< Psalms 115 >

1 Not unto us, O LORD, not unto us, but unto Thy name give glory, for Thy mercy, and for Thy truth's sake.
Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
2 Wherefore should the nations say: 'Where is now their God?'
Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
3 But our God is in the heavens; whatsoever pleased Him He hath done.
Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
4 Their idols are silver and gold, the work of men's hands.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
5 They have mouths, but they speak not; eyes have they, but they see not;
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
6 They have ears, but they hear not; noses have they, but they smell not;
zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
7 They have hands, but they handle not; feet have they, but they walk not; neither speak they with their throat.
Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
8 They that make them shall be like unto them; yea, every one that trusteth in them.
Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
9 O Israel, trust thou in the LORD! He is their help and their shield!
Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
10 O house of Aaron, trust ye in the LORD! He is their help and their shield!
Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
11 Ye that fear the LORD, trust in the LORD! He is their help and their shield.
Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
12 The LORD hath been mindful of us, He will bless — He will bless the house of Israel; He will bless the house of Aaron.
Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
13 He will bless them that fear the LORD, both small and great.
Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
14 The LORD increase you more and more, you and your children.
Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
15 Blessed be ye of the LORD who made heaven and earth.
Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
16 The heavens are the heavens of the LORD; but the earth hath He given to the children of men.
Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
17 The dead praise not the LORD, neither any that go down into silence;
Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
18 But we will bless the LORD from this time forth and for ever. Hallelujah.
bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.

< Psalms 115 >