< Leviticus 7 >

1 And this is the law of the guilt-offering: it is most holy.
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya hatia. Kwa sababu hiyo ni sadaka takatifu sana.
2 In the place where they kill the burnt-offering shall they kill the guilt-offering: and the blood thereof shall be dashed against the altar round about.
Ni lazima waichinje sadaka ya hatia mahali panapostali kuchinjwa, na ni lazima watainyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
3 And he shall offer of it all the fat thereof: the fat tail, and the fat that covereth the inwards,
Mafuta yote yaliyomo ndani yake yataondolewa: mafuta ya mkiani, mafuta yaliyo sehamu za ndani,
4 and the two kidneys, and the fat that is on them, which is by the loins, and the lobe above the liver, which he shall take away by the kidneys.
zile figo mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake, yaliyo karibu na kiuno, na yanayofunika ini—nyama hii yote lazima iondolewe pamoja na hizo figo.
5 And the priest shall make them smoke upon the altar for an offering made by fire unto the LORD; it is a guilt-offering.
Kuhani ataviteketeza vipande hivi juu ya madhabahu viwe dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia
6 Every male among the priests may eat thereof; it shall be eaten in a holy place; it is most holy.
Kila mwanaume miongoni mwa familia ya kuhani anaweza kula sehemu ya sadaka hii. Lakini ni lazima iliwe ndani ya mahali patakatifu kwa sababu ni takatifu sana.
7 As is the sin-offering, so is the guilt-offering; there is one law for them; the priest that maketh atonement therewith, he shall have it.
Nayo sadaka ya dhambi ni kama ilivyo sadaka ya hatia. Ni sheria ileile hutumika kwa zote mbili. Zote ni mali ya kuhani azitumiaye kufanya upatanisho.
8 And the priest that offereth any man's burnt-offering, even the priest shall have to himself the skin of the burnt-offering which he hath offered.
Kuhani atoaye sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuchuku ngozi ya sadaka hiyo kwa ajili yake mwenyewe.
9 And every meal-offering that is baked in the oven, and all that is dressed in the stewing-pan, and on the griddle, shall be the priest's that offereth it.
Kila sadaka ya nafaka inayookwa mekoni, na kila sadaka kama hiyo ipikwayo kaangoni au kwenye sufuria itakuwa ya kuhani aitoaye.
10 And every meal-offering, mingled with oil, or dry, shall all the sons of Aaron have, one as well as another.
Kila sadaka ya nafaka, ama iwe unga mkavu au uliochanganywa na mafuta ya zeitu itakuwa ya ukoo wa Aroni kwa usawa.
11 And this is the law of the sacrifice of peace-offerings, which one may offer unto the LORD.
Hii ndiyo sheria ya dhabihu ya sadaka za amani, ambazo watu watazitoa kwa Yahweh.
12 If he offer it for a thanksgiving, then he shall offer with the sacrifice of thanksgiving unleavened cakes mingled with oil, and unleavened wafers spread with oil, and cakes mingled with oil, of fine flour soaked.
Iwapo mtu yeyote anaitoa ili kuonyesha shukrani kwa Yahweh, basi ataitoa pamoja na dhabih uya mikate iliyotengenezwa bila hamira, bali kwa mafuta ya zeituni yaliyochanganywa na unga lakini bila hamira, na maandazi yaliyotengenezwa bila hamira, bali yaliyopakwa mafuta juu yake, na mikate miembamba iliyofanywa kwa unga laini uliochanganywa na mafuta.
13 With cakes of leavened bread he shall present his offering with the sacrifice of his peace-offerings for thanksgiving.
Kwa kusudi la kutoa shukrani, pia anapaswa kutoa pamoja na sadaka yake ya amani, vipande vya mikate iliyotiwa hamira.
14 And of it he shall present one out of each offering for a gift unto the LORD; it shall be the priest's that dasheth the blood of the peace-offerings against the altar.
Ni lazima atatoa moja kila aina ya sadaka hizi kama sadaka iliyoletwa kwa Yahweh. Nayo itakuwa ya makuhani wanaonyunyizia damu ya sadaka ya amani kwenye madhabahu.
15 And the flesh of the sacrifice of his peace-offerings for thanksgiving shall be eaten on the day of his offering; he shall not leave any of it until the morning.
Mtu anayeleta sadaka ya amani kwa kusudi la kutoa shukrani ni lazima ataila nyama ya sadaka yake siku ya kutoa dhabihu. Hatakiwi kusaza chochote kilicho cha sadaka hiyo hata asubuhi ya pili.
16 But if the sacrifice of his offering be a vow, or a freewill-offering, it shall be eaten on the day that he offereth his sacrifice; and on the morrow that which remaineth of it may be eaten.
Lakini iwapo dhabihu ya matoleo yake kusudi lake ni nadhiri, au kwa kusudi la sadaka ya hiari, nyama yake italiwa siku iyo hiyo aitoapo dhabihu yake, lakini chochote kinachosalia cha sadaka hiyo kinaweza kuliwa siku inayofuata.
17 But that which remaineth of the flesh of the sacrifice on the third day shall be burnt with fire.
Hata hivyo, nyama yoyote ya dhabihu inayobaki siku ya tatu ni lazima ichomwe moto.
18 And if any of the flesh of the sacrifice of his peace-offerings be at all eaten on the third day, it shall not be accepted, neither shall it be imputed unto him that offereth it; it shall be an abhorred thing, and the soul that eateth of it shall bear his iniquity.
Iwapo kipande chochote cha nyama hiyo ya dhabihu kinachobaki kinaliwa katika siku ya tatu, hakitakubalika, wala hakitatolewa kwa aliyeitoa. Kitakuwa ni kitu cha kuchukiza, na mtu akilaye atabeba hatia ya dhambi mwenyewe yake.
19 And the flesh that toucheth any unclean thing shall not be eaten; it shall be burnt with fire. And as for the flesh, every one that is clean may eat thereof.
Nyama yoyote inayogusa kitu kilicho najisi haitaliwa. Ni lazima ichomwe moto. Na kwa ajili ya nyama inayobaki, yeyote aliye safi anaweza kuila.
20 But the soul that eateth of the flesh of the sacrifice of peace-offerings, that pertain unto the LORD, having his uncleanness upon him, that soul shall be cut off from his people.
Hata hivyo, mtu najisi anayekula nyama kutoka kwenye dhabihu ya matoleo ya amani ambayo ni ya Yahweh yapasa mtu huyu akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
21 And when any one shall touch any unclean thing, whether it be the uncleanness of man, or an unclean beast, or any unclean detestable thing, and eat of the flesh of the sacrifice of peace-offerings, which pertain unto the LORD, that soul shall be cut off from his people.
Iwapo mtu yeyote anagusa kitu chochote kilichonajisi—iwe ni unajisi wa binadamu, au wa mnyama aliyenajisi, au wa kitu fulani kilichonajisi na chenye kuchukiza, na kisha akala baadhi ya nyama ya dhabihu ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Yahweh, lazima mtu huyo akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
22 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Kisha Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
23 Speak unto the children of Israel, saying: Ye shall eat no fat, of ox, or sheep, or goat.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'hamruhusiwi kula mafuta ya fahali au kondoo au mbuzi.
24 And the fat of that which dieth of itself, and the fat of that which is torn of beasts, may be used for any other service; but ye shall in no wise eat of it.
Mafuta ya mnyama yoyote afaye peke yake bila ya kuwa dhabihu, au mafuta ya mnyama yeyote aliyeraruliwa na wanyama pori, yanaweza kutumika kwa makusudi mengine, lakini hakika hamtayala.
25 For whosoever eateth the fat of the beast, of which men present an offering made by fire unto the LORD, even the soul that eateth it shall be cut off from his people.
Yeyote atakayekula mafuta ya mnyama ambayo watu wanaweza kuyatoa kuwa dhabihu ya iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, mtu huyo lazima atakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake.
26 And ye shall eat no manner of blood, whether it be of fowl or of beast, in any of your dwellings.
Hamtakula damu yoyote katika mojawapo ya nyumba zenu, ama iwe kutoka kwa ndege au mnyama.
27 Whosoever it be that eateth any blood, that soul shall be cut off from his people.
Yeyote alaye damu yoyote, mtu huyo lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.'”
28 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Kwa hiyo Yahweh akazungumza na Musa na akasema,
29 Speak unto the children of Israel, saying: He that offereth his sacrifice of peace-offerings unto the LORD shall bring his offering unto the LORD out of his sacrifice of peace-offerings.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Yeye atoaye dhabidhu ya sadaka ya amani kwa Yahweh lazima alete sehemu ya dhabihu yake kwa Yahweh.
30 His own hands shall bring the offerings of the LORD made by fire: the fat with the breast shall he bring, that the breast may be waved for a wave-offering before the LORD.
Mikono yake mwenyewe lazima iilete hiyo sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto. Naye atayaleta hayo mafuta pamoja na kidari, ili kwamba kidari kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
31 And the priest shall make the fat smoke upon the altar; but the breast shall be Aaron's and his sons'.
Kuhani atayachoma mafuta hayo juu ya madhabahu, lakini kile kidari kitakuwa mali ya Aroni na uzao wake.
32 And the right thigh shall ye give unto the priest for a heave-offering out of your sacrifices of peace-offerings.
Ni lazima utatoa paja la kulia kwa kuhani kama sadaka iliyotokana na dhabihu ya sadaka yako ya amani.
33 He among the sons of Aaron, that offereth the blood of the peace-offerings, and the fat, shall have the right thigh for a portion.
Yule kuhani, mmoja wa wazao wa Aroni, atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani—ni lazima atapata paja la kulia kama mgao wake wa sadaka.
34 For the breast of waving and the thigh of heaving have I taken of the children of Israel out of their sacrifices of peace-offerings, and have given them unto Aaron the priest and unto his sons as a due for ever from the children of Israel.
Kwa kuwa nimetwaa kidari, na paja la sadaka ya kutikiswa kutoka kwa watu wa Israeli uwe mchango wao, na amepewa Aroni kuhani na wanawe kuwa mgao wao wa kawaida.
35 This is the consecrated portion of Aaron, and the consecrated portion of his sons, out of the offerings of the LORD made by fire, in the day when they were presented to minister unto the LORD in the priest's office;
Huu ndiyo mgao wa Aroni na uzao wake utokanao na matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, siku ile Musa alipowaweka wakfu ili kumtumikia Yahweh katika kazi ya kuhani.
36 which the LORD commanded to be given them of the children of Israel, in the day that they were anointed. It is a due for ever throughout their generations.
Huu ndio mgao ambao Yahweh aliamru waweze kupewa kutoka kwa watu wa Israeli, katika siku hiyo aliyowatia mafuta ya upako wawe makuhani. Nao utakuwa mgao wao wa kila siku katika vizazi vyote.
37 This is the law of the burnt-offering, of the meal-offering, and of the sin-offering, and of the guilt-offering, and of the consecration-offering, and of the sacrifice of peace-offerings;
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya kuteketezwa, ya sadaka ya nafaka, ya sadaka ya dhambi, ya sadaka ya hatia, ya sadaka ya kuweka wakfu, na ya dhabihu, ya sadaka za amani,
38 which the LORD commanded Moses in mount Sinai, in the day that he commanded the children of Israel to present their offerings unto the LORD, in the wilderness of Sinai.
ni sheria ambazo Yahweh alizitoa kwa Musa kwenye Mlima Sinai siku aliyowaamru watu wa Israeli kutoa dhabihu zao kwa Yahweh katika jangwa la Sinai.'”

< Leviticus 7 >