< John 11 >

1 Now a certain man was sick, named Lazarus, of Bethany, the town of Mary and her sister Martha.
Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
2 (It was that Mary which anointed the Lord with ointment, and wiped his feet with her hair, whose brother Lazarus was sick.)
Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
3 Therefore his sisters sent to him, saying, Lord, behold, he whom you love is sick.
Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!”
4 When Jesus heard that, he said, This sickness is not to death, but for the glory of God, that the Son of God might be glorified thereby.
Yesu aliposikia hivyo akasema, “Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe.”
5 Now Jesus loved Martha, and her sister, and Lazarus.
Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
6 When he had heard therefore that he was sick, he stayed two days still in the same place where he was.
Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
7 Then after that says he to his disciples, Let us go into Judaea again.
Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Twendeni tena Yudea!”
8 His disciples say to him, Master, the Jews of late sought to stone you; and go you thither again?
Wanafunzi wakamwambia, “Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?”
9 Jesus answered, Are there not twelve hours in the day? If any man walk in the day, he stumbles not, because he sees the light of this world.
Yesu akajibu, “Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
10 But if a man walk in the night, he stumbles, because there is no light in him.
Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.”
11 These things said he: and after that he says to them, Our friend Lazarus sleeps; but I go, that I may awake him out of sleep.
Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.”
12 Then said his disciples, Lord, if he sleep, he shall do well.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
13 However, Jesus spoke of his death: but they thought that he had spoken of taking of rest in sleep.
Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
14 Then said Jesus to them plainly, Lazarus is dead.
Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
15 And I am glad for your sakes that I was not there, to the intent you may believe; nevertheless let us go to him.
Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
16 Then said Thomas, which is called Didymus, to his fellow disciples, Let us also go, that we may die with him.
Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
17 Then when Jesus came, he found that he had lain in the grave four days already.
Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
18 Now Bethany was near to Jerusalem, about fifteen furlongs off:
Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
19 And many of the Jews came to Martha and Mary, to comfort them concerning their brother.
Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
20 Then Martha, as soon as she heard that Jesus was coming, went and met him: but Mary sat still in the house.
Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
21 Then said Martha to Jesus, Lord, if you had been here, my brother had not died.
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
22 But I know, that even now, whatever you will ask of God, God will give it you.
Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 Jesus says to her, Your brother shall rise again.
Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.”
24 Martha says to him, I know that he shall rise again in the resurrection at the last day.
Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.”
25 Jesus said to her, I am the resurrection, and the life: he that believes in me, though he were dead, yet shall he live:
Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
26 And whoever lives and believes in me shall never die. Believe you this? (aiōn g165)
na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” (aiōn g165)
27 She says to him, Yes, Lord: I believe that you are the Christ, the Son of God, which should come into the world.
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”
28 And when she had so said, she went her way, and called Mary her sister secretly, saying, The Master is come, and calls for you.
Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, “Mwalimu yuko hapa, anakuita.”
29 As soon as she heard that, she arose quickly, and came to him.
Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
30 Now Jesus was not yet come into the town, but was in that place where Martha met him.
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
31 The Jews then which were with her in the house, and comforted her, when they saw Mary, that she rose up hastily and went out, followed her, saying, She goes to the grave to weep there.
Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
32 Then when Mary was come where Jesus was, and saw him, she fell down at his feet, saying to him, Lord, if you had been here, my brother had not died.
Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!”
33 When Jesus therefore saw her weeping, and the Jews also weeping which came with her, he groaned in the spirit, and was troubled.
Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
34 And said, Where have you laid him? They said to him, Lord, come and see.
Kisha akawauliza, “Mlimweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo uone.”
35 Jesus wept.
Yesu akalia machozi.
36 Then said the Jews, Behold how he loved him!
Basi, Wayahudi wakasema, “Tazameni jinsi alivyompenda!”
37 And some of them said, Could not this man, which opened the eyes of the blind, have caused that even this man should not have died?
Lakini baadhi yao wakasema, “Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?”
38 Jesus therefore again groaning in himself comes to the grave. It was a cave, and a stone lay on it.
Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
39 Jesus says, Take you away the stone. Martha, the sister of him that was dead, said to him, Lord, by this time he stinks: for he has been dead four days.
Yesu akasema, “Ondoeni hilo jiwe!” Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, “Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!”
40 Jesus says to her, Said I not to you, that, if you would believe, you should see the glory of God?
Yesu akamwambia, “Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”
41 Then they took away the stone from the place where the dead was laid. And Jesus lifted up his eyes, and said, Father, I thank you that you have heard me.
Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, “Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
42 And I knew that you hear me always: but because of the people which stand by I said it, that they may believe that you have sent me.
Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
43 And when he thus had spoken, he cried with a loud voice, Lazarus, come forth.
Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro! Toka nje!”
44 And he that was dead came forth, bound hand and foot with grave clothes: and his face was bound about with a napkin. Jesus says to them, Loose him, and let him go.
Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mkamwache aende zake.”
45 Then many of the Jews which came to Mary, and had seen the things which Jesus did, believed on him.
Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
46 But some of them went their ways to the Pharisees, and told them what things Jesus had done.
Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
47 Then gathered the chief priests and the Pharisees a council, and said, What do we? for this man does many miracles.
kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, “Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
48 If we let him thus alone, all men will believe on him: and the Romans shall come and take away both our place and nation.
Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!”
49 And one of them, named Caiaphas, being the high priest that same year, said to them, You know nothing at all,
Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Ninyi hamjui kitu!
50 Nor consider that it is expedient for us, that one man should die for the people, and that the whole nation perish not.
Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?”
51 And this spoke he not of himself: but being high priest that year, he prophesied that Jesus should die for that nation;
Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
52 And not for that nation only, but that also he should gather together in one the children of God that were scattered abroad.
na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
53 Then from that day forth they took counsel together for to put him to death.
Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
54 Jesus therefore walked no more openly among the Jews; but went there to a country near to the wilderness, into a city called Ephraim, and there continued with his disciples.
Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
55 And the Jews’ passover was near at hand: and many went out of the country up to Jerusalem before the passover, to purify themselves.
Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
56 Then sought they for Jesus, and spoke among themselves, as they stood in the temple, What think you, that he will not come to the feast?
Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, “Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?”
57 Now both the chief priests and the Pharisees had given a commandment, that, if any man knew where he were, he should show it, that they might take him.
Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.

< John 11 >