< Psalms 109 >

1 HOLD not thy peace, O God of my praise;
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 For the mouth of the wicked and the mouth of the deceitful are opened against me: they have spoken against me with a lying tongue.
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 They compassed me about also with words of hatred; and fought against me without a cause.
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 For my love they are my adversaries: but I give myself unto prayer.
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 And they have rewarded me evil for good, and hatred for my love.
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 Set thou a wicked man over him: and let Satan stand at his right hand.
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 When he shall be judged, let him be condemned: and let his prayer become sin.
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 Let his days be few; and let another take his office.
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 Let his children be fatherless, and his wife a widow.
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 Let his children be continually vagabonds, and beg: let them seek their bread also out of their desolate places.
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 Let the extortioner catch all that he hath; and let the strangers spoil his labour.
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 Let there be none to extend mercy unto him: neither let there be any to favour his fatherless children.
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 Let his posterity be cut off; and in the generation following let their name be blotted out.
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 Let the iniquity of his fathers be remembered with the Lord; and let not the sin of his mother be blotted out.
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 Let them be before the Lord continually, that he may cut off the memory of them from the earth.
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 Because that he remembered not to shew mercy, but persecuted the poor and needy man, that he might even slay the broken in heart.
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 As he loved cursing, so let it come unto him: as he delighted not in blessing, so let it be far from him.
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 As he clothed himself with cursing like as with his garment, so let it come into his bowels like water, and like oil into his bones.
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 Let it be unto him as the garment which covereth him, and for a girdle wherewith he is girded continually.
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 Let this be the reward of mine adversaries from the Lord, and of them that speak evil against my soul.
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 But do thou for me, O God the Lord, for thy name’s sake: because thy mercy is good, deliver thou me.
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 For I am poor and needy, and my heart is wounded within me.
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 I am gone like the shadow when it declineth: I am tossed up and down as the locust.
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 My knees are weak through fasting; and my flesh faileth of fatness.
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 I became also a reproach unto them: when they looked upon me they shaked their heads.
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 Help me, O Lord my God: O save me according to thy mercy:
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 That they may know that this is thy hand; that thou, Lord, hast done it.
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 Let them curse, but bless thou: when they arise, let them be ashamed; but let thy servant rejoice.
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 Let mine adversaries be clothed with shame, and let them cover themselves with their own confusion, as with a mantle.
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 I will greatly praise the Lord with my mouth; yea, I will praise him among the multitude.
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 For he shall stand at the right hand of the poor, to save him from those that condemn his soul.
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.

< Psalms 109 >