< Leviticus 10 >

1 And Nadab and Abihu, the sons of Aaron, took each of them his censer, and put fire therein, and laid incense thereon, and offered strange fire before the LORD, which He had not commanded them.
Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua kila mtu kifukizo chake, akaweka moto ndani yake, na kisha uvumba. Kisha wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa.
2 And there came forth fire from before the LORD, and devoured them, and they died before the LORD.
Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh na kuwala, nao wakafa mbele za Yahweh.
3 Then Moses said unto Aaron: 'This is it that the LORD spoke, saying: Through them that are nigh unto Me I will be sanctified, and before all the people I will be glorified.' And Aaron held his peace.
Kisha Musa akamwambia Aroni, Hivi ndiyo Yahweh alivyokuwa akizunguzia aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wajao mbele zangu. Nami nitatukuzwa mbele za watu wote.'” Naye Aroni hakusema neno lolote.
4 And Moses called Mishael and Elzaphan, the sons of Uzziel the uncle of Aaron, and said unto them: 'Draw near, carry your brethren from before the sanctuary out of the camp.'
Musa akamwita Mishaeli na Elzafani, wana wa Uzieli mjomba wa Aroni, naye akamwambia, “njoo huku na uwatowe ndugu zako nje ya kambi watoke mbele ya hema.”
5 So they drew near, and carried them in their tunics out of the camp, as Moses had said.
Hivyo wakakaribia na kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani, nao wakawapeleka nje ya kambi, kama Musa alivyokuwa ameelekeza. Kisha Musa akamwambia Aroni na wanawe wengine wawili, Eliezari na Ithamari, “
6 And Moses said unto Aaron, and unto Eleazar and unto Ithamar, his sons: 'Let not the hair of your heads go loose, neither tend your clothes, that ye die not, and that He be not wroth with all the congregation; but let your brethren, the whole house of Israel, bewail the burning which the LORD hath kindled.
Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu, ili kwamba msije mkafa, na kwamba Yahweh asilikasirikie kusanyiko zima. Lakini waacheni jamaa zenu, nyumba yote ya Israeli waweze kufanya ibada za maombolezo kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto.
7 And ye shall not go out from the door of the tent of meeting, lest ye die; for the anointing oil of the LORD is upon you.' And they did according to the word of Moses.
Msiende nje kutoka kwenye ingilio la hema la kukutania, ama sivyo mtakufa, kwa kuwa mafuta ya Yahweh ya upako yako juu yenu.” Kwa hiyo wakatenda sawasawa na maelekezo ya Musa.
8 And the LORD spoke unto Aaron, saying:
Mungu akazungumza na Aroni, akisema,
9 'Drink no wine nor strong drink, thou, nor thy sons with thee, when ye go into the tent of meeting, that ye die not; it shall be a statute forever throughout your generations.
“Msinywe mvinyo wala kinywaji kikali, wewe, au wanao wanaobaki pamoja nawe, ili kwamba mtakapoingia kwenye hema ya kukutania msije mkafa. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu,
10 And that ye may put difference between the holy and the common, and between the unclean and the clean;
ili kupaambanua kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida, na kati ya najisi na safi,
11 and that ye may teach the children of Israel all the statutes which the LORD hath spoken unto them by the hand of Moses.'
ili kwamba mweze kuwafundisha watu wa Israeli amri zote ambazo Yahweh ameziamru kwa kinywa cha Musa.
12 And Moses spoke unto Aaron, and unto Eleazar and unto Ithamar, his sons that were left: 'Take the meal-offering that remaineth of the offerings of the LORD made by fire, and eat it without leaven beside the altar; for it is most holy.
Musa akazungumza na Aroni na wanawe wawili waliosalia; Eliazari naIthamari, Twaeni sadaka ya nafaka inayobaki kutokana na sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto, nanyi ileni kando ya madhabahu bila hamiara, kwa kuwa ni takatifu sana.
13 And ye shall eat it in a holy place, because it is thy due, and thy sons' due, of the offerings of the LORD made by fire; for so I am commanded.
lazima mtaila mahali patatifu kwa sababu huo ni mgao wako wewe na mgao wa wanao wa matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, kwa kuwa hivi ndivyo limeamriwa niwaambie.
14 And the breast of waving and the thigh of heaving shall ye eat in a clean place; thou, and thy sons, and thy daughters with thee; for they are given as thy due, and thy sons' due, out of the sacrifices of the peace-offerings of the children of Israel.
Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh, yapasa mzile mahali palipo safi panapokubalika kwa Mungu. Wewe mwenyewe, wanao na binti zako waliopamoja nawe mtakula sehemu hizo, kwa kuwa zimetolewa kuwa mgao wako na mgao wa wanao kutokana na dhabihu ya sadaka ya ushirika wa watu wa Israeli.
15 The thigh of heaving and the breast of waving shall they bring with the offerings of the fat made by fire, to wave it for a wave-offering before the LORD; and it shall be thine, and thy sons' with thee, as a due for ever; as the LORD hath commanded.'
Lile paja lililotolewa na kidari kilichotikiswa, ni lazima ziletwe pamoja na sadaka ya mafuta iliyofanywa kwa moto, ili kutikiswa mbele za Yahweh. Nazo zitakuwa zako wewe na wanao kuwa mgao wenu daima, kama Yahweh alivyoamru.
16 And Moses diligently inquired for the goat of the sin-offering, and, behold, it was burnt; and he was angry with Eleazar and with Ithamar, the sons of Aaron that were left, saying:
Kisha Musa akauliza kuhusu yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye akagundua kwamba alikuwa ametekezwa kwa moto. Kwa hiyo akawakasirikia Eliazari na Ithamari, wana wa Aroni waliosalia; akawaambia,
17 'Wherefore have ye not eaten the sin-offering in the place of the sanctuary, seeing it is most holy, and He hath given it you to bear the iniquity of the congregation, to make atonement for them before the LORD?
“Kwa nini hamjaila sadaka ya dhambi katika eneo la hema, kwa kuwa ni takatifu sana, na kwa kuwa Yahweh amishaitoa kwenu ili kuchukua uovu wa kusanyiko, ili kufanya upatanisho kwa aijli yao mbele zake?
18 Behold, the blood of it was not brought into the sanctuary within; ye should certainly have eaten it in the sanctuary, as I commanded.'
Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema, kwa hiyo iliwapasa kwa hakika kuwa mekwisha ila kwenye eneo la hema, kama nilivyoagiza?
19 And Aaron spoke unto Moses: 'Behold, this day have they offered their sin-offering and their burnt-offering before the LORD, and there have befallen me such things as these; and if I had eaten the sin-offering to-day, would it have been well-pleasing in the sight of the LORD?
Kisha Aroni akamjibu Musa, “Tazama, leo walitoa sadaka yao ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa mbele za Yahweh, na jambo hili vilevile limetendeka kwangu leo. Ikiwa nimeshakula sadaka ya dhambi leo, Je! Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?”
20 And when Moses heard that, it was well-pleasing in his sight.
Naye Musa aliposikia hivyo, akaridhika.

< Leviticus 10 >