< Job 9 >

1 Then Job answered and said:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Of a truth I know that it is so; and how can man be just with God?
“kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
3 If one should desire to contend with Him, he could not answer Him one of a thousand.
Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
4 He is wise in heart, and mighty in strength; who hath hardened himself against Him, and prospered?
Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
5 Who removeth the mountains, and they know it not, when He overturneth them in His anger.
ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
6 Who shaketh the earth out of her place, and the pillars thereof tremble.
ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
7 Who commandeth the sun, and it riseth not; and sealeth up the stars.
Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
8 Who alone stretcheth out the heavens, and treadeth upon the waves of the sea.
ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
9 Who maketh the Bear, Orion, and the Pleiades, and the chambers of the south.
ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
10 Who doeth great things past finding out; yea, marvellous things without number.
Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11 Lo, He goeth by me, and I see Him not. He passeth on also, but I perceive Him not.
Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
12 Behold, He snatcheth away, who can hinder Him? Who will say unto Him: 'What doest Thou?'
Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
13 God will not withdraw His anger; the helpers of Rahab did stoop under Him.
Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14 How much less shall I answer Him, and choose out my arguments with Him?
Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
15 Whom, though I were righteous, yet would I not answer; I would make supplication to Him that contendeth with me.
Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
16 If I had called, and He had answered me; yet would I not believe that He would hearken unto my voice —
Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
17 He that would break me with a tempest, and multiply my wounds without cause;
kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
18 That would not suffer me to take my breath, but fill me with bitterness.
Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
19 If it be a matter of strength, lo, He is mighty! and if of justice, who will appoint me a time?
Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
20 Though I be righteous, mine own mouth shall condemn me; though I be innocent, He shall prove me perverse.
Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
21 I am innocent — I regard not myself, I despise my life.
Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
22 It is all one — therefore I say: He destroyeth the innocent and the wicked.
Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
23 If the scourge slay suddenly, He will mock at the calamity of the guiltless.
Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
24 The earth is given into the hand of the wicked; he covereth the faces of the judges thereof; if it be not He, who then is it?
Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
25 Now my days are swifter than a runner; they flee away, they see no good.
Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
26 They are passed away as the swift ships; as the vulture that swoopeth on the prey.
Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
27 If I say: 'I will forget my complaint, I will put off my sad countenance, and be of good cheer',
Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
28 I am afraid of all my pains, I know that Thou wilt not hold me guiltless.
Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 I shall be condemned; why then do I labour in vain?
Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
30 If I wash myself with snow water, and make my hands never so clean;
Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
31 Yet wilt Thou plunge me in the ditch, and mine own clothes shall abhor me.
Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
32 For He is not a man, as I am, that I should answer Him, that we should come together in judgment.
Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
33 There is no arbiter betwixt us, that might lay his hand upon us both.
Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
34 Let Him take His rod away from me, and let not His terror make me afraid;
Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
35 Then would I speak, and not fear Him; for I am not so with myself.
Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.

< Job 9 >