< Genesis 31 >
1 And he heard the words of Laban’s sons, saying, Jacob has taken away all that was our father’s; and of that which was our father’s has he gotten all this glory.
Yakobo akawasikia wana wa Labani wakisema, “Yakobo amechukua kila kitu kilichokuwa cha baba yetu naye amepata utajiri huu wote kutokana na vile vilivyokuwa mali ya baba yetu.”
2 And Jacob beheld the countenance of Laban, and, behold, it was not toward him as before.
Yakobo akatambua kwamba moyo wa Labani kwake haukuwa kama ulivyokuwa mwanzo.
3 And the LORD said to Jacob, Return to the land of your fathers, and to your kindred; and I will be with you.
Ndipo Bwana akamwambia Yakobo, “Rudi katika nchi ya baba zako na kwa watu wako, nami nitakuwa pamoja nawe.”
4 And Jacob sent and called Rachel and Leah to the field to his flock,
Hivyo Yakobo akatuma ujumbe kwa Raheli na Lea waje machungani yalikokuwa makundi yake.
5 And said to them, I see your father’s countenance, that it is not toward me as before; but the God of my father has been with me.
Akawaambia, “Naona moyo wa baba yenu kwangu sivyo kama ulivyokuwa mwanzoni, lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami.
6 And you know that with all my power I have served your father.
Mnajua kwamba nimemtumikia baba yenu kwa nguvu zangu zote,
7 And your father has deceived me, and changed my wages ten times; but God suffered him not to hurt me.
hata hivyo baba yenu amenidanganya kwa kubadilisha ujira wangu mara kumi. Hata hivyo, Mungu hakumruhusu kunidhuru.
8 If he said thus, The speckled shall be your wages; then all the cattle bore speckled: and if he said thus, The ringstraked shall be your hire; then bore all the cattle ringstraked.
Kama alisema, ‘Wenye madoadoa watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye madoadoa, kama alisema, ‘Wenye mistari watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye mistari.
9 Thus God has taken away the cattle of your father, and given them to me.
Hivyo Mungu amechukua mifugo ya baba yenu na amenipa mimi.
10 And it came to pass at the time that the cattle conceived, that I lifted up my eyes, and saw in a dream, and, behold, the rams which leaped on the cattle were ringstraked, speckled, and spotted.
“Wakati fulani majira ya kuzaliana niliota ndoto ambayo niliinua macho na kuona kwamba wale mabeberu waliokuwa wakipanda kundi walikuwa wa mistari, madoadoa na mabakabaka.
11 And the angel of God spoke to me in a dream, saying, Jacob: And I said, Here am I.
Malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, ‘Yakobo.’ Nikamjibu, ‘Mimi hapa.’
12 And he said, Lift up now your eyes, and see, all the rams which leap on the cattle are ringstraked, speckled, and spotted: for I have seen all that Laban does to you.
Akasema, ‘Inua macho yako uone wale mabeberu wote wanaopanda kundi wana mistari, madoadoa au mabakabaka, kwa maana nimeona yale yote ambayo Labani amekuwa akikutendea.
13 I am the God of Bethel, where you anointed the pillar, and where you vowed a vow to me: now arise, get you out from this land, and return to the land of your kindred.
Mimi ndiye Mungu wa Betheli, ulikomiminia ile nguzo mafuta na pale mahali uliponiwekea nadhiri. Sasa ondoka katika nchi hii mara moja urudi katika nchi uliyozaliwa.’”
14 And Rachel and Leah answered and said to him, Is there yet any portion or inheritance for us in our father’s house?
Ndipo Raheli na Lea wakajibu, “Je bado tu tunalo fungu lolote katika urithi wa nyumba ya baba yetu?
15 Are we not counted of him strangers? for he has sold us, and has quite devoured also our money.
Je, yeye hatuhesabu sisi kama wageni? Sio kwamba ametuuza tu, bali ametumia hata na vile vilivyolipwa kwa ajili yetu.
16 For all the riches which God has taken from our father, that is ours, and our children’s: now then, whatever God has said to you, do.
Hakika utajiri wote ambao Mungu ameuchukua kutoka kwa baba yetu ni mali yetu na watoto wetu. Hivyo fanya lolote lile Mungu alilokuambia.”
17 Then Jacob rose up, and set his sons and his wives on camels;
Ndipo Yakobo akawapandisha watoto wake na wake zake juu ya ngamia,
18 And he carried away all his cattle, and all his goods which he had gotten, the cattle of his getting, which he had gotten in Padanaram, for to go to Isaac his father in the land of Canaan.
naye akawaswaga wanyama wote mbele yake pamoja na vitu vyote alivyokuwa amechuma huko Padan-Aramu kwenda kwa baba yake Isaki katika nchi ya Kanaani.
19 And Laban went to shear his sheep: and Rachel had stolen the images that were her father’s.
Labani alipokuwa amekwenda kukata kondoo wake manyoya, Raheli aliiba miungu ya nyumba ya baba yake.
20 And Jacob stole away unawares to Laban the Syrian, in that he told him not that he fled.
Zaidi ya hayo, Yakobo alimdanganya Labani Mwaramu kwa kutokumwambia kwamba anakimbia.
21 So he fled with all that he had; and he rose up, and passed over the river, and set his face toward the mount Gilead.
Hivyo akakimbia pamoja na vitu vyote alivyokuwa navyo na kuvuka Mto Frati akaelekea nchi ya vilima katika Gileadi.
22 And it was told Laban on the third day that Jacob was fled.
Siku ya tatu Labani akaambiwa kwamba Yakobo amekimbia.
23 And he took his brothers with him, and pursued after him seven days’ journey; and they overtook him in the mount Gilead.
Akiwachukua jamaa zake, akamfuatia Yakobo kwa siku saba na kumkuta kwenye nchi ya vilima katika Gileadi.
24 And God came to Laban the Syrian in a dream by night, and said to him, Take heed that you speak not to Jacob either good or bad.
Ndipo Mungu akamjia Labani Mwaramu katika ndoto usiku na kumwambia, “Jihadhari usiseme neno lolote kwa Yakobo, liwe zuri au baya.”
25 Then Laban overtook Jacob. Now Jacob had pitched his tent in the mount: and Laban with his brothers pitched in the mount of Gilead.
Yakobo alikuwa amepiga hema lake katika nchi ya vilima katika Gileadi wakati Labani alipomkuta, Labani na jamaa yake wakapiga kambi huko pia.
26 And Laban said to Jacob, What have you done, that you have stolen away unawares to me, and carried away my daughters, as captives taken with the sword?
Ndipo Labani akamwambia Yakobo, “Umefanya nini? Umenidanganya na umewachukua binti zangu kama mateka katika vita.
27 Why did you flee away secretly, and steal away from me; and did not tell me, that I might have sent you away with mirth, and with songs, with tabret, and with harp?
Kwa nini ulikimbia kwa siri na kunidanganya? Kwa nini hukuniambia ili nikuage kwa furaha na nyimbo za matari na vinubi?
28 And have not suffered me to kiss my sons and my daughters? you have now done foolishly in so doing.
Hata hukuniruhusu niwabusu wajukuu zangu na kuwaaga binti zangu. Umefanya kitu cha kipumbavu.
29 It is in the power of my hand to do you hurt: but the God of your father spoke to me last night, saying, Take you heed that you speak not to Jacob either good or bad.
Nina uwezo wa kukudhuru, lakini usiku uliopita Mungu wa baba yako alisema nami, akaniambia, ‘Jihadhari, usiseme neno lolote kwa Yakobo liwe zuri au baya.’
30 And now, though you would needs be gone, because you sore longed after your father’s house, yet why have you stolen my gods?
Sasa umeondoka kwa sababu umetamani kurudi nyumbani kwa baba yako. Lakini kwa nini umeiba miungu yangu?”
31 And Jacob answered and said to Laban, Because I was afraid: for I said, Peradventure you would take by force your daughters from me.
Yakobo akamjibu Labani, “Niliogopa, kwa sababu nilifikiri ungeweza kuninyangʼanya binti zako kwa nguvu.
32 With whomsoever you find your gods, let him not live: before our brothers discern you what is your with me, and take it to you. For Jacob knew not that Rachel had stolen them.
Lakini kama ukimkuta yeyote aliye na miungu yako, hataishi. Mbele ya jamaa yetu, angalia mwenyewe uone kama kuna chochote chako hapa nilicho nacho, kama kipo, kichukue.” Basi Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameiba hiyo miungu.
33 And Laban went into Jacob’s tent, and into Leah’s tent, and into the two maidservants’ tents; but he found them not. Then went he out of Leah’s tent, and entered into Rachel’s tent.
Kwa hiyo Labani akaingia ndani ya hema la Yakobo na ndani ya hema la Lea na ndani ya hema la watumishi wawili wa kike, lakini hakukuta chochote. Baadaye alipotoka katika hema la Lea, akaingia hema la Raheli.
34 Now Rachel had taken the images, and put them in the camel’s furniture, and sat on them. And Laban searched all the tent, but found them not.
Basi Raheli ndiye alikuwa amechukua ile miungu ya nyumbani kwao na kuiweka katika matandiko ya ngamia na kukalia. Labani akatafuta kila mahali kwenye hema lakini hakupata chochote.
35 And she said to her father, Let it not displease my lord that I cannot rise up before you; for the custom of women is on me. And he searched but found not the images.
Raheli akamwambia baba yake, “Usikasirike, bwana wangu kwa kuwa siwezi kusimama ukiwepo, niko katika hedhi.” Labani akatafuta lakini hakuweza kuipata miungu ya nyumbani kwake.
36 And Jacob was wroth, and strived with Laban: and Jacob answered and said to Laban, What is my trespass? what is my sin, that you have so hotly pursued after me?
Yakobo akakasirika na kumshutumu Labani, akisema, “Uhalifu wangu ni nini?” Akamuuliza Labani, “Ni dhambi gani niliyofanya hata unaniwinda?
37 Whereas you have searched all my stuff, what have you found of all your household stuff? set it here before my brothers and your brothers, that they may judge between us both.
Sasa kwa kuwa umepekua vitu vyangu vyote umepata nini kilicho cha nyumbani mwako? Kiweke hapa mbele ya jamaa yako na yangu, nao waamue kati yetu sisi wawili.
38 This twenty years have I been with you; your ewes and your she goats have not cast their young, and the rams of your flock have I not eaten.
“Mpaka sasa nimekuwa pamoja nawe miaka ishirini. Kondoo wako na mbuzi wako hawajaharibu mimba, wala sijala kondoo dume kutoka makundi yako.
39 That which was torn of beasts I brought not to you; I bore the loss of it; of my hand did you require it, whether stolen by day, or stolen by night.
Sikukuletea mfugo aliyeraruliwa na wanyama pori, nilibeba hasara mimi mwenyewe. Tena ulinidai malipo kwa chochote kilichoibwa mchana au usiku.
40 Thus I was; in the day the drought consumed me, and the frost by night; and my sleep departed from my eyes.
Hii ndiyo iliyokuwa hali yangu: Niliumia kwa joto la mchana na baridi usiku, pia usingizi ulinipa.
41 Thus have I been twenty years in your house; I served you fourteen years for your two daughters, and six years for your cattle: and you have changed my wages ten times.
Ilikuwa hivi kwa miaka ile ishirini niliyokuwa nyumbani kwako. Nilikutumikia miaka ile kumi na minne kwa ajili ya binti zako wawili, miaka sita kwa ajili ya makundi yako, nawe ulibadilisha ujira wangu mara kumi.
42 Except the God of my father, the God of Abraham, and the fear of Isaac, had been with me, surely you had sent me away now empty. God has seen my affliction and the labor of my hands, and rebuked you last night.
Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Abrahamu na Hofu ya Isaki, hakuwa pamoja nami, hakika ungenifukuza mikono mitupu. Lakini Mungu ameona taabu yangu na kazi ngumu ya mikono yangu, naye usiku uliopita amekukemea.”
43 And Laban answered and said to Jacob, These daughters are my daughters, and these children are my children, and these cattle are my cattle, and all that you see is mine: and what can I do this day to these my daughters, or to their children which they have born?
Labani akamjibu Yakobo, “Wanawake hawa ni binti zangu, watoto hawa ni watoto wangu na makundi haya ni makundi yangu. Vyote unavyoviona ni vyangu. Lakini hata hivyo ninaweza kufanya nini kuhusu hawa binti zangu, au kuhusu watoto waliowazaa?
44 Now therefore come you, let us make a covenant, I and you; and let it be for a witness between me and you.
Njoo sasa na tufanye agano, wewe na mimi, na liwe kama shahidi kati yetu.”
45 And Jacob took a stone, and set it up for a pillar.
Hivyo Yakobo akachukua jiwe, akalisimamisha kama nguzo.
46 And Jacob said to his brothers, Gather stones; and they took stones, and made an heap: and they did eat there on the heap.
Akawaambia jamaa yake, “Kusanyeni mawe.” Hivyo wakachukua mawe na kuyakusanya yakawa lundo, wakala chakula hapo karibu na hilo lundo.
47 And Laban called it Jegarsahadutha: but Jacob called it Galeed.
Labani akaliita Yegar-Sahadutha na Yakobo akaliita Galeedi.
48 And Laban said, This heap is a witness between me and you this day. Therefore was the name of it called Galeed;
Labani akasema, “Lundo hili ni shahidi kati yako na mimi leo.” Ndiyo maana likaitwa Galeedi.
49 And Mizpah; for he said, The LORD watch between me and you, when we are absent one from another.
Pia liliitwa Mispa, kwa sababu alisema, “Bwana na aweke ulinzi kati yako na mimi wakati kila mmoja akiwa mbali na mwingine.
50 If you shall afflict my daughters, or if you shall take other wives beside my daughters, no man is with us; see, God is witness between me and you.
Kama ukiwatenda mabaya binti zangu au ukioa wake wengine zaidi ya binti zangu, hata ingawa hakuna hata mmoja aliye pamoja nasi, kumbuka kwamba Mungu ni shahidi kati yako na mimi.”
51 And Laban said to Jacob, Behold this heap, and behold this pillar, which I have cast between me and you:
Pia Labani akamwambia Yakobo, “Hili ndilo lundo, na hii ndiyo nguzo niliyoisimamisha kati yako na mimi.
52 This heap be witness, and this pillar be witness, that I will not pass over this heap to you, and that you shall not pass over this heap and this pillar to me, for harm.
Lundo hili ni shahidi na nguzo hii ni shahidi, kwamba sitavuka lundo hili kuja upande wako kukudhuru, nawe kwamba hutavuka lundo hili na nguzo hii kuja upande wangu kunidhuru.
53 The God of Abraham, and the God of Nahor, the God of their father, judge between us. And Jacob swore by the fear of his father Isaac.
Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Nahori, Mungu wa baba zao, aamue kati yetu.” Hivyo Yakobo akaapa kwa jina la Hofu ya baba yake Isaki.
54 Then Jacob offered sacrifice on the mount, and called his brothers to eat bread: and they did eat bread, and tarried all night in the mount.
Yakobo akatoa dhabihu juu ya kilima na akawaalika jamaa zake kula chakula. Baada ya kula, wakalala huko.
55 And early in the morning Laban rose up, and kissed his sons and his daughters, and blessed them: and Laban departed, and returned to his place.
Kesho yake asubuhi na mapema, Labani akawabusu wajukuu zake, binti zake na kuwabariki. Kisha akaondoka, akarudi nyumbani.