< Job 14 >

1 Man that is born of a woman is of few days and full of trouble.
Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
2 He comes forth like a flower, and is cut down: he flees also as a shadow, and continues not.
Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
3 And does you open your eyes on such an one, and bring me into judgment with you?
Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
4 Who can bring a clean thing out of an unclean? not one.
Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
5 Seeing his days are determined, the number of his months are with you, you have appointed his bounds that he cannot pass;
Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
6 Turn from him, that he may rest, till he shall accomplish, as an hireling, his day.
Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
7 For there is hope of a tree, if it be cut down, that it will sprout again, and that the tender branch thereof will not cease.
Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
8 Though the root thereof wax old in the earth, and the stock thereof die in the ground;
Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
9 Yet through the scent of water it will bud, and bring forth boughs like a plant.
hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
10 But man dies, and wastes away: yes, man gives up the ghost, and where is he?
Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
11 As the waters fail from the sea, and the flood decays and dries up:
Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
12 So man lies down, and rises not: till the heavens be no more, they shall not awake, nor be raised out of their sleep.
vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
13 O that you would hide me in the grave, that you would keep me secret, until your wrath be past, that you would appoint me a set time, and remember me! (Sheol h7585)
Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol h7585)
14 If a man die, shall he live again? all the days of my appointed time will I wait, till my change come.
Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
15 You shall call, and I will answer you: you will have a desire to the work of your hands.
Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
16 For now you number my steps: do you not watch over my sin?
Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
17 My transgression is sealed up in a bag, and you sew up my iniquity.
Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
18 And surely the mountains falling comes to nothing, and the rock is removed out of his place.
Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
19 The waters wear the stones: you wash away the things which grow out of the dust of the earth; and you destroy the hope of man.
maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
20 You prevail for ever against him, and he passes: you change his countenance, and send him away.
Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
21 His sons come to honor, and he knows it not; and they are brought low, but he perceives it not of them.
Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
22 But his flesh on him shall have pain, and his soul within him shall mourn.
Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.

< Job 14 >