< Numbers 18 >

1 And the LORD said unto Aaron: 'Thou and thy sons and thy fathers' house with thee shall bear the iniquity of the sanctuary; and thou and thy sons with thee shall bear the iniquity of your priesthood.
BWANA akamwambia Haruni, “Wewe, wana wako, na uzao wa baba yako watawajibika kwa dhambi zote zilizotendwa mahali patakatifu. Lakini wewe na wana wako pekee mtawajibika kwa uovu uliofanywa na yeyote mahali patakatifu.
2 And thy brethren also, the tribe of Levi, the tribe of thy father, bring thou near with thee, that they may be joined unto thee, and minister unto thee, thou and thy sons with thee being before the tent of the testimony.
Na ndugu zako nao wa kabila ya Lawi, kabila la ukoo wako, utawaleta pamoja na wewe ili kwamba waweze kuungana na wewe ili wakusaidie wakati wewe na wanao mnapokuwa mnatumikia mbele ya hema ya amri ya agano.
3 And they shall keep thy charge, and the charge of all the Tent; only they shall not come nigh unto the holy furniture and unto the altar, that they die not, neither they, nor ye.
Watakutumikia wewe na hema yote. Hata hivyo, wasisogee karibu na chochote ndani ya mahali patakatifu au kitu chochote kilichounganishwa na madhabahu, vinginevyo wewe na wao mtakufa.
4 And they shall be joined unto thee, and keep the charge of the tent of meeting, whatsoever the service of the Tent may be; but a common man shall not draw nigh unto you.
Wataungana na wewe na kuitunza hema ya kukutania, kwa kazi zote zinazohusiana na hema. Mtu mgeni asikusogelee.
5 And ye shall keep the charge of the holy things, and the charge of the altar, that there be wrath no more upon the children of Israel.
Wewe utaajibika kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya madhabahu ili kwamba hasira yangu isiwajilie watu wa Israeli tena.
6 And I, behold, I have taken your brethren the Levites from among the children of Israel; for you they are given as a gift unto the LORD, to do the service of the tent of meeting.
Tazama, Mmi mwenyewe nimewachagua ndugu zako wa kabila ya Walawi kutoka mioingoni mwa uzao wa Israeli. Wao ni zawadi kwako. walitolewa kwangu ili waifanye kazi inayohusiana na hema ya kukutania.
7 And thou and thy sons with thee shall keep your priesthood in everything that pertaineth to the altar, and to that within the veil; and ye shall serve; I give you the priesthood as a service of gift; and the common man that draweth nigh shall be put to death.'
Lakini ni wewe pekee yako na wanao ndio mnaoruhusiwa kufanya kazi ya ukuhani kuhusiana na kila kitu kilichounganishwa na madhabahu na kitu chochote ndani ya lile pazia. Wewe mwenyewe lazima ukamilishe majukumu hayo. Mimi ninakupa ukuhani kama zawadi. Mgeni yeyote anayekaribia atauawa.”
8 And the LORD spoke unto Aaron: 'And I, behold, I have given thee the charge of My heave-offerings; even of all the hallowed things of the children of Israel unto thee have I given them for a consecrated portion, and to thy sons, as a due for ever.
Kisha BWANA akamwambia Haruni, “Tazama, Nimekupa majukumu ya kusimamia sadaka za kuinuliwa kwangu, na sadaka zengine takatifu ambazo wana wa Israeli wanatoa kwangu. Nimekupa sadaka hizi wewe na wana wako kuwa haki yako milele.
9 This shall be thine of the most holy things, reserved from the fire: every offering of theirs, even every meal-offering of theirs, and every sin-offering of theirs, and every guilt-offering of theirs, which they may render unto Me, shall be most holy for thee and for thy sons.
Hivi ni vitu vitakatifu sana, amabavyo visiteketezwe kwa moto: kutoka kwenye sadaka zao-kila sadaka ya unga, kila sadaka ya dhambi, na kila sadaka ya hatia- ni vitu vitakatifu sana kwa ajili yako na wana wako.
10 In a most holy place shalt thou eat thereof; every male may eat thereof; it shall be holy unto thee.
Sadaka hizi ni takatifu sana; kila mume lazima aile, kwa kuwa ni vitakatifu kwako.
11 And this is thine: the heave-offering of their gift, even all the wave-offerings of the children of Israel; I have given them unto thee, and to thy sons and to thy daughters with thee, as a due for ever; every one that is clean in thy house may eat thereof.
Hizi ni sadaka ambazo zitakuwa zako: Sadaka zao, sadaka zote za kuinuliwa za wana wa Israeli. Nimekupa wewe, wana wako na binti zako kuwa gawio lako la milele. Kila mmoja ambaye ni msafi katika familia yako anaweza kula sadaka zozote katika hizi.
12 All the best of the oil, and all the best of the wine, and of the corn, the first part of them which they give unto the LORD, to thee have I given them.
Mafuta yote mazuri, ile divai nzuri yote mpya na unga, malimbuko ambyo watu hutoa kwangu- vitu hivi vyote nimekupa wewe.
13 The first-ripe fruits of all that is in their land, which they bring unto the LORD, shall be thine; every one that is clean in thy house may eat thereof.
Mavuno ya kwanza yaliyoiva yaliyo katika ardhi yao ambayo wanaleta kwangu, yatakuwa yako. Kila mtu aliye msafi kwenye famila yako anaweza kula vitu hivi.
14 Every thing devoted in Israel shall be thine.
Kila kitu kilichotolewa wakfu katika Israeli kitakuwa chako.
15 Every thing that openeth the womb, of all flesh which they offer unto the LORD, both of man and beast, shall be thine; howbeit the first-born of man shalt thou surely redeem, and the firstling of unclean beasts shalt thou redeem.
Kila kitu kinachofungua tumbo, kila limbuko ambalo watu hutoa kwa BWANA, vyote vya watu na wanyama, vitakuwa vyako. Hata hivyo, watu lazima wawakomboe wazaliwa wa kwanza wa kiume, na watawakomboa wazaliwa wa kwanza wa wanyama wasio safi.
16 And their redemption-money — from a month old shalt thou redeem them — shall be, according to thy valuation, five shekels of silver, after the shekel of the sanctuary — the same is twenty gerahs.
Wale ambao wanahitaji kukombolewa na watu watakombolewa wakiwa na umri wa mwezi mmoja. Ndipo watu watawakomboa kwa bei ya shekeli tano, kwa kiwango cha shekeli za mahali patakatifu, ambacho ni sawa na gera ishirini.
17 But the firstling of an ox, or the firstling of a sheep, or the firstling of a goat, thou shalt not redeem; they are holy: thou shalt dash their blood against the altar, and shalt make their fat smoke for an offering made by fire, for a sweet savour unto the LORD.
Lakini mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe, au mzaliwa wa kwana wa kondoo, au mzaliwa wa kwanza wa mbuzi-msiwakomboe hawa wanyama, wametengwa kwa ajili yangu. Utanyunyizia damu yake madhabahuni na kuteketeza mafuta yao kama sadaka ya moto, ambayo ni harufu nzuri ya kumpendeza BWANA.
18 And the flesh of them shall be thine, as the wave-breast and as the right thigh, it shall be thine.
Nyama yao itakuwa yako. Kama kidali cha kuinuliwa na paja la kulia, nyama yao itakuwa yako.
19 All the heave-offerings of the holy things, which the children of Israel offer unto the LORD, have I given thee, and thy sons and thy daughters with thee, as a due for ever; it is an everlasting covenant of salt before the LORD unto thee and to thy seed with thee.'
Sadaka yote takatifu ambayo watu wa Israeli wanaitoa kwa BWANA, nimekupa wewe, na wana wako na binti zako walio pamoja nawe. Kama gawio la kudumu. Hili ni agano la milele la chumvi, agano linalofunga milele, mbele za BWANA kwako wewe na uzao wako walio pamoja na wewe.”
20 And the LORD said unto Aaron: 'Thou shalt have no inheritance in their land, neither shalt thou have any portion among them; I am thy portion and thine inheritance among the children of Israel.
BWANA akasema na Haruni. “hautakuwa na urithi katika ardhi ya watu, wala hautakuwa na gawio miongoni mwa watu. Mimi ndimi gawiio lenu na urithi wenu miongoni mwa watu wa Israeli.
21 And unto the children of Levi, behold, I have given all the tithe in Israel for an inheritance, in return for their service which they serve, even the service of the tent of meeting.
Tazama, Nimewapatia uzao wa Lawi, zaka zote za Israeli kuwa urithi wao kwa sababu ya huduma wanayotoa katika hema ya kukutania.
22 And henceforth the children of Israel shall not come nigh the tent of meeting, lest they bear sin, and die.
Kuanzi a sasa, watu wa Israeli wasisogee karibu na hema ya kukutania, vinginevyo wataajibika kwa dhambi hii na kufa.
23 But the Levites alone shall do the service of the tent of meeting, and they shall bear their iniquity; it shall be a statute for ever throughout your generations, and among the children of Israel they shall have no inheritance.
Walawi wafanya kazi inayohusiana na hema ya kukutania. Wataajibika kwa dhambi inyohusiana na hema. Hii itakuwa sheri ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Na miongoni mwa watu wa Israeli hawa hawatakuwa na urithi.
24 For the tithe of the children of Israel, which they set apart as a gift unto the LORD, I have given to the Levites for an inheritance; therefore I have said unto them: Among the children of Israel they shall have no inheritance.'
Kwa kuwa zaka za wana wa Israeli, wanazotoa kama mchango kwangu -ndivyo hivyo ambavyo nimewapa Walawi kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu ya kuwaambia, Kuwa hawatakuwa na urithi kati ya watu wa Israeli.
25 And the LORD spoke unto Moses, saying:
BWANA akanena na Musa, akamwambia,
26 'Moreover thou shalt speak unto the Levites, and say unto them: When ye take of the children of Israel the tithe which I have given you from them for your inheritance, then ye shall set apart of it a gift for the LORD, even a tithe of the tithe.
“Inakupasa ukaseme na Walawi uwaambie, 'Mnapopokea zaka toka kwa watu ambayo BWANA amewapa kutoka kwao kuwa urithi, ndipo na nyie mtakapotoa sehemu ya kumi ya zaka hizo.
27 And the gift which ye set apart shall be reckoned unto you, as though it were the corn of the threshing-floor, and as the fulness of the wine-press.
Zaka yenu itahesabika kama moja ya mapato ya sakafu ya kupuria nafaka ya mazao yenu au mazao ya vinu vya kukamulia zabibu.
28 Thus ye also shall set apart a gift unto the LORD of all your tithes, which ye receive of the children of Israel; and thereof ye shall give the gift which is set apart unto the LORD to Aaron the priest.
Kwa hiyo na ninyi lazima mtoe mchango wenu kwa BWANA kutokana na zaka mnazopata kutoka kwa watu wa Israeli. Kutokana na hizo mtatoa matoleo yenu kwa Haruni yule kuhani.
29 Out of all that is given you ye shall set apart all of that which is due unto the LORD, of all the best thereof, even the hallowed part thereof out of it.
Kwa kila sadaka mnayopata, mtatoa matoleo yenu kwa BWANA. Mtafanya hivi kutokana na vitu vizuri na vitakatifu sana ambavyo mmepewa.
30 Therefore thou shalt say unto them: When ye set apart the best thereof from it, then it shall be counted unto the Levites as the increase of the threshing-floor, and as the increase of the wine-press.
Kwa hiyo utawaambia, 'Mnapotoa hayo matoleo mazuri, ndipo itahesabika kwa Walawi kuwa ni mazao yao kutoka kwenye sakafu za kupuria na vinu vyao vya kukamulia.
31 And ye may eat it in every place, ye and your households; for it is your reward in return for your service in the tent of meeting.
Ndipo matakapokula nafaka zote zinazobaki mahali popote, ninyi na famailia zenu kwa sababu ndiyo malipo yenu ya kazi y a kwenye hema ya kukutania.
32 And ye shall bear no sin by reason of it, seeing that ye have set apart from it the best thereof; and ye shall not profane the holy things of the children of Israel, that ye die not.'
Hamtakuwa na hatia yeyote kwa kuvila na kuvinywa, kama mtatoa kwa BWANA matoleo yenu mazuri mliyopokea. Lakini msizinajisi sadaka takatifu za wana wa Israeli, vinginevyo mtakufa.,”

< Numbers 18 >