< Judges 15 >

1 But it came to pass after a while, in the time of wheat harvest, that Samson visited his wife with a kid; and he said: 'I will go in to my wife into the chamber.' But her father would not suffer him to go in.
Baada ya siku kadhaa, wakati wa mavuno ya ngano, Samsoni akachukua mbuzi mdogo akaenda kumtembelea mkewe. Akajiambia mwenyewe, “Nitaenda kwenye chumba cha mke wangu.” Lakini baba yake hakumruhusu aingie.
2 And her father said: 'I verily thought that thou hadst utterly hated her; therefore I gave her to thy companion; is not her younger sister fairer than she? take her, I pray thee, instead of her.'
Baba yake akasema, “Nilidhani umemchukia, hivyo nikampatia rafiki yako. Dada yake mdogo ni mzuri kuliko yeye, Mchukue badala yake.”
3 And Samson said unto them: 'This time shall I be quits with the Philistines, when I do them a mischief.'
Samsoni akawaambia, 'Wakati huu sitakuwa na hatia juu ya Wafilisti wakati nikiwaumiza.'
4 And Samson went and caught three hundred foxes, and took torches, and turned tail to tail, and put a torch in the midst between every two tails.
Samsoni akaenda na kukamata mbweha mia tatu akawafunga pamoja kila jozi, mkia hadi mkia. Kisha akachukua taa na kuzifunga katikati ya kila mkia.
5 And when he had set the torches on fire, he let them go into the standing corn of the Philistines, and burnt up both the shocks and the standing corn, and also the oliveyards.
Alipokwisha kuviwasha moto vienge, akawaachia mbweha katika nafaka za Wafilisti zilizosimama, nao wakawasha moto nafaka zote zilizopandwa, na nafaka iliyosimama shambani, pamoja na mashamba ya mizabibu na mizeituni.
6 Then the Philistines said: 'Who hath done this?' And they said: 'Samson, the son-in-law of the Timnite, because he hath taken his wife, and given her to his companion.' And the Philistines came up, and burnt her and her father with fire.
Wafilisti waliuliza, “Ni nani aliyefanya hili?” Wakaambiwa, “Samsoni, mkwe wa Mtimna alifanya hivyo kwa sababu Mtimna alimchukua mke wa Samsoni akampa rafiki yake.” Basi Wafilisti wakamwendea wakamchoma kwa moto yeye na baba yake.
7 And Samson said unto them: 'If ye do after this manner, surely I will be avenged of you, and after that I will cease.'
Samsoni akawaambia, “Ikiwa ndivyo mnavyofanya, nitalipiza kisasi juu yenu, na baada ya hayo, nitaacha.”
8 And he smote them hip and thigh with a great slaughter; and he went down and dwelt in the cleft of the rock of Etam.
Kisha akawakata vipande vipande, paja na mguu, kwa kuwauwa sana. Kisha akashuka chini akaishi katika pango katika mwamba wa Etamu.
9 Then the Philistines went up, and pitched in Judah, and spread themselves against Lehi.
Ndipo Wafilisti wakaja, wakajitahidi kupigana vita huko Yuda, wakaanzisha jeshi lao huko Lehi.
10 And the men of Judah said: 'Why are ye come up against us?' And they said: 'To bind Samson are we come up, to do to him as he hath done to us.'
Watu wa Yuda wakasema, “Kwa nini mmekuja kutupiga?” Wakasema, “Tunashambulia ili tuweze kumkamata Samsoni, na tumtendee kama alivyotutendea.”
11 Then three thousand men of Judah went down to the cleft of the rock of Etam, and said to Samson: 'Knowest thou not that the Philistines are rulers over us? what then is this that thou hast done unto us?' And he said unto them: 'As they did unto me, so have I done unto them.'
Kisha watu elfu tatu wa Yuda wakashuka hata kwenye pango la Eatamu, wakamwambia Samsoni, “Je, hujui kwamba Wafilisti hutawala juu yetu? Je! umetutendea nini?” Samsoni akawaambia, “Kwa kadili walivyonitendea mimi, vivyo hivyo nimewatendea wao.”
12 And they said unto him: 'We are come down to bind thee, that we may deliver thee into the hand of the Philistines.' And Samson said unto them: 'Swear unto me, that ye will not fall upon me yourselves.'
Wakamwambia Samsoni, “Tumeshuka kukufunga na kukutia mikononi mwa Wafilisti.” Samsoni akawaambia, “Niapieni kwamba hamtaniua ninyi wenyewe.”
13 And they spoke unto him, saying: 'No; but we will bind thee fast, and deliver thee into their hand; but surely we will not kill thee.' And they bound him with two new ropes, and brought him up from the rock.
Wakamwambia, “La, tutakufunga tu kwa kamba na kukupeleka kwao. Tunakuahidi sisi hatutakuua.” Kisha wakamfunga na kamba mbili mpya na kumleta kutoka kwenye mwamba.
14 When he came unto Lehi, the Philistines shouted as they met him; and the spirit of the LORD came mightily upon him, and the ropes that were upon his arms became as flax that was burnt with fire, and his bands dropped from off his hands.
Alipofika Lehi, Wafilisti walipiga kelele walipokutana naye. Kisha Roho wa Bwana akaja juu yake kwa nguvu. Kamba zilizokuwa juu ya mikono yake zikawa kama kitambaa cha kuteketezwa, na zikaanguka mikononi mwake.
15 And he found a new jawbone of an ass, and put forth his hand, and took it, and smote a thousand men therewith.
Samsoni alipata mfupa mbichi wa taya ya punda, naye akaichukua na kuua watu elfu kwa mfupa huo.
16 And Samson said: With the jawbone of an ass, heaps upon heaps, with the jawbone of an ass have I smitten a thousand men.
Samsoni akasema, “Kwa taya ya punda, chungu juu ya chungu, na njaa ya punda nimewaua watu elfu.”
17 And it came to pass, when he had made an end of speaking, that he cast away the jawbone out of his hand; and that place was called Ramath-lehi.
Samsoni alipomaliza kuzungumza, akatupa taya, na akaita mahali pale Ramath Lehi.
18 And he was sore athirst, and called on the LORD, and said: 'Thou hast given this great deliverance by the hand of Thy servant; and now shall I die for thirst, and fall into the hand of the uncircumcised?'
Samsoni alikuwa na kiu sana akamwita Bwana na kusema, “Umempa mtumishi wako ushindi mkubwa. Lakini sasa nitakufa kwa kiu na kuanguka mikononi mwa wale wasiootahiriwa?”
19 But God cleaved the hollow place that is in Lehi, and there came water thereout; and when he had drunk, his spirit came back, and he revived; wherefore the name thereof was called En-hakkore, which is in Lehi unto this day.
Na Mungu akapafungua mahali pa shimo palipo katika Lehi, na maji yakatoka. Alipokunywa, nguvu zake zikarejea na akahuishwa. Kwa hiyo aliita jina la mahali hapo Enhakore, na ni huko Lehi hadi leo.
20 And he judged Israel in the days of the Philistines twenty years.
Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli katika siku za Wafilisti kwa miaka ishirini.

< Judges 15 >