< Psalms 124 >
1 A Song of Ascents; of David. 'If it had not been the LORD who was for us', let Israel now say;
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
2 'If it had not been the LORD who was for us, when men rose up against us,
kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
3 Then they had swallowed us up alive, when their wrath was kindled against us;
wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
4 Then the waters had overwhelmed us, the stream had gone over our soul;
mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
5 Then the proud waters had gone over our soul.'
maji yaendayo kasi yangalituchukua.
6 Blessed be the LORD, who hath not given us as a prey to their teeth.
Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7 Our soul is escaped as a bird out of the snare of the fowlers; the snare is broken, and we are escaped.
Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
8 Our help is in the name of the LORD, who made heaven and earth.
Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.