< Joel 2 >

1 Blow ye the horn in Zion, and sound an alarm in My holy mountain; let all the inhabitants of the land tremble; for the day of the LORD cometh, for it is at hand;
Piga tarumbeta katika Sayuni, na piga kelele juu ya mlima wangu mtakatifu! Wakazi wote wa nchi watetemeke kwa hofu; maana siku ya Bwana inakuja; Hakika iko karibu.
2 A day of darkness and gloominess, a day of clouds and thick darkness, as blackness spread upon the mountains; a great people and a mighty, there hath not been ever the like, neither shall be any more after them, even to the years of many generations.
Ni siku ya giza na weusi, siku ya mawingu na giza nene. Kama asubuhi inayoenea kwenye milima, jeshi kubwa na la nguvu linakaribia. Hakujawahi kuwako jeshi kama hilo, na hakutakuwa tena, hata baada ya vizazi vingi.
3 A fire devoureth before them, and behind them a flame blazeth; the land is as the garden of Eden before them, and behind them a desolate wilderness; yea, and nothing escapeth them.
Moto unatumia kila kitu mbele yake, na nyuma yake moto unawaka. Nchi hiyo ni kama bustani ya Edeni mbele yake, lakini nyuma yake kuna jangwa lililoharibika. Hakika hakuna chochote kitakayotoroka.
4 The appearance of them is as the appearance of horses; and as horsemen, so do they run.
Muonekano wa jeshi ni kama farasi, na wanakimbia kama wapanda farasi.
5 Like the noise of chariots, on the tops of the mountains do they leap, like the noise of a flame of fire that devoureth the stubble, as a mighty people set in battle array.
Wanaruka kwa kelele kama ile ya magari juu ya vilele vya milima, kama kelele za muale wa moto ambao huangamiza majani, kama jeshi la nguvu lililo tayari kwa vita.
6 At their presence the peoples are in anguish; all faces have gathered blackness.
Mbele yao watu wako katika maumivu na nyuso zao zote zinakuwa za rangi.
7 They run like mighty men, they climb the wall like men of war; and they move on every one in his ways, and they entangle not their paths.
Wanakimbia kama wapiganaji wenye nguvu; wanapanda kuta kama askari; wanasonga, kila mmoja kwa hatua, na hawavunji safu zao.
8 Neither doth one thrust another, they march every one in his highway; and they break through the weapons, and suffer no harm.
Wala hakuna mmoja anayemsukuma mwingine kando; wanasonga, kila mmoja katika njia yake; wao huvunja kwa njia ya ulinzi na si kuanguka nje ya mstari.
9 They leap upon the city, they run upon the wall, they climb up into the houses; they enter in at the windows like a thief.
Wanakimbilia jiji, wanakimbia kwenye ukuta, wanapanda ndani ya nyumba, na hupita kupitia madirisha kama wezi.
10 Before them the earth quaketh, the heavens tremble; the sun and the moon are become black, and the stars withdraw their shining.
Nchi hutikisika mbele yao, mbingu hutetemeka, jua na mwezi ni giza, na nyota zinaacha kuangaza.
11 And the LORD uttereth His voice before His army; for His camp is very great, for he is mighty that executeth His word; for great is the day of the LORD and very terrible; and who can abide it?
Bwana huinua sauti yake mbele ya jeshi lake; maana wapiganaji wake ni wengi sana; kwa maana wao ni wenye nguvu, wale wanaofanya amri zake. Kwa maana siku ya Bwana ni kubwa na ya kutisha sana. Nani anayeweza kuishi?
12 Yet even now, saith the LORD, turn ye unto Me with all your heart, and with fasting, and with weeping, and with lamentation;
“Lakini hata sasa,” asema Bwana, “Nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote. Haraka, lia na omboleza.”
13 And rend your heart, and not your garments, and turn unto the LORD your God; for He is gracious and compassionate, long-suffering, and abundant in mercy, and repenteth Him of the evil.
Rarueni miyoyo yenu, si mavazi yenu tu, na kurudi kwa Bwana Mungu wenu. Kwa maana ni mwenye neema na mwenye huruma, si mwepesi wa hasira na wingi katika uaminifu wa agano, na angependa kugeuka kutokana na adhabu.
14 Who knoweth whether He will not turn and repent, and leave a blessing behind Him, even a meal-offering and a drink-offering unto the LORD your God?
Nani anajua? Labda angegeuka na kuwa na huruma, na kuacha baraka nyuma yake, sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji kwa Bwana, Mungu wenu?
15 Blow the horn in Zion, sanctify a fast, call a solemn assembly;
Piga tarumbeta huko Sayuni, itisha kwa ajili ya funga takatifu, na itisheni kusanyiko takatifu.
16 Gather the people, sanctify the congregation, assemble the elders, gather the children, and those that suck the breasts; let the bridegroom go forth from his chamber, and the bride out of her pavilion.
Kusanyeni watu, wito kwa kusanyiko takatifu. Kusanya wazee, kukusanya watoto na watoto wachanga. Bwana arusi waweze kutoka nje ya vyumba vyao, na bibi arusi kutoka kwenye vyumba vyao.
17 Let the priests, the ministers of the LORD, weep between the porch and the altar, and let them say: 'Spare thy people, O LORD, and give not Thy heritage to reproach, that the nations should make them a byword: wherefore should they say among the peoples: Where is their God?'
Basi makuhani, watumishi wa Bwana, waliao kati ya patakatifu na madhabahu. Wawaambie, Waitie watu wako, Ee Bwana, wala usitoe urithi wako kwa aibu, ili mataifa watawawale juu yao. Kwa nini wanapaswa kusema kati ya mataifa, “Yuko wapi Mungu wao?”
18 Then was the LORD jealous for His land, and had pity on His people.
Ndipo Bwana alikuwa mwenye bidii kwa nchi yake na kuwahurumia watu wake.
19 And the LORD answered and said unto His people: 'Behold, I will send you corn, and wine, and oil, and ye shall be satisfied therewith; and I will no more make you a reproach among the nations;
Bwana akawajibu watu wake, Tazama, nitawaletea nafaka, divai mpya, na mafuta. Utaridhishwa nao, wala sitawafanya kuwa aibu kati ya mataifa.
20 But I will remove far off from you the northern one, and will drive him into a land barren and desolate, with his face toward the eastern sea, and his hinder part toward the western sea; that his foulness may come up, and his ill savour may come up, because he hath done great things.'
Nitawaondoa washambuliaji wa kaskazini mbali nanyi, na nitawapitisha katika nchi kavu na iliyoachwa. Sehemu ya mbele ya jeshi lao itaingia bahari ya mashariki, na sehemuya nyuma itaingia bahari ya magharibi. Uvundo wake utainuka juu, na harufu yake mbaya itainuka juu. Hakika, amefanya mambo makuu.
21 Fear not, O land, be glad and rejoice; for the LORD hath done great things.
Msiogope, nchi, shangilieni na kufurahi, kwa kuwa Bwana atafanya mambo makuu.
22 Be not afraid, ye beasts of the field; for the pastures of the wilderness do spring, for the tree beareth its fruit, the fig-tree and the vine do yield their strength.
Usiogope, wanyama wa kondeni, kwa kuwa malisho ya jangwa yatakua, miti itazaa matunda yake, na miti ya mizabibu na mizabibu itazaa mavuno yao yote.
23 Be glad then, ye children of Zion, and rejoice in the LORD your God; for He giveth you the former rain in just measure, and He causeth to come down for you the rain, the former rain and the latter rain, at the first.
Furahini, enyi watu wa Sayuni, na kufurahi katika Bwana, Mungu wenu. Kwa maana atakupa mvua ya vuli kwa kiasi na kuleta mvua kwa ajili yenu, mvua ya vuli na mvua ya masika kama hapo awali.
24 And the floors shall be full of corn, and the vats shall overflow with wine and oil.
Sakafu ya kupepetea zitajaa ngano, na vyombo vitafurika kwa divai mpya na mafuta.
25 And I will restore to you the years that the locust hath eaten, the canker-worm, and the caterpiller, and the palmer-worm, My great army which I sent among you.
“Nitawawezesha miaka ya mazao ambayo nzige walikula, Palale, nzige, na nzige wakuteketeza - jeshi langu lenye nguvu ambalo nimelituma kati yenu.
26 And ye shall eat in plenty and be satisfied, and shall praise the name of the LORD your God, that hath dealt wondrously with you; and My people shall never be ashamed.
Mutakula chakula tele na kushiba, na kulitukuza jina la Bwana, Mungu wenu, aliyefanya miujiza kati yenu, wala sitawaletea tena watu wangu.
27 And ye shall know that I am in the midst of Israel, and that I am the LORD your God, and there is none else; and My people shall never be ashamed.
Utajua ya kwamba mimi niko kati ya Israeli, na kwamba mimi ni Bwana, Mungu wako, wala hakuna mwingine, wala sitawaletea aibu watu wangu.
28 And it shall come to pass afterward, that I will pour out My spirit upon all flesh; and your sons and your daughters shall prophesy, your old men shall dream dreams, your young men shall see visions;
Itakuwa baada ya hayo nitamimina Roho yangu juu ya wenye mwili yote, na wana wenu na binti zenu watatabiri. Wazee wenu wataota ndoto, vijana wenu wataona maono.
29 And also upon the servants and upon the handmaids in those days will I pour out My spirit.
Pia juu ya watumishi na watumishi wa kike, siku hizo nitaimimina Roho wangu.
30 And I will shew wonders in the heavens and in the earth, blood, and fire, and pillars of smoke.
Nitaonyesha maajabu mbinguni na duniani, damu, moto na nguzo za moshi.
31 The sun shall be turned into darkness, and the moon into blood, before the great and terrible day of the LORD come.
Jua litakuwa giza na mwezi kuwa damu, kabla ya siku kuu na ya kutisha ya Bwana itakapokuja.
32 And it shall come to pass, that whosoever shall call on the name of the LORD shall be delivered; for in mount Zion and in Jerusalem there shall be those that escape, as the LORD hath said, and among the remnant those whom the LORD shall call.
Itakuwa kwamba kila mtu anayeita jina la Yahweh ataokolewa. Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na Yerusalemu watakuwa na wale waliokoka, kama Bwana alivyosema, na kati ya wale walisalia, wale ambao Bwana anawaita.

< Joel 2 >