< Psalms 135 >

1 Hallelujah. Praise ye the name of the LORD; give praise, O ye servants of the LORD,
Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
2 Ye that stand in the house of the LORD, in the courts of the house of our God.
ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Praise ye the LORD, for the LORD is good; sing praises unto His name, for it is pleasant.
Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
4 For the LORD hath chosen Jacob unto Himself, and Israel for His own treasure.
Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
5 For I know that the LORD is great, and that our Lord is above all gods.
Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
6 Whatsoever the LORD pleased, that hath He done, in heaven and in earth, in the seas and in all deeps;
Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
7 Who causeth the vapours to ascend from the ends of the earth; He maketh lightnings for the rain; He bringeth forth the wind out of His treasuries.
Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
8 Who smote the first-born of Egypt, both of man and beast.
Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
9 He sent signs and wonders into the midst of thee, O Egypt, upon Pharaoh, and upon all his servants.
Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Who smote many nations, and slew mighty kings:
Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
11 Sihon king of the Amorites, and Og king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan;
Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
12 And gave their land for a heritage, a heritage unto Israel His people.
Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
13 O LORD, Thy name endureth for ever; thy memorial, O LORD, throughout all generations.
Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
14 For the LORD will judge His people, and repent Himself for His servants.
Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
15 The idols of the nations are silver and gold, the work of men's hands.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
16 They have mouths, but they speak not; eyes have they, but they see not;
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
17 They have ears, but they hear not; neither is there any breath in their mouths.
zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
18 They that make them shall be like unto them; yea, every one that trusteth in them.
Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
19 O house of Israel, bless ye the LORD; O house of Aaron, bless ye the LORD;
Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
20 O house of Levi, bless ye the LORD; ye that fear the LORD, bless ye the LORD.
Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
21 Blessed be the LORD out of Zion, who dwelleth at Jerusalem. Hallelujah.
Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.

< Psalms 135 >