< Proverbs 27 >
1 Boast not yourself of to morrow; for you know not what a day may bring forth.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Let another man praise you, and not your own mouth; a stranger, and not your own lips.
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 A stone is heavy, and the sand weighty; but a fool’s wrath is heavier than them both.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 Wrath is cruel, and anger is outrageous; but who is able to stand before envy?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Open rebuke is better than secret love.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Faithful are the wounds of a friend; but the kisses of an enemy are deceitful.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 The full soul loathes an honeycomb; but to the hungry soul every bitter thing is sweet.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 As a bird that wanders from her nest, so is a man that wanders from his place.
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 Ointment and perfume rejoice the heart: so does the sweetness of a man’s friend by hearty counsel.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 Your own friend, and your father’s friend, forsake not; neither go into your brother’s house in the day of your calamity: for better is a neighbor that is near than a brother far off.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 My son, be wise, and make my heart glad, that I may answer him that reproaches me.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 A prudent man foresees the evil, and hides himself; but the simple pass on, and are punished.
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Take his garment that is surety for a stranger, and take a pledge of him for a strange woman.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 He that blesses his friend with a loud voice, rising early in the morning, it shall be counted a curse to him.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 A continual dropping in a very rainy day and a contentious woman are alike.
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 Whoever hides her hides the wind, and the ointment of his right hand, which denudes itself.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 Iron sharpens iron; so a man sharpens the countenance of his friend.
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 Whoever keeps the fig tree shall eat the fruit thereof: so he that waits on his master shall be honored.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 As in water face answers to face, so the heart of man to man.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 Hell and destruction are never full; so the eyes of man are never satisfied. (Sheol )
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol )
21 As the fining pot for silver, and the furnace for gold; so is a man to his praise.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Though you should bray a fool in a mortar among wheat with a pestle, yet will not his foolishness depart from him.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Be you diligent to know the state of your flocks, and look well to your herds.
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 For riches are not for ever: and does the crown endure to every generation?
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 The hay appears, and the tender grass shows itself, and herbs of the mountains are gathered.
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 The lambs are for your clothing, and the goats are the price of the field.
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 And you shall have goats’ milk enough for your food, for the food of your household, and for the maintenance for your maidens.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.