< Psalms 112 >
1 Hallelujah. Happy is the man that feareth the LORD, that delighteth greatly in His commandments.
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 His seed shall be mighty upon earth; the generation of the upright shall be blessed.
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 Wealth and riches are in his house; and his merit endureth for ever.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 Unto the upright He shineth as a light in the darkness, gracious, and full of compassion, and righteous.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 Well is it with the man that dealeth graciously and lendeth, that ordereth his affairs rightfully.
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 For he shall never be moved; the righteous shall be had in everlasting remembrance.
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 He shall not be afraid of evil tidings; his heart is stedfast, trusting in the LORD.
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 His heart is established, he shall not be afraid, until he gaze upon his adversaries.
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 He hath scattered abroad, he hath given to the needy; his righteousness endureth for ever; his horn shall be exalted in honour.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 The wicked shall see it, and be vexed; he shall gnash with his teeth, and melt away; the desire of the wicked shall perish.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.