< Romans 16 >

1 I commend to you Phebe our sister, which is a servant of the church which is at Cenchrea:
Namkabidhi kwenu Fibi dada yetu, ambaye ni mtumishi wa kanisa ambalo liko Kenkrea,
2 That you receive her in the Lord, as becomes saints, and that you assist her in whatever business she has need of you: for she has been a succorer of many, and of myself also.
ili kwamba mnaweza kumpokea katika Bwana. Fanyeni hivi katika kicho cha thamani cha waumini, na msimame pamoja naye katika jambo lolote atakalokuwa na uhitaji nalo. Maana yeye mwenyewe amekuwa mhudumu wa wengi, na kwa ajili yangu mwenyewe.
3 Greet Priscilla and Aquila my helpers in Christ Jesus:
Msalimu Priska na Akila, watenda kazi pamoja nami katika Kristo Yesu,
4 Who have for my life laid down their own necks: to whom not only I give thanks, but also all the churches of the Gentiles.
ambao kwa maisha yangu waliyahatarisha maisha yao wenyewe. Ninatoa shukrani kwao, na siyo tu mimi, bali pia kwa makanisa yote ya mataifa.
5 Likewise greet the church that is in their house. Salute my well-beloved Epaenetus, who is the first fruits of Achaia to Christ.
Lisalimie kanisa ambalo liko nyumbani kwao. Msalimie Epanieto mpendwa wangu, ambaye ni mzaliwa wa kwanza wa Kristo katika Asia.
6 Greet Mary, who bestowed much labor on us.
Msalimie Mariamu ambaye ametenda kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
7 Salute Andronicus and Junia, my kinsmen, and my fellow-prisoners, who are of note among the apostles, who also were in Christ before me.
Msalimie Androniko na Yunia, jamaa zangu, na wafungwa pamoja nami. Ni wa muhimu miongoni mwa mitume, ambao pia walitangulia kumjua Kristo kabla yangu.
8 Greet Amplias my beloved in the Lord.
Msalimie Ampliato, mpendwa wangu katika Bwana.
9 Salute Urbane, our helper in Christ, and Stachys my beloved.
Msalimie Urbano, mtenda kazi pamoja nami katika Kristo, na Stakisi mpendwa wangu.
10 Salute Apelles approved in Christ. Salute them which are of Aristobulus’ household.
Msalimie Apele, mwenye kukubaliwa katika Kristo. Wasalimie wote ambao walio katika nyumba ya Aristobulo.
11 Salute Herodion my kinsman. Greet them that be of the household of Narcissus, which are in the Lord.
Nisalimie Herodioni, jamaa yangu. Nisalimie wote walio katika nyumba ya Narkiso, ambao wako katika Bwana.
12 Salute Tryphena and Tryphosa, who labor in the Lord. Salute the beloved Persis, which labored much in the Lord.
Nisalimie Trifaina na Trifosa, wanaotenda kazi kwa bidii katika Bwana. msalimie Persisi mpendwa, ambaye ametenda kazi zaidi kwa Bwana,
13 Salute Rufus chosen in the Lord, and his mother and mine.
Nisalimie Rufo, aliyechaguliwa katika Bwana na mama yake na wangu.
14 Salute Asyncritus, Phlegon, Hermas, Patrobas, Hermes, and the brothers which are with them.
Msalimie Asinkrito, Flegon, Herme, Patroba, Herma, na ndugu wote walio pamoja nao.
15 Salute Philologus, and Julia, Nereus, and his sister, and Olympas, and all the saints which are with them.
Nisalimie Filologo naYulia, Nerea na dada yake, na Olimpa, na waumini wote walio pamoja nao.
16 Salute one another with an holy kiss. The churches of Christ salute you.
Nisalimie kila mmoja kwa busu takatifu. Makanisa yote katika Kristo yawasalimu.
17 Now I beseech you, brothers, mark them which cause divisions and offenses contrary to the doctrine which you have learned; and avoid them.
Sasa nawasihi, ndugu, kutafakari juu ya hao ambao wanasababisha mgawanyiko na vipingamizi. Wanakwenda kinyume na mafundisho ambayo mmekwisha kujifunza. Geukeni mtoke kwao.
18 For they that are such serve not our Lord Jesus Christ, but their own belly; and by good words and fair speeches deceive the hearts of the simple.
Kwa maana watu kama hawa hawamtumikii Kristo Bwana, bali matumbo yao wenyewe. Kwa maneno yao laini na pongezi za uongo wanadanganya mioyo ya wasio na hatia.
19 For your obedience is come abroad to all men. I am glad therefore on your behalf: but yet I would have you wise to that which is good, and simple concerning evil.
Kwa mfano wa utii wenu mwamfikia kila mmoja. Kwa hiyo, nafurahi juu yenu, lakini nawataka ninyi mwe na busara katika hali ya wema, na kutokuwa na hatia mbele ya uovu.
20 And the God of peace shall bruise Satan under your feet shortly. The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen.
Mungu wa amani hatakawia kumwangamiza shetani chini ya nyayo zenu. Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.
21 Timotheus my workfellow, and Lucius, and Jason, and Sosipater, my kinsmen, salute you.
Timotheo, mtendakazi pamoja nami, awasalimu, na Lukio, Yasoni na Sospeter, jamaa zangu.
22 I Tertius, who wrote this letter, salute you in the Lord.
Mimi, Tertio, niliyeuandika waraka huu, nawasalimu katika jina la Bwana.
23 Gaius my host, and of the whole church, salutes you. Erastus the chamberlain of the city salutes you, and Quartus a brother.
Gayo, aliyenitunza na kwa kanisa lote, lawasalimu. Erasto, mtunza hazina wa mji, awasalimu, pamoja na Kwarto aliye ndugu.
24 The grace of our Lord Jesus Christ be with you all. Amen.
(Zingatia: Katika nakala halisi za kwanza, mstari huu haupo. Tazama Warumi 16: 20. “Neema ya Bwana Yesu Kristo ikae nanyi nyote. Amina.”)
25 Now to him that is of power to establish you according to my gospel, and the preaching of Jesus Christ, according to the revelation of the mystery, which was kept secret since the world began, (aiōnios g166)
Sasa kwake yeye aliye na uwezo kufanya msimame kulingana na injili na mafundisho ya Yesu Kristo, kulingana na ufunuo wa siri iliyofichwa kwa muda mrefu, (aiōnios g166)
26 But now is made manifest, and by the scriptures of the prophets, according to the commandment of the everlasting God, made known to all nations for the obedience of faith: (aiōnios g166)
lakini sasa imekwisha funuliwa na kufanywa kujulikana na maandiko ya unabii kulingana na amri ya Mungu wa milele, kwa utii wa imani miongoni mwa mataifa yote? (aiōnios g166)
27 To God only wise, be glory through Jesus Christ for ever. Amen. (aiōn g165)
Kwa Mungu pekee mwenye hekima, kupitia Yesu Kristo, kuwe na utukufu milele yote. Amina (aiōn g165)

< Romans 16 >