< Psalms 4 >
1 For the Leader; with string-music. A Psalm of David. Answer me when I call, O God of my righteousness, Thou who didst set me free when I was in distress; be gracious unto me, and hear my prayer.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.
2 O ye sons of men, how long shall my glory be put to shame, in that ye love vanity, and seek after falsehood? (Selah)
Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
3 But know that the LORD hath set apart the godly man as His own; the LORD will hear when I call unto Him.
Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga wale wamchao kwa ajili yake; Bwana atanisikia nimwitapo.
4 Tremble, and sin not; commune with your own heart upon your bed, and be still. (Selah)
Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.
5 Offer the sacrifices of righteousness, and put your trust in the LORD.
Toeni dhabihu zilizo haki; mtegemeeni Bwana.
6 Many there are that say: 'Oh that we could see some good!' LORD, lift Thou up the light of Thy countenance upon us.
Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye kutuonyesha jema lolote?” Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.
7 Thou hast put gladness in my heart, more than when their corn and their wine increase.
Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
8 In peace will I both lay me down and sleep; for Thou, LORD, makest me dwell alone in safety.
Nitajilaza chini na kulala kwa amani, kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana, waniwezesha kukaa kwa salama.