< Ruth 1 >

1 AND IT came to pass in the days when the judges judged, that there was a famine in the land. And a certain man of Beth-lehem in Judah went to sojourn in the field of Moab, he, and his wife, and his two sons.
Ilitokea katika siku za utawala wa majaji kuwa kulikuwa na njaa katika nchi, na mtu mmoja wa Bethelehemu ya Yuda alikwenda katika nchi ya Moabu pamoja na mke wake na watoto wake walili wa kiume.
2 And the name of the man was Elimelech, and the name of his wife Naomi, and the name of his two sons Mahlon and Chilion, Ephrathites of Beth-lehem in Judah. And they came into the field of Moab, and continued there.
Jina la mtu huyo lilikuwa Elimeleki, na jina la mke wake lilikuwa Naomi. Majina ya watoto wake wawili wa kiume waliitwa Mahiloni na Kileoni, ambao walikuwa Waefraimu wa Betherehemu ya Yuda. Waliwasili katika nchi ya Moabu na kuishi hapo.
3 And Elimelech Naomi's husband died; and she was left, and her two sons.
Ndipo Elimeleki, mume wa Naomi, alikufa, na Naomi aliachwa na watoto wake wa kiume wawili.
4 And they took them wives of the women of Moab: the name of the one was Orpah, and the name of the other Ruth; and they dwelt there about ten years.
Watoto hawa walioa wanawake wa Moabu; jina la mmoja lilikuwa Oripa, na jina la mwingine lilikuwa Ruth. waliishi huko kwa takribani miaka kumi.
5 And Mahlon and Chilion died both of them; and the woman was left of her two children and of her husband.
Kisha wote Mahiloni na Kileoni walikufa, na kumuacha Naomi bila mme wake na bila watoto wake wawili.
6 Then she arose with her daughters-in-law, that she might return from the field of Moab; for she had heard in the field of Moab how that the LORD had remembered His people in giving them bread.
Ndipo Naomi aliamua kuondoka Moabu pamoja na wake wa watoto wake na kurudi Yuda kwa sababu alikuwa amesikia katika mkoa wa Moabu kuwa Yahweh amewasaidia watu wake katika uhitaji na amewapa chakula.
7 And she went forth out of the place where she was, and her two daughters-in-law with her; and they went on the way to return unto the land of Judah.
Hivyo aliondoka sehemu aliyokuwa pamoja na wake wa watoto wake wawili, walitelemka njia kurudi kwenye nchi ya Yuda.
8 And Naomi said unto her two daughters-in-law: 'Go, return each of you to her mother's house; the LORD deal kindly with you, as ye have dealt with the dead, and with me.
Naomi aliwaambia wake wa watoto wake, “Nendeni, mrudi, kila mmoja wenu, kwenye nyumba ya mama yake. na Mungu aonyeshe wema juu yenu, kama mlivyo onyesha wema kwao waliokufa na kwangu.
9 The LORD grant you that ye may find rest, each of you in the house of her husband.' Then she kissed them; and they lifted up their voice, and wept.
Mungu awajalie ninyi kupata pumziko, kila mmoja wenu katika nyumba ya mme mwingine.” Kisha akawabusu, na wakapaza sauti zao na kulia.
10 And they said unto her: 'Nay, but we will return with thee unto thy people.'
Wakamwambia, “Hapana! tutarudi pamoja na wewe kwa watu wako.”
11 And Naomi said: 'Turn back, my daughters; why will ye go with me? have I yet sons in my womb, that they may be your husbands?
Lakini Naomi alisema, “Rudini, wanangu! Kwa nini mtakwenda na mimi? Kwani bado nina watoto katika tumbo langu kwa ajili yenu, ili kwamba waje wawe waume zenu?
12 Turn back, my daughters, go your way; for I am too old to have a husband. If I should say: I have hope, should I even have an husband to-night, and also bear sons;
Rudini, wanangu, nendeni katika njia zenu wenyewe, kwa kuwa mimi ni mzee sana kuwa na mme. Kama nikisema, 'Natumaini nipate mume usiku huu,' na kisha kuzaa watoto wakiume, kwa hiyo mnaweza kusubiri mpaka wakue?
13 would ye tarry for them till they were grown? would ye shut yourselves off for them and have no husbands? nay, my daughters; for it grieveth me much for your sakes, for the hand of the LORD is gone forth against me.'
Mtasubiri na msiolewe sasa? Hapana, wanangu! Ina nihuzunisha zaidi, kuliko inavyo wahuzunisha ninyi, kwa sababu mkono wa Yahweh umeenda kinyume na mimi.”
14 And they lifted up their voice, and wept again; and Orpah kissed her mother-in-law; but Ruth cleaved unto her.
Ndipo wake wa watoto wake wakapaza sauti zao na kulia tena. Oripa alimuaga kwa kumbusu, lakini Ruth aliendelea kubaki naye.
15 And she said: 'Behold, thy sister-in-law is gone back unto her people, and unto her god; return thou after thy sister-in-law.'
Naomi alisema, “sikiliza, mwenzako amerudi kwa watu wake na miungu yake. Ruri pamoja naye.”
16 And Ruth said: 'Entreat me not to leave thee, and to return from following after thee; for whither thou goest, I will go; and where thou lodgest, I will lodge; thy people shall be my people, and thy God my God;
lakini Ruth alisema, “Usiniache niondoke mbali nawe, kwa kuwa uendako, nitakwenda, utakapoishi, nitaishi; watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.
17 where thou diest, will I die, and there will I be buried; the LORD do so to me, and more also, if aught but death part thee and me.'
Mahali utakapofia, nitafia hapo, na hapo nitazikwa. Yahweh aniwezeshe, na hata zaidi, ikiwa kuna chochote isipokuwa kifo kamwe hakiwezi kututenganisha.
18 And when she saw that she was stedfastly minded to go with her, she left off speaking unto her.
Naomi alipoona kuwa Ruth alikuwa ameamua kwenda naye, aliacha kubishana naye.
19 So they two went until they came to Beth-lehem. And it came to pass, when they were come to Beth-lehem, that all the city was astir concerning them, and the women said: 'Is this Naomi?'
Hivyo wote wawili walisafiri mpaka walipofika mjini Bethelehemu. Kwa hiyo walipofika Bethlehemu, mji wote uliwafurahia, wanawake walisema, “Huyu ni Naomi?”
20 And she said unto them: 'Call me not Naomi, call me Marah; for the Almighty hath dealt very bitterly with me.
Lakini aliwaambia, “Msiniite Naomi. Niiteni Mchungu, kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitenda mambo machungu sana.
21 I went out full, and the LORD hath brought me back home empty; why call ye me Naomi, seeing the LORD hath testified against me, and the Almighty hath afflicted me?'
Nilikwenda nikiwa nimejaa, lakini Yahweh kanirudisha nyumbani nikiwa sina wote. Hivyo kwa nini mnaniita Naomi, wakati mnaona Yahweh amenihukumu, kuwa Mwenyezi Mungu amenitaabisha?”
22 So Naomi returned, and Ruth the Moabitess, her daughter-in-law, with her, who returned out of the field of Moab — and they came to Beth-lehem in the beginning of barley harvest.
Kwa hivyo Naomi na Ruth Mmoabu, mke wa mtoto wake, walirudi kutoka nchi ya Moabu. walirudi Bethrehemu mwazo wa mavuno ya shairi.

< Ruth 1 >