< Psalms 142 >
1 I cried unto YHWH with my voice; with my voice unto YHWH did I make my supplication.
Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
2 I poured out my complaint before him; I shewed before him my trouble.
Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
3 When my spirit was overwhelmed within me, then thou knewest my path. In the way wherein I walked have they privily laid a snare for me.
Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
4 I looked on my right hand, and beheld, but there was no man that would know me: refuge failed me; no man cared for my soul.
Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
5 I cried unto thee, O YHWH: I said, Thou art my refuge and my portion in the land of the living.
Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
6 Attend unto my cry; for I am brought very low: deliver me from my persecutors; for they are stronger than I.
Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
7 Bring my soul out of prison, that I may praise thy name: the righteous shall compass me about; for thou shalt deal bountifully with me.
Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.