< Psalms 137 >

1 By the rivers of Babylon, there we sat down, yea, we wept, when we remembered Zion.
Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
2 Upon the willows in the midst thereof we hanged up our harps.
Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
3 For there they that led us captive asked of us words of song, and our tormentors asked of us mirth: 'Sing us one of the songs of Zion.'
Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
4 How shall we sing the LORD'S song in a foreign land?
Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
5 If I forget thee, O Jerusalem, let my right hand forget her cunning.
Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6 Let my tongue cleave to the roof of my mouth, if I remember thee not; if I set not Jerusalem above my chiefest joy.
Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
7 Remember, O LORD, against the children of Edom the day of Jerusalem; who said: 'Rase it, rase it, even to the foundation thereof.'
Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
8 O daughter of Babylon, that art to be destroyed; happy shall he be, that repayeth thee as thou hast served us.
Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
9 Happy shall he be, that taketh and dasheth thy little ones against the rock.
Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.

< Psalms 137 >