and openeth their ears in oppression.
Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
16 Even so would he have removed thee out of the strait into a broad place, where there is no straitness; and that which should be set on thy table should be full of fatness.
Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
17 But thou hast fulfilled the judgment of the wicked: judgment and justice take hold on thee.
Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
18 Because there is wrath, beware lest he take thee away with his stroke: then a great ransom cannot deliver thee.
Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
19 Will he esteem thy riches? no, not gold, nor all the forces of strength.
Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
20 Desire not the night, when people are cut off in their place.
Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
21 Take heed, regard not iniquity: for this hast thou chosen rather than affliction.
Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
22 Behold, God exalteth by his power: who teacheth like him?
Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Who hath enjoined him his way? or who can say, Thou hast wrought iniquity?
Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
24 Remember that thou magnify his work, which men behold.
Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
25 Every man may see it; man may behold it afar off.
Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
26 Behold, God is great, and we know him not, neither can the number of his years be searched out.
Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
27 For he maketh small the drops of water: they pour down rain according to the vapour thereof:
Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
28 Which the clouds do drop and distil upon man abundantly.
ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
29 Also can any understand the spreadings of the clouds, or the noise of his tabernacle?
Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
30 Behold, he spreadeth his light upon it, and covereth the bottom of the sea.
Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
31 For by them judgeth he the people; he giveth meat in abundance.
Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
32 With clouds he covereth the light; and commandeth it not to shine by the cloud that cometh betwixt.
Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
33 The noise thereof sheweth concerning it, the cattle also concerning the vapour.
Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.

< Job 36 >