< Psalms 56 >
1 Be merciful to me, O God: for man would swallow me up; he fighting daily oppresses me.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
2 My enemies would daily swallow me up: for they be many that fight against me, O you most High.
Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
3 What time I am afraid, I will trust in you.
Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
4 In God I will praise his word, in God I have put my trust; I will not fear what flesh can do to me.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
5 Every day they wrest my words: all their thoughts are against me for evil.
Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
6 They gather themselves together, they hide themselves, they mark my steps, when they wait for my soul.
Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
7 Shall they escape by iniquity? in your anger cast down the people, O God.
Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
8 You tell my wanderings: put you my tears into your bottle: are they not in your book?
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9 When I cry to you, then shall my enemies turn back: this I know; for God is for me.
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10 In God will I praise his word: in the LORD will I praise his word.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11 In God have I put my trust: I will not be afraid what man can do to me.
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12 Your vows are on me, O God: I will render praises to you.
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13 For you have delivered my soul from death: will not you deliver my feet from falling, that I may walk before God in the light of the living?
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.