< Jonah 2 >

1 Then Jonah prayed unto the LORD his God out of the fish's belly.
Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
2 And he said: I called out of mine affliction unto the LORD, and He answered me; out of the belly of the nether-world cried I, and Thou heardest my voice. (Sheol h7585)
Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol h7585)
3 For Thou didst cast me into the depth, in the heart of the seas, and the flood was round about me; all Thy waves and Thy billows passed over me.
Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
4 And I said: 'I am cast out from before Thine eyes'; yet I will look again toward Thy holy temple.
Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
5 The waters compassed me about, even to the soul; the deep was round about me; the weeds were wrapped about my head.
Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
6 I went down to the bottoms of the mountains; the earth with her bars closed upon me for ever; yet hast Thou brought up my life from the pit, O LORD my God.
Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
7 When my soul fainted within me, I remembered the LORD; and my prayer came in unto Thee, into Thy holy temple.
“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
8 They that regard lying vanities forsake their own mercy.
“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
9 But I will sacrifice unto Thee with the voice of thanksgiving; that which I have vowed I will pay. Salvation is of the LORD.
Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
10 And the LORD spoke unto the fish, and it vomited out Jonah upon the dry land.
Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.

< Jonah 2 >