< Psalms 106 >

1 Hallelujah. O give thanks unto the LORD; for He is good; for His mercy endureth for ever.
Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Who can express the mighty acts of the LORD, or make all His praise to be heard?
Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
3 Happy are they that keep justice, that do righteousness at all times.
Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
4 Remember me, O LORD, when Thou favourest Thy people; O think of me at Thy salvation;
Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
5 That I may behold the prosperity of Thy chosen, that I may rejoice in the gladness of Thy nation, that I may glory with Thine inheritance.
Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
6 We have sinned with our fathers, we have done iniquitously, we have dealt wickedly.
Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
7 Our fathers in Egypt gave no heed unto Thy wonders; they remembered not the multitude of Thy mercies; but were rebellious at the sea, even at the Red Sea.
Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
8 Nevertheless He saved them for His name's sake, that He might make His mighty power to be known.
Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
9 And He rebuked the Red Sea, and it was dried up; and He led them through the depths, as through a wilderness.
Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
10 And He saved them from the hand of him that hated them, and redeemed them from the hand of the enemy.
Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
11 And the waters covered their adversaries; there was not one of them left.
Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
12 Then believed they His words; they sang His praise.
Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
13 They soon forgot His works; they waited not for His counsel;
Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
14 But lusted exceedingly in the wilderness, and tried God in the desert.
Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
15 And He gave them their request; but sent leanness into their soul.
Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
16 They were jealous also of Moses in the camp, and of Aaron the holy one of the LORD.
Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
17 The earth opened and swallowed up Dathan, and covered the company of Abiram.
Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
18 And a fire was kindled in their company; the flame burned up the wicked.
Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
19 They made a calf in Horeb, and worshipped a molten image.
Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
20 Thus they exchanged their glory for the likeness of an ox that eateth grass.
Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
21 They forgot God their saviour, who had done great things in Egypt;
Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
22 Wondrous works in the land of Ham, terrible things by the Red Sea.
Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
23 Therefore He said that He would destroy them, had not Moses His chosen stood before Him in the breach, to turn back His wrath, lest He should destroy them.
Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
24 Moreover, they scorned the desirable land, they believed not His word;
Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
25 And they murmured in their tents, they hearkened not unto the voice of the LORD.
bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
26 Therefore He swore concerning them, that He would overthrow them in the wilderness;
Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
27 And that He would cast out their seed among the nations, and scatter them in the lands.
akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
28 They joined themselves also unto Baal of Peor, and ate the sacrifices of the dead.
Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
29 Thus they provoked Him with their doings, and the plague broke in upon them.
Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
30 Then stood up Phinehas, and wrought judgment, and so the plague was stayed.
Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
31 And that was counted unto him for righteousness, unto all generations for ever.
Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
32 They angered Him also at the waters of Meribah, and it went ill with Moses because of them;
Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
33 For they embittered his spirit, and he spoke rashly with his lips.
Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
34 They did not destroy the peoples, as the LORD commanded them;
Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
35 But mingled themselves with the nations, and learned their works;
bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
36 And they served their idols, which became a snare unto them;
nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
37 Yea, they sacrificed their sons and their daughters unto demons,
Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
38 And shed innocent blood, even the blood of their sons and of their daughters, whom they sacrificed unto the idols of Canaan; and the land was polluted with blood.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
39 Thus were they defiled with their works, and went astray in their doings.
Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
40 Therefore was the wrath of the LORD kindled against His people, and He abhorred His inheritance.
Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
41 And He gave them into the hand of the nations; and they that hated them ruled over them.
Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
42 Their enemies also oppressed them, and they were subdued under their hand.
Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
43 Many times did He deliver them; but they were rebellious in their counsel, and sank low through their iniquity.
Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
44 Nevertheless He looked upon their distress, when He heard their cry;
Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
45 And He remembered for them His covenant, and repented according to the multitude of His mercies.
Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
46 He made them also to be pitied of all those that carried them captive.
Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
47 Save us, O LORD our God, and gather us from among the nations, that we may give thanks unto Thy holy name, that we may triumph in Thy praise.
Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
48 Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting even to everlasting, and let all the people say: 'Amen.' Hallelujah.
Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.

< Psalms 106 >