< Numbers 3 >

1 Now these are the generations of Aaron and Moses in the day that the LORD spoke with Moses in mount Sinai.
Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
2 And these are the names of the sons of Aaron: Nadab the first-born, and Abihu, Eleazar, and Ithamar.
Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
3 These are the names of the sons of Aaron, the priests that were anointed, whom he consecrated to minister in the priest's office.
Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
4 And Nadab and Abihu died before the LORD, when they offered strange fire before the LORD, in the wilderness of Sinai, and they had no children; and Eleazar and Ithamar ministered in the priest's office in the presence of Aaron their father.
Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
5 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
6 'Bring the tribe of Levi near, and set them before Aaron the priest, that they may minister unto him.
“Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
7 And they shall keep his charge, and the charge of the whole congregation before the tent of meeting, to do the service of the tabernacle.
Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
8 And they shall keep all the furniture of the tent of meeting, and the charge of the children of Israel, to do the service of the tabernacle.
Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
9 And thou shalt give the Levites unto Aaron and to his sons; they are wholly given unto him from the children of Israel.
Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
10 And thou shalt appoint Aaron and his sons, that they may keep their priesthood; and the common man that draweth nigh shall be put to death.'
Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
11 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
12 'And I, behold, I have taken the Levites from among the children of Israel instead of every first-born that openeth the womb among the children of Israel; and the Levites shall be Mine;
“Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
13 for all the first-born are Mine: on the day that I smote all the first-born in the land of Egypt I hallowed unto Me all the first-born in Israel, both man and beast, Mine they shall be: I am the LORD.'
kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
14 And the LORD spoke unto Moses in the wilderness of Sinai, saying:
Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
15 'Number the children of Levi by their fathers' houses, by their families; every male from a month old and upward shalt thou number them.'
“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
16 And Moses numbered them according to the word of the LORD, as he was commanded.
Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
17 And these were the sons of Levi by their names: Gershon, and Kohath, and Merari.
Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
18 And these are the names of the sons of Gershon by their families: Libni and Shimei.
Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
19 And the sons of Kohath by their families: Amram and Izhar, Hebron and Uzziel.
Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
20 And the sons of Merari by their families: Mahli and Mushi. These are the families of the Levites according to their fathers' houses.
Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
21 Of Gershon was the family of the Libnites, and the family of the Shimeites; these are the families of the Gershonites.
Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
22 Those that were numbered of them, according to the number of all the males, from a month old and upward, even those that were numbered of them were seven thousand and five hundred.
Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
23 The families of the Gershonites were to pitch behind the tabernacle westward;
Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
24 the prince of the fathers' house of the Gershonites being Eliasaph the son of Lael,
Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
25 and the charge of the sons of Gershon in the tent of meeting the tabernacle, and the Tent, the covering thereof, and the screen for the door of the tent of meeting,
Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
26 and the hangings of the court, and the screen for the door of the court — which is by the tabernacle, and by the altar, round about—and the cords of it, even whatsoever pertaineth to the service thereof.
mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
27 And of Kohath was the family of the Amramites, and the family of the Izharites, and the family of the Hebronites, and the family of the Uzzielites; these are the families of the Kohathites:
Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
28 according to the number of all the males, from a month old and upward, eight thousand and six hundred, keepers of the charge of the sanctuary.
Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
29 The families of the sons of Kohath were to pitch on the side of the tabernacle southward;
Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
30 the prince of the fathers' house of the families of the Kohathites being Elizaphan the son of Uzziel,
Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
31 and their charge the ark, and the table, and the candlestick, and the altars, and the vessels of the sanctuary wherewith the priests minister, and the screen, and all that pertaineth to the service thereof;
Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
32 Eleazar the son of Aaron the priest being prince of the princes of the Levites, and having the oversight of them that keep the charge of the sanctuary.
Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
33 Of Merari was the family of the Mahlites, and the family of the Mushites; these are the families of Merari.
Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
34 And those that were numbered of them, according to the number of all the males, from a month old and upward, were six thousand and two hundred;
Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
35 the prince of the fathers' house of the families of Merari being Zuriel the son of Abihail; they were to pitch on the side of the tabernacle northward;
Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
36 the appointed charge of the sons of Merari being the boards of the tabernacle, and the bars thereof, and the pillars thereof, and the sockets thereof, and all the instruments thereof, and all that pertaineth to the service thereof;
Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
37 and the pillars of the court round about, and their sockets, and their pins, and their cords.
na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
38 And those that were to pitch before the tabernacle eastward, before the tent of meeting toward the sunrising, were Moses, and Aaron and his sons, keeping the charge of the sanctuary, even the charge for the children of Israel; and the common man that drew nigh was to be put to death.
Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
39 All that were numbered of the Levites, whom Moses and Aaron numbered at the commandment of the LORD, by their families, all the males from a month old and upward, were twenty and two thousand.
Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
40 And the LORD said unto Moses: 'Number all the first-born males of the children of Israel from a month old and upward, and take the number of their names.
Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
41 And thou shalt take the Levites for Me, even the LORD, instead of all the first-born among the children of Israel; and the cattle of the Levites instead of all the firstlings among the cattle of the children of Israel.'
Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
42 And Moses numbered, as the LORD commanded him, all the first-born among the children of Israel.
Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
43 And all the first-born males according to the number of names, from a month old and upward, of those that were numbered of them, were twenty and two thousand two hundred and threescore and thirteen.
Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
44 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
45 'Take the Levites instead of all the first-born among the children of Israel, and the cattle of the Levites instead of their cattle; and the Levites shall be Mine, even the LORD'S.
“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
46 And as for the redemption of the two hundred and three score and thirteen of the first-born of the children of Israel, that are over and above the number of the Levites,
Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
47 thou shalt take five shekels apiece by the poll; after the shekel of the sanctuary shalt thou take them — the shekel is twenty gerahs.
kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
48 And thou shalt give the money wherewith they that remain over of them are redeemed unto Aaron and to his sons.'
Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
49 And Moses took the redemption-money from them that were over and above them that were redeemed by the Levites;
Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
50 from the first-born of the children of Israel took he the money: a thousand three hundred and threescore and five shekels, after the shekel of the sanctuary.
Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
51 And Moses gave the redemption-money unto Aaron and to his sons, according to the word of the LORD, as the LORD commanded Moses.
Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

< Numbers 3 >