< Psalms 108 >

1 A Song, a Psalm of David. My heart is steadfast, O God; I will sing, yea, I will sing praises, even with my glory.
Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
2 Awake, psaltery and harp; I will awake the dawn.
Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
3 I will give thanks unto Thee, O LORD, among the peoples; and I will sing praises unto Thee among the nations.
Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
4 For Thy mercy is great above the heavens, and Thy truth reacheth unto the skies.
Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
5 Be Thou exalted, O God, above the heavens; and Thy glory be above all the earth.
Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
6 That Thy beloved may be delivered, save with Thy right hand, and answer me.
Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
7 God spoke in His holiness, that I would exult; that I would divide Shechem, and mete out the valley of Succoth.
Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
8 Gilead is mine, Manasseh is mine; Ephraim also is the defence of my head; Judah is my sceptre.
Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
9 Moab is my washpot; upon Edom do I cast my shoe; over Philistia do I cry aloud.
Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
10 Who will bring me into the fortified city? Who will lead me unto Edom?
Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
11 Hast not Thou cast us off, O God? and Thou goest not forth, O God, with our hosts?
Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
12 Give us help against the adversary; for vain is the help of man.
Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
13 Through God we shall do valiantly; for He it is that will tread down our adversaries.
Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.

< Psalms 108 >