< Psalms 106 >
1 Praise you the LORD. O give thanks to the LORD; for he is good: for his mercy endures for ever.
Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Who can utter the mighty acts of the LORD? who can show forth all his praise?
Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
3 Blessed are they that keep judgment, and he that does righteousness at all times.
Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
4 Remember me, O LORD, with the favor that you bore to your people: O visit me with your salvation;
Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
5 That I may see the good of your chosen, that I may rejoice in the gladness of your nation, that I may glory with your inheritance.
Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
6 We have sinned with our fathers, we have committed iniquity, we have done wickedly.
Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
7 Our fathers understood not your wonders in Egypt; they remembered not the multitude of your mercies; but provoked him at the sea, even at the Red sea.
Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
8 Nevertheless he saved them for his name’s sake, that he might make his mighty power to be known.
Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
9 He rebuked the Red sea also, and it was dried up: so he led them through the depths, as through the wilderness.
Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
10 And he saved them from the hand of him that hated them, and redeemed them from the hand of the enemy.
Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
11 And the waters covered their enemies: there was not one of them left.
Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
12 Then believed they his words; they sang his praise.
Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
13 They soon forgot his works; they waited not for his counsel:
Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
14 But lusted exceedingly in the wilderness, and tempted God in the desert.
Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
15 And he gave them their request; but sent leanness into their soul.
Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
16 They envied Moses also in the camp, and Aaron the saint of the LORD.
Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
17 The earth opened and swallowed up Dathan and covered the company of Abiram.
Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
18 And a fire was kindled in their company; the flame burned up the wicked.
Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
19 They made a calf in Horeb, and worshipped the molten image.
Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
20 Thus they changed their glory into the similitude of an ox that eats grass.
Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
21 They forgot God their savior, which had done great things in Egypt;
Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
22 Wondrous works in the land of Ham, and terrible things by the Red sea.
Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
23 Therefore he said that he would destroy them, had not Moses his chosen stood before him in the breach, to turn away his wrath, lest he should destroy them.
Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
24 Yes, they despised the pleasant land, they believed not his word:
Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
25 But murmured in their tents, and listened not to the voice of the LORD.
bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
26 Therefore he lifted up his hand against them, to overthrow them in the wilderness:
Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
27 To overthrow their seed also among the nations, and to scatter them in the lands.
akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
28 They joined themselves also to Baalpeor, and ate the sacrifices of the dead.
Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
29 Thus they provoked him to anger with their inventions: and the plague broke in on them.
Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
30 Then stood up Phinehas, and executed judgment: and so the plague was stayed.
Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
31 And that was counted to him for righteousness to all generations for ever more.
Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
32 They angered him also at the waters of strife, so that it went ill with Moses for their sakes:
Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
33 Because they provoked his spirit, so that he spoke unadvisedly with his lips.
Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
34 They did not destroy the nations, concerning whom the LORD commanded them:
Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
35 But were mingled among the heathen, and learned their works.
bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
36 And they served their idols: which were a snare to them.
nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
37 Yes, they sacrificed their sons and their daughters to devils,
Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
38 And shed innocent blood, even the blood of their sons and of their daughters, whom they sacrificed to the idols of Canaan: and the land was polluted with blood.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
39 Thus were they defiled with their own works, and went a whoring with their own inventions.
Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
40 Therefore was the wrath of the LORD kindled against his people, so that he abhorred his own inheritance.
Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
41 And he gave them into the hand of the heathen; and they that hated them ruled over them.
Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
42 Their enemies also oppressed them, and they were brought into subjection under their hand.
Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
43 Many times did he deliver them; but they provoked him with their counsel, and were brought low for their iniquity.
Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
44 Nevertheless he regarded their affliction, when he heard their cry:
Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
45 And he remembered for them his covenant, and repented according to the multitude of his mercies.
Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
46 He made them also to be pitied of all those that carried them captives.
Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
47 Save us, O LORD our God, and gather us from among the heathen, to give thanks to your holy name, and to triumph in your praise.
Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
48 Blessed be the LORD God of Israel from everlasting to everlasting: and let all the people say, Amen. Praise you the LORD.
Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.