< Psalms 80 >
1 Give ear, O Shepherd of Israel, you that lead Joseph like a flock; you that dwell between the cherubim, shine forth.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 Before Ephraim and Benjamin and Manasseh stir up your strength, and come and save us.
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Turn us again, O God, and cause your face to shine; and we shall be saved.
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 O LORD God of hosts, how long will you be angry against the prayer of your people?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 You feed them with the bread of tears; and give them tears to drink in great measure.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 You make us a strife to our neighbors: and our enemies laugh among themselves.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Turn us again, O God of hosts, and cause your face to shine; and we shall be saved.
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 You have brought a vine out of Egypt: you have cast out the heathen, and planted it.
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 You prepared room before it, and did cause it to take deep root, and it filled the land.
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 The hills were covered with the shadow of it, and the boughs thereof were like the goodly cedars.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 She sent out her boughs to the sea, and her branches to the river.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Why have you then broken down her hedges, so that all they which pass by the way do pluck her?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 The boar out of the wood does waste it, and the wild beast of the field does devour it.
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Return, we beseech you, O God of hosts: look down from heaven, and behold, and visit this vine;
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 And the vineyard which your right hand has planted, and the branch that you made strong for yourself.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 It is burned with fire, it is cut down: they perish at the rebuke of your countenance.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Let your hand be on the man of your right hand, on the son of man whom you made strong for yourself.
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 So will not we go back from you: quicken us, and we will call on your name.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Turn us again, O LORD God of hosts, cause your face to shine; and we shall be saved.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.