< Psalms 88 >
1 A Song, a Psalm of the sons of Korah; for the Leader; upon Mahalath Leannoth. Maschil of Heman the Ezrahite. O LORD, God of my salvation, what time I cry in the night before Thee,
Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
2 Let my prayer come before Thee, incline Thine ear unto my cry.
Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
3 For my soul is sated with troubles, and my life draweth nigh unto the grave. (Sheol )
Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol )
4 I am counted with them that go down into the pit; I am become as a man that hath no help;
Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5 Set apart among the dead, like the slain that lie in the grave, whom Thou rememberest no more; and they are cut off from Thy hand.
Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6 Thou hast laid me in the nethermost pit, in dark places, in the deeps.
Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7 Thy wrath lieth hard upon me, and all Thy waves Thou pressest down. (Selah)
Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
8 Thou hast put mine acquaintance far from me; Thou hast made me an abomination unto them; I am shut up, and I cannot come forth.
Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 Mine eye languisheth by reason of affliction; I have called upon Thee, O LORD, every day, I have spread forth my hands unto Thee.
Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 Wilt Thou work wonders for the dead? Or shall the shades arise and give Thee thanks? (Selah)
Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
11 Shall Thy mercy be declared in the grave? or Thy faithfulness in destruction?
Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 Shall Thy wonders be known in the dark? and Thy righteousness in the land of forgetfulness?
Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 But as for me, unto Thee, O LORD, do I cry, and in the morning doth my prayer come to meet Thee.
Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 LORD, why castest Thou off my soul? Why hidest Thou Thy face from me?
Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 I am afflicted and at the point of death from my youth up; I have borne Thy terrors, I am distracted.
Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 Thy fierce wrath is gone over me; Thy terrors have cut me off.
Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 They came round about me like water all the day; they compassed me about together.
Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
18 Friend and companion hast Thou put far from me, and mine acquaintance into darkness.
Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.