< Psalms 19 >

1 The heavens declare the glory of El; and the firmameint sheweth his handywork.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2 Day unto day uttereth speech, and night unto night sheweth knowledge.
Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3 There is no speech nor language, where their voice is not heard.
Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
4 Their line is gone out through all the earth, and their words to the end of the world. In them hath he set a tabernacle for the sun,
Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
5 Which is as a bridegroom coming out of his chamber, and rejoiceth as a strong man to run a race.
linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
6 His going forth is from the end of the heaven, and his circuit unto the ends of it: and there is nothing hid from the heat thereof.
Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
7 The law of YHWH is perfect, converting the soul: the testimony of YHWH is sure, making wise the simple.
Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
8 The statutes of YHWH are right, rejoicing the heart: the commandment of YHWH is pure, enlightening the eyes.
Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
9 The fear of YHWH is clean, enduring for ever: the judgments of YHWH are true and righteous altogether.
Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
10 More to be desired are they than gold, yea, than much fine gold: sweeter also than honey and the honeycomb.
Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
11 Moreover by them is thy servant warned: and in keeping of them there is great reward.
Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
12 Who can understand his errors? cleanse thou me from secret faults.
Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
13 Keep back thy servant also from presumptuous sins; let them not have dominion over me: then shall I be upright, and I shall be innocent from the great transgression.
Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
14 Let the words of my mouth, and the meditation of my heart, be acceptable in thy sight, O YHWH, my strength, and my redeemer.
Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.

< Psalms 19 >