< Psalms 143 >

1 Hear my prayer, O YHWH, give ear to my supplications: in thy faithfulness answer me, and in thy righteousness.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
2 And enter not into judgment with thy servant: for in thy sight shall no man living be justified.
Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
3 For the enemy hath persecuted my soul; he hath smitten my life down to the ground; he hath made me to dwell in darkness, as those that have been long dead.
Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
4 Therefore is my spirit overwhelmed within me; my heart within me is desolate.
Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
5 I remember the days of old; I meditate on all thy works; I muse on the work of thy hands.
Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
6 I stretch forth my hands unto thee: my soul thirsteth after thee, as a thirsty land. (Selah)
Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
7 Hear me speedily, O YHWH: my spirit faileth: hide not thy face from me, lest I be like unto them that go down into the pit.
Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
8 Cause me to hear thy lovingkindness in the morning; for in thee do I trust: cause me to know the way wherein I should walk; for I lift up my soul unto thee.
Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
9 Deliver me, O YHWH, from mine enemies: I flee unto thee to hide me.
Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
10 Teach me to do thy will; for thou art my Elohim: thy spirit is good; lead me into the land of uprightness.
Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
11 Quicken me, O YHWH, for thy name's sake: for thy righteousness' sake bring my soul out of trouble.
Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
12 And of thy mercy cut off mine enemies, and destroy all them that afflict my soul: for I am thy servant.
Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

< Psalms 143 >