< Job 12 >

1 And Job answered and said,
Ndipo Ayubu akajibu:
2 No doubt but you are the people, and wisdom shall die with you.
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 But I have understanding as well as you; I am not inferior to you: yes, who knows not such things as these?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 I am as one mocked of his neighbor, who calls on God, and he answers him: the just upright man is laughed to scorn.
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 He that is ready to slip with his feet is as a lamp despised in the thought of him that is at ease.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 The tabernacles of robbers prosper, and they that provoke God are secure; into whose hand God brings abundantly.
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 But ask now the beasts, and they shall teach you; and the fowls of the air, and they shall tell you:
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 Or speak to the earth, and it shall teach you: and the fishes of the sea shall declare to you.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 Who knows not in all these that the hand of the LORD has worked this?
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 In whose hand is the soul of every living thing, and the breath of all mankind.
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 Does not the ear try words? and the mouth taste his meat?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 With the ancient is wisdom; and in length of days understanding.
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 With him is wisdom and strength, he has counsel and understanding.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 Behold, he breaks down, and it cannot be built again: he shuts up a man, and there can be no opening.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 Behold, he withholds the waters, and they dry up: also he sends them out, and they overturn the earth.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 With him is strength and wisdom: the deceived and the deceiver are his.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 He leads counsellors away spoiled, and makes the judges fools.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 He looses the bond of kings, and girds their loins with a girdle.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 He leads princes away spoiled, and overthrows the mighty.
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 He removes away the speech of the trusty, and takes away the understanding of the aged.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 He pours contempt on princes, and weakens the strength of the mighty.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 He discovers deep things out of darkness, and brings out to light the shadow of death.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 He increases the nations, and destroys them: he enlarges the nations, and straitens them again.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 He takes away the heart of the chief of the people of the earth, and causes them to wander in a wilderness where there is no way.
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 They grope in the dark without light, and he makes them to stagger like a drunken man.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.

< Job 12 >