< 1 Kings 13 >

1 And, behold, there came a man of God out of Judah by the word of Yhwh unto Beth–el: and Jeroboam stood by the altar to burn incense.
Kwa neno la Bwana, mtu wa Mungu alifika Betheli kutoka Yuda wakati Yeroboamu alipokuwa amesimama kando ya madhabahu ili kutoa sadaka.
2 And he cried against the altar in the word of Yhwh, and said, O altar, altar, thus saith Yhwh; Behold, a child shall be born unto the house of David, Josiah by name; and upon thee shall he offer the priests of the high places that burn incense upon thee, and men’s bones shall be burnt upon thee.
Akapiga kelele dhidi ya madhabahu kwa neno la Bwana: “Ee madhabahu, madhabahu! Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika nyumba ya Daudi. Juu yako atawatoa dhabihu makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu wale ambao wanatoa sadaka hapa sasa, nayo mifupa ya wanadamu itachomwa juu yako.’”
3 And he gave a sign the same day, saying, This is the sign which Yhwh hath spoken; Behold, the altar shall be rent, and the ashes that are upon it shall be poured out.
Siku iyo hiyo, mtu wa Mungu akatoa ishara: “Hii ndiyo ishara Bwana aliyotangaza: Madhabahu haya yatapasuka na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.”
4 And it came to pass, when king Jeroboam heard the saying of the man of God, which had cried against the altar in Beth–el, that he put forth his hand from the altar, saying, Lay hold on him. And his hand, which he put forth against him, dried up, so that he could not pull it in again to him.
Mfalme Yeroboamu aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, alipopiga kelele dhidi ya madhabahu huko Betheli, akanyoosha mkono wake kutoka madhabahuni na kusema, “Mkamate!” Lakini mkono aliokuwa ameunyoosha kumwelekea yule mtu ukasinyaa na kubaki hapo hapo, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha.
5 The altar also was rent, and the ashes poured out from the altar, according to the sign which the man of God had given by the word of Yhwh.
Pia, madhabahu yalipasuka na majivu yakamwagika sawasawa na ishara iliyotolewa na mtu wa Mungu kwa neno la Bwana.
6 And the king answered and said unto the man of God, Intreat now the face of Yhwh thy God, and pray for me, that my hand may be restored me again. And the man of God besought Yhwh, and the king’s hand was restored him again, and became as it was before.
Kisha mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “Niombee kwa Bwana Mungu wako ili mkono wangu upate kupona.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwombea kwa Bwana, nao mkono wa mfalme ukapona na kuwa kama ulivyokuwa hapo kwanza.
7 And the king said unto the man of God, Come home with me, and refresh thyself, and I will give thee a reward.
Mfalme akamwambia yule mtu wa Mungu, “Twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
8 And the man of God said unto the king, If thou wilt give me half thine house, I will not go in with thee, neither will I eat bread nor drink water in this place:
Lakini yule mtu wa Mungu akamjibu mfalme, “Hata kama ungenipa nusu ya mali zako, nisingekwenda pamoja na wewe, wala nisingekula mkate au kunywa maji hapa.
9 For so was it charged me by the word of Yhwh, saying, Eat no bread, nor drink water, nor turn again by the same way that thou camest.
Kwa kuwa niliagizwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate wala usinywe maji au kurudi kwa njia uliyojia.’”
10 So he went another way, and returned not by the way that he came to Beth–el.
Kwa hiyo akafuata njia nyingine na hakurudi kupitia njia ile ambayo alikuwa ameijia Betheli.
11 Now there dwelt an old prophet in Beth–el; and his sons came and told him all the works that the man of God had done that day in Beth–el: the words which he had spoken unto the king, them they told also to their father.
Basi kulikuwepo na nabii fulani mzee aliyekuwa anaishi Betheli, ambaye wanawe walikuja kumwambia yote ambayo mtu wa Mungu alikuwa ameyafanya pale siku ile. Pia wakamwambia baba yao yale aliyomwambia mfalme.
12 And their father said unto them, What way went he? For his sons had seen what way the man of God went, which came from Judah.
Baba yao akawauliza, “Ameelekea njia gani?” Nao wanawe wakamwonyesha ile njia yule mtu wa Mungu kutoka Yuda aliyopita.
13 And he said unto his sons, Saddle me the donkey. So they saddled him the donkey: and he rode thereon,
Hivyo akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda.” Walipokwisha kumtandikia punda, akampanda
14 And went after the man of God, and found him sitting under an oak: and he said unto him, Art thou the man of God that camest from Judah? And he said, I am.
na kumfuatilia yule mtu wa Mungu. Akamkuta ameketi chini ya mwaloni na akamuuliza, “Je, wewe ndiwe mtu wa Mungu kutoka Yuda?” Akamjibu, “Mimi ndiye.”
15 Then he said unto him, Come home with me, and eat bread.
Basi nabii akamwambia, “Karibu nyumbani pamoja na mimi ule.”
16 And he said, I may not return with thee, nor go in with thee: neither will I eat bread nor drink water with thee in this place:
Yule mtu wa Mungu akasema, “Siwezi kurudi na kwenda nawe, wala siwezi kula mkate au kunywa maji pamoja nawe mahali hapa.
17 For it was said to me by the word of Yhwh, Thou shalt eat no bread nor drink water there, nor turn again to go by the way that thou camest.
Nimeambiwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate au kunywa maji huko au kurudia njia uliyojia.’”
18 He said unto him, I am a prophet also as thou art; and an angel spake unto me by the word of Yhwh, saying, Bring him back with thee into thine house, that he may eat bread and drink water. But he lied unto him.
Yule nabii mzee akajibu, “Mimi pia ni nabii, kama wewe. Naye malaika alisema nami kwa neno la Bwana: ‘Mrudishe aje katika nyumba yako ili apate kula mkate na kunywa maji.’” (Lakini alikuwa akimwambia uongo.)
19 So he went back with him, and did eat bread in his house, and drank water.
Hivyo mtu wa Mungu akarudi pamoja naye na akala na kunywa katika nyumba yake.
20 And it came to pass, as they sat at the table, that the word of Yhwh came unto the prophet that brought him back:
Wakati walipokuwa wameketi mezani, neno la Bwana likamjia yule nabii mzee aliyemrudisha huyo mtu wa Mungu.
21 And he cried unto the man of God that came from Judah, saying, Thus saith Yhwh, Forasmuch as thou hast disobeyed the mouth of Yhwh, and hast not kept the commandment which Yhwh thy God commanded thee,
Akampazia sauti yule mtu wa Mungu aliyekuwa ametoka Yuda, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Umeasi neno la Bwana na hukushika amri uliyopewa na Bwana Mungu wako,
22 But camest back, and hast eaten bread and drunk water in the place, of the which the Lord did say to thee, Eat no bread, and drink no water; thy carcase shall not come unto the sepulchre of thy fathers.
bali ulirudi na ukala mkate na kunywa maji mahali ambapo alikuambia usile wala usinywe. Kwa hiyo maiti yako haitazikwa katika kaburi la baba zako.’”
23 And it came to pass, after he had eaten bread, and after he had drunk, that he saddled for him the donkey, to wit, for the prophet whom he had brought back.
Wakati huyo mtu wa Mungu alipomaliza kula na kunywa, nabii aliyekuwa amemrudisha akamtandikia punda wake.
24 And when he was gone, a lion met him by the way, and slew him: and his carcase was cast in the way, and the donkey stood by it, the lion also stood by the carcase.
Alipokuwa akienda akakutana na simba njiani, akamuua na maiti yake ikabwagwa barabarani, yule punda wake na simba wakiwa wamesimama karibu yake.
25 And, behold, men passed by, and saw the carcase cast in the way, and the lion standing by the carcase: and they came and told it in the city where the old prophet dwelt.
Baadhi ya watu waliopita pale waliona maiti imebwagwa pale chini, simba akiwa amesimama kando ya maiti, wakaenda na kutoa habari katika mji ambao nabii mzee aliishi.
26 And when the prophet that brought him back from the way heard thereof, he said, It is the man of God, who was disobedient unto the word of Yhwh: Therefore Yhwh hath delivered him unto the lion, which hath torn him, and slain him, according to the word of Yhwh, which he spake unto him.
Yule nabii aliyekuwa amemrudisha kutoka safari yake aliposikia habari hii akasema, “Ni yule mtu wa Mungu ambaye aliasi neno la Bwana. Bwana amemtoa kwa simba, ambaye amemrarua na kumuua, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limemwonya.”
27 And he spake to his sons, saying, Saddle me the donkey. And they saddled him.
Nabii akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda,” nao wakafanya hivyo.
28 And he went and found his carcase cast in the way, and the donkey and the lion standing by the carcase: the lion had not eaten the carcase, nor torn the donkey.
Kisha akatoka akaenda akakuta maiti imebwagwa chini barabarani, punda na simba wakiwa wamesimama kando yake. Simba hakuwa amekula ile maiti wala kumrarua punda.
29 And the prophet took up the carcase of the man of God, and laid it upon the donkey, and brought it back: and the old prophet came to the city, to mourn and to bury him.
Basi yule nabii mzee akachukua maiti ya mtu wa Mungu, akailaza juu ya punda na akairudisha katika mji wake, ili amwombolezee na kumzika.
30 And he laid his carcase in his own grave; and they mourned over him, saying, Alas, my brother!
Kisha akailaza ile maiti katika kaburi lake huyo nabii mzee, nao wakaomboleza juu yake na kusema, “Ee ndugu yangu!”
31 And it came to pass, after he had buried him, that he spake to his sons, saying, When I am dead, then bury me in the sepulchre wherein the man of God is buried; lay my bones beside his bones:
Baada ya kumzika, akawaambia wanawe, “Wakati nitakapokufa, mnizike kwenye kaburi alimozikwa huyu mtu wa Mungu; lazeni mifupa yangu kando ya mifupa yake.
32 For the saying which he cried by the word of Yhwh against the altar in Beth–el, and against all the houses of the high places which are in the cities of Samaria, shall surely come to pass.
Kwa maana ujumbe alioutangaza kwa neno la Bwana dhidi ya madhabahu huko Betheli na dhidi ya madhabahu yote katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Samaria, hakika yatatokea kweli.”
33 After this thing Jeroboam returned not from his evil way, but made again of the lowest of the people priests of the high places: whosoever would, he consecrated him, and he became one of the priests of the high places.
Hata baada ya haya, Yeroboamu hakubadili njia zake mbaya, lakini mara nyingine tena akaweka makuhani kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu kutoka watu wa aina zote. Yeyote aliyetaka kuwa kuhani alimweka wakfu kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu.
34 And this thing became sin unto the house of Jeroboam, even to cut it off, and to destroy it from off the face of the earth.
Hii ilikuwa ndiyo dhambi ya nyumba ya Yeroboamu ambayo iliisababishia kuanguka na kuangamia kwake hadi kutoweka kwenye uso wa dunia.

< 1 Kings 13 >