< Psalms 91 >

1 O thou that dwellest in the covert of the Most High, and abidest in the shadow of the Almighty;
Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
2 I will say of the LORD, who is my refuge and my fortress, my God, in whom I trust,
Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
3 That He will deliver thee from the snare of the fowler, and from the noisome pestilence.
Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
4 He will cover thee with His pinions, and under His wings shalt thou take refuge; His truth is a shield and a buckler.
Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
5 Thou shalt not be afraid of the terror by night, nor of the arrow that flieth by day;
Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
6 Of the pestilence that walketh in darkness, nor of the destruction that wasteth at noonday.
wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
7 A thousand may fall at Thy side, and ten thousand at Thy right hand; it shall not come nigh thee.
Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
8 Only with thine eyes shalt thou behold, and see the recompense of the wicked.
Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
9 For thou hast made the LORD who is my refuge, even the Most High, thy habitation.
Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
10 There shall no evil befall thee, neither shall any plague come nigh thy tent.
Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
11 For He will give His angels charge over thee, to keep thee in all thy ways.
Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
12 They shall bear thee upon their hands, lest thou dash thy foot against a stone.
Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
13 Thou shalt tread upon the lion and asp; the young lion and the serpent shalt thou trample under feet.
Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
14 'Because he hath set his love upon Me, therefore will I deliver him; I will set him on high, because he hath known My name.
Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
15 He shall call upon Me, and I will answer him; I will be with him in trouble; I will rescue him, and bring him to honour.
Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
16 With long life will I satisfy him, and make Him to behold My salvation.'
Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.

< Psalms 91 >