< Lamentations 4 >

1 How is the gold become dim! How is the most fine gold changed! The hallowed stones are poured out at the head of every street.
Dhahabu imechakaa; jinsi gani dhahabu safi imebadilika! Mawe matakatifu yamezagaa katika kila njia ya mtaa.
2 The precious sons of Zion, comparable to fine gold, how are they esteemed as earthen pitchers, the work of the hands of the potter!
Wana wa dhamani wa Sayuni walikuwa na dhamani ya uzito wa dhahabu safi, lakini sasa hawana dhamani zaidi ya majagi ya udogo, kazi ya mikono ya mfinyazi!
3 Even the jackals draw out the breast, they give suck to their young ones; the daughter of my people is become cruel, like the ostriches in the wilderness.
Ata mbwa wa mitaani wanatoa maziwa yao kuwanyonyesha watoto wao, lakini binti wa watu wangu amekuwa katili, kama mbuni katika jangwa.
4 The tongue of the sucking child cleaveth to the roof of his mouth for thirst; the young children ask bread, and none breaketh it unto them.
Ulimi wa mtoto mchanga anaye nyonya unagota juu mdomo wake kwa kiu; watoto wanaomba chakula, lakini hakuna kwa ajili yao.
5 They that did feed on dainties are desolate in the streets; they that were brought up in scarlet embrace dunghills.
Wao walizoea kula chakula cha gharama sasa wana shinda njaa mitaani; wao walio lelewa kwa kuvaa nguo za zambarau, sasa wamelala katika majalala.
6 For the iniquity of the daughter of my people is greater than the sin of Sodom, that was overthrown as in a moment, and no hands fell upon her.
Hukumu ya binti wa watu wangu ni kubwa kuliko hiyo ya Sodoma, na ilipinduliwa kwa dakika na hakuna aliye yanyua mkono kumsaidia.
7 Her princes were purer than snow, they were whiter than milk, they were more ruddy in body than rubies, their polishing was as of sapphire;
Viongozi wake walikuwa wasafi kuliko theluji, weupe kuliko maziwa; miili yao ilikuwa imara kuliko jiwe, mwili wao ulikuwa kama yakuti samawi.
8 Their visage is blacker than coal; they are not known in the streets; their skin is shrivelled upon their bones; it is withered, it is become like a stick.
Muonekano wao umekuwa mweusi kama giza; hawatambuliki mitaani. Ngozi zao zimesinya kwenye mifupa yao; imekuwa kavu kama kuni.
9 They that are slain with the sword are better than they that are slain with hunger; for these pine away, stricken through, for want of the fruits of the field.
Hao walio uawa kwa upanga walikuwa na furaha zaidi kuliko hao walio kufa kwa njaa, walio potea, wakatobolewa kwa ukosefu wa mavuno shambani.
10 The hands of women full of compassion have sodden their own children; they were their food in the destruction of the daughter of my people.
Mikono ya wanawake wenye huruma imewachemsha watoto wao; wamekuwa chakula chao wakati ambapo binti wa watu wangu alipo kuwa akiharibiwa.
11 The LORD hath accomplished His fury, He hath poured out His fierce anger; and He hath kindled a fire in Zion, which hath devoured the foundations thereof.
Yahweh alionyesha gadhabu yake yote; alimwaga hasira yake kali. Aliwasha moto Sayuni uliteketeza misingi yake.
12 The kings of the earth believed not, neither all the inhabitants of the world, that the adversary and the enemy would enter into the gates of Jerusalem.
Wafalme wa dunia hawaku amini, wala wakazi wa dunia, kwamba maadui au wapinzani waliweza kuingia malangoni ya Yerusalemu.
13 It is because of the sins of her prophets, and the iniquities of her priests, that have shed the blood of the just in the midst of her.
Haya yalitokea kwasababu ya dhambi za manabii na na maasi ya makuhani walio mwaga damu ya wenye haki mbele zake.
14 They wander as blind men in the streets, they are polluted with blood, so that men cannot touch their garments.
Walitanga, kwa upofu, mitaani. Walikuwa wamejitia unajisi kwa damu hiyo ambapo hakuna aliye ruhusiwa kushika nguo zao.
15 'Depart ye! unclean!' men cried unto them, 'Depart, depart, touch not'; yea, they fled away and wandered; men said among the nations: 'They shall no more sojourn here.'
“Kaa mbali! Wewe mnajisi!” Watu waliwapazia sauti. “Kaa mbali! Kaa mbali! Usiguse!” Hivyo wakatanga; watu walisema miongoni mwa mataifa, “Hawawezi kukaa hapa tena.”
16 The anger of the LORD hath divided them; He will no more regard them; they respected not the persons of the priests, they were not gracious unto the elders.
Yahweh mwenyewe akawatawanyisha; hawatazami tena. Hawa waheshimu makuhani, na hawaonyeshi upendeleo kwa wazee.
17 As for us, our eyes do yet fail for our vain help; in our watching we have watched for a nation that could not save.
Macho yetu yalikwama, yakitazama bure kwa msaada; kutoka minara yetu ya ulinzi tulitazama taifa lisilo weza tuokoa.
18 They hunt our steps, that we cannot go in our broad places; our end is near, our days are fulfilled; for our end is come.
Walifuata hatua zetu, hatukuweza kutembea mitaani mwetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu na siku zetu zilihesabiwa, mwisho wetu ulifika.
19 Our pursuers were swifter than the eagles of the heaven; they chased us upon the mountains, they lay in wait for us in the wilderness.
Walio tukimbiza walikuwa wepesi kuliko tai wa aangani. Walitukimbiza kwenye milima na kutuwinda nyikani.
20 The breath of our nostrils, the anointed of the LORD, was taken in their pits; of whom we said: 'Under his shadow we shall live among the nations.'
Pumzi katika pua zetu - mpakwa mafuta wa Yahweh - ndiye aliye kamatwa katika shimo; ambaye ndiye aliye semewa, “Chini ya kivuli chake tutaishi miongoni mwa mataifa.”
21 Rejoice and be glad, O daughter of Edom, that dwellest in the land of Uz: the cup shall pass over unto thee also; thou shalt be drunken, and shalt make thyself naked.
Shangilia na ufurahi, binti wa Edomu, wewe unaye ishi nchi ya Uzi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa; utalewa na kuvua nguo.
22 The punishment of thine iniquity is accomplished, O daughter of Zion, He will no more carry thee away into captivity; He will punish thine iniquity, O daughter of Edom, He will uncover thy sins.
Binti wa Sayuni, hukumu yako itafika mwisho, hataongeza mateka yako lakini binti wa Edomu, ata muhadhibu; ata funua dhambi zako.

< Lamentations 4 >