< Micah 5 >
1 Now gather yourself in troops, O daughter of troops: he has laid siege against us: they shall smite the judge of Israel with a rod on the cheek.
Panga majeshi yako, ee mji wa majeshi, kwa kuwa kuzingirwa kumepangwa dhidi yetu. Watampiga mtawala wa Israeli shavuni kwa fimbo.
2 But you, Bethlehem Ephratah, though you be little among the thousands of Judah, yet out of you shall he come forth to me that is to be ruler in Israel; whose goings forth have been from of old, from everlasting.
“Lakini wewe, Bethlehemu Efrathi, ingawa u mdogo miongoni mwa koo za Yuda, kutoka kwako atatokea kwa ajili yangu yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli, ambaye asili yake ni kutoka zamani, kutoka milele.”
3 Therefore will he give them up, until the time that she which travails has brought forth: then the remnant of his brothers shall return to the children of Israel.
Kwa hiyo Israeli utaachwa mpaka wakati mwanamke aliye na utungu atakapozaa na ndugu zake wengine warudi kujiunga na Waisraeli.
4 And he shall stand and feed in the strength of the LORD, in the majesty of the name of the LORD his God; and they shall abide: for now shall he be great to the ends of the earth.
Atasimama na kulichunga kundi lake katika nguvu ya Bwana, katika utukufu wa jina la Bwana Mungu wake. Nao wataishi kwa usalama, kwa kuwa wakati huo ukuu wake utaenea hadi miisho ya dunia.
5 And this man shall be the peace, when the Assyrian shall come into our land: and when he shall tread in our palaces, then shall we raise against him seven shepherds, and eight principal men.
Naye atakuwa amani yao. Wakati Mwashuru atakapovamia nchi yetu na kupita katika ngome zetu, tutawainua wachungaji saba dhidi yake, hata viongozi wanane wa watu.
6 And they shall waste the land of Assyria with the sword, and the land of Nimrod in the entrances thereof: thus shall he deliver us from the Assyrian, when he comes into our land, and when he treads within our borders.
Wataitawala nchi ya Ashuru kwa upanga, nchi ya Nimrodi kwa upanga. Atatuokoa kutoka kwa Mwashuru atakapoivamia nchi yetu na kuingia katika mipaka yetu.
7 And the remnant of Jacob shall be in the middle of many people as a dew from the LORD, as the showers on the grass, that tarries not for man, nor waits for the sons of men.
Mabaki ya Yakobo yatakuwa katikati ya mataifa mengi kama umande kutoka kwa Bwana, kama manyunyu juu ya majani, ambayo hayamngoji mtu wala kukawia kwa mwanadamu.
8 And the remnant of Jacob shall be among the Gentiles in the middle of many people as a lion among the beasts of the forest, as a young lion among the flocks of sheep: who, if he go through, both treads down, and tears in pieces, and none can deliver.
Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa, katikati ya mataifa mengi, kama simba miongoni mwa wanyama wa msituni, kama mwana simba miongoni mwa makundi ya kondoo, ambaye anaumiza vibaya na kuwararua kila anapopita katikati yao, wala hakuna awezaye kuokoa.
9 Your hand shall be lifted up on your adversaries, and all your enemies shall be cut off.
Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako, nao adui zako wote wataangamizwa.
10 And it shall come to pass in that day, says the LORD, that I will cut off your horses out of the middle of you, and I will destroy your chariots:
“Katika siku ile,” asema Bwana, “nitaangamiza farasi zenu katikati yenu na kubomoa magari yenu ya vita.
11 And I will cut off the cities of your land, and throw down all your strong holds:
Nitaiangamiza miji ya nchi yenu na kuziangusha chini ngome zenu zote.
12 And I will cut off witchcrafts out of your hand; and you shall have no more soothsayers:
Nitaangamiza uchawi wenu na hamtapiga tena ramli.
13 Your graven images also will I cut off, and your standing images out of the middle of you; and you shall no more worship the work of your hands.
Nitaangamiza vinyago vyenu vya kuchonga na mawe yenu ya ibada yatoke katikati yenu; hamtasujudia tena kazi ya mikono yenu.
14 And I will pluck up your groves out of the middle of you: so will I destroy your cities.
Nitangʼoa nguzo za Ashera katikati yenu na kubomoa miji yenu.
15 And I will execute vengeance in anger and fury on the heathen, such as they have not heard.
Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayajanitii.”