< Numbers 9 >

1 And the LORD spoke unto Moses in the wilderness of Sinai, in the first month of the second year after they were come out of the land of Egypt, saying:
BWANA akanena na Musa katika katika jangwa la Sinai, mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya kutoka katika nci ya Misri. Akasema,
2 'Let the children of Israel keep the passover in its appointed season.
“Wana wa Israeli wataikumbuka Pasaka katika wakati wake kila mwaka.
3 In the fourteenth day of this month, at dusk, ye shall keep it in its appointed season; according to all the statutes of it, and according to all the ordinances thereof, shall ye keep it.'
Siku ya kumi na nne ya mwezi huu, muda wa jioni, utaikumbuka Pasaka kila mwaka kwa muda uliopanggwa. Lazima uikumbuke, fuata taratibu zake zote na utii sheria zake zote zinazohusiana na tukio hilo.
4 And Moses spoke unto the children of Israel, that they should keep the passover.
Kwa hiyo, Musa akawaambia wana wa Isareli kuwa wataishika sikukuu ya Pasaka.
5 And they kept the passover in the first month, on the fourteenth day of the month, at dusk, in the wilderness of Sinai; according to all that the LORD commanded Moses, so did the children of Israel.
Kwa hiyo wakaishika sikuu ya Pasaka katika mwezi wa kwanza, wakati wa jioni wa siku ya kumi na nne ya mwezi katika jangwa la Sinai. Wana wa Israeli walitii kila kitu ambacho BWANA alimwamuru Musa kukifanya.
6 But there were certain men, who were unclean by the dead body of a man, so that they could not keep the passover on that day; and they came before Moses and before Aaron on that day.
Kulikuwa na watu fulani walionajisika kwa sababu ya maiti ya mtu. Hawakuweza kuishika Pasaka siku hiyo. Kwa hiyo walikwenda kwa Musa na Haruni siku hiyohiyo.
7 And those men said unto him: 'We are unclean by the dead body of a man; wherefore are we to be kept back, so as not to bring the offering of the LORD in its appointed season among the children of Israel?'
Wakamwambia Musa, “Sisi tumenajisika kwa sababu ya maiti ya mtu. Kwa nini basi unatutaka tuendelee kutoa sadaka kwa BWANA kwa wakati wa mwaka uliopangwa kwa wana wa Israeli?”
8 And Moses said unto them: 'Stay ye, that I may hear what the LORD will command concerning you.'
Naye Musa akawaambia, “Subirini nimsikilize BWANA ataniambia nini juu Yenu.”
9 And the LORD spoke unto Moses, saying:
BWANA akanena na Musa, akamwambia,
10 'Speak unto the children of Israel, saying: If any man of you or of your generations shall be unclean by reason of a dead body, or be in a journey afar off, yet he shall keep the passover unto the LORD;
“Nena na wana wa Israeli, uwaambie, 'kama mmoja wenu au mwana wa uzao wenu amenajisika kwa sababu ya maiti, au ana safari ndefu, bado anaweza kuishika Pasaka ya BWANA.
11 in the second month on the fourteenth day at dusk they shall keep it; they shall eat it with unleavened bread and bitter herbs;
Wataishika Pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili wakati wa jioni. Wataila kwa mikate isyotiwa chahcu na mboga chungu.
12 they shall leave none of it unto the morning, nor break a bone thereof; according to all the statute of the passover they shall keep it.
Wasiiache mpaka jioni, au kuvunja mifupa yake. Watafuata taratibu zote za Pasaka.
13 But the man that is clean, and is not on a journey, and forbeareth to keep the passover, that soul shall be cut off from his people; because he brought not the offering of the LORD in its appointed season, that man shall bear his sin.
Lakini mtu yeyote asiye najisi na hayuko safarini, na akashindwa kuishika Pasaka, huyo mtu lazima aondolewe kati ya watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ambayo BWANA huitaka kwa wakati wa mwaka uliopangwa. Huyo mtu lazima aibebe dhambi yake.
14 And if a stranger shall sojourn among you, and will keep the passover unto the LORD: according to the statute of the passover, and according to the ordinance thereof, so shall he do; ye shall have one statute, both for the stranger, and for him that is born in the land.'
Kama mtu mgeni anayeishi kati yenu na akaishika, Pasaka kwa heshima ya BWANA, ataishika na kufanya amri zote, na kutii taratibu zake. Utakuwa na sheria hizohizo kwa wageni na kwa wote waliaozaliwa katika nchi.
15 And on the day that the tabernacle was reared up the cloud covered the tabernacle, even the tent of the testimony; and at even there was upon the tabernacle as it were the appearance of fire, until morning.
Na siku hiyo ambayo masikani iliposimamishwa, wingu lilifunika masikani, ile hema ya amari ya agano. Ilipokuwa jioni wingu lilkuwa juu ya masikani. Lilionekana kama moto mpaka asubuhi.
16 So it was alway: the cloud covered it, and the appearance of fire by night.
Liliendelea hivyohivyo. Lile wingu lilifunika masikani na kuonekana kama moto wakati wa usiku.
17 And whenever the cloud was taken up from over the Tent, then after that the children of Israel journeyed; and in the place where the cloud abode, there the children of Israel encamped.
Na kila wingu lilipochukuliwa kutoka kwenye hema, wana wa Isareli waliendelea na safari yao. Na kila wingu liliposimama, watu waliweka kambi.
18 At the commandment of the LORD the children of Israel journeyed, and at the commandment of the LORD they encamped: as long as the cloud abode upon the tabernacle they remained encamped.
Wana wa Israrli walisafiri kwa amri ya BWANA, na kwa amri yake waliweka kambi. Wakati wingu liliposimama juu ya masikani, nao walikaa kwenye kambi zao.
19 And when the cloud tarried upon the tabernacle many days, then the children of Israel kept the charge of the LORD, and journeyed not.
Na wingu lilipobaki kwenye masikani kwa siku nyingi, wana wa Israeli walitakiwa kutii maelekezo ya BWANA na kusitisha safari yao.
20 And sometimes the cloud was a few days upon the tabernacle; according to the commandment of the LORD they remained encamped, and according to the commandment of the LORD they journeyed.
Wakati mwingine wingu lilibaki kwa siku chache tu kwenye masikani. Kwa mazingira kama hayo walilazimika kutii amri ya BWANA - waliweka kambi na kisha kuendelea na safari tena kwa amri yake.
21 And sometimes the cloud was from evening until morning; and when the cloud was taken up in the morning, they journeyed; or if it continued by day and by night, when the cloud was taken up, they journeyed.
Wakati mwingine wingu lilikuwepo kambini kuanzia jioni mpaka asubuhi. Na wingu liliponyanyuliwa asubuhi, walisafiri. Kama liliendelea kwa mchana wote na kwa usiku wote, ni pale tu wingu liliponyanyuliwa ndipo walipoendelea na safari.
22 Whether it were two days, or a month, or a year, that the cloud tarried upon the tabernacle, abiding thereon, the children of Israel remained encamped, and journeyed not; but when it was taken up, they journeyed.
Hata kama wingu lilibaki kwenye masikini kwa siku mbili, kwa mwezi mmoja, au kwa mwaka mmoja, ili mradi tu limebaki pale, wana wa Israeli walibaki kwenye kambi zao na kusitisha safari. Lakini pale wingu liliponyanyuliwa, walianza safari yao.
23 At the commandment of the LORD they encamped, and at the commandment of the LORD they journeyed; they kept the charge of the LORD, at the commandment of the LORD by the hand of Moses.
Walifanya kambi kwa amri ya BWANA, na walisafiri kwa amri yake. Walitii amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa

< Numbers 9 >