< Job 6 >
1 Then Job answered and said:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Oh that my vexation were but weighed, and my calamity laid in the balances altogether!
“Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
3 For now it would be heavier than the sand of the seas; therefore are my words broken.
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For the arrows of the Almighty are within me, the poison whereof my spirit drinketh up; the terrors of God do set themselves in array against me.
Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
5 Doth the wild ass bray when he hath grass? or loweth the ox over his fodder?
Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
6 Can that which hath no savour be eaten without salt? or is there any taste in the juice of mallows?
Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
7 My soul refuseth to touch them; they are as the sickness of my flesh.
Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
8 Oh that I might have my request, and that God would grant me the thing that I long for!
Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
9 Even that it would please God to crush me; that He would let loose His hand, and cut me off!
kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
10 Then should I yet have comfort; yea, I would exult in pain, though He spare not; for I have not denied the words of the Holy One.
Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11 What is my strength, that I should wait? and what is mine end, that I should be patient?
Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
12 Is my strength the strength of stones? or is my flesh of brass?
Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
13 Is it that I have no help in me, and that sound wisdom is driven quite from me?
Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
14 To him that is ready to faint kindness is due from his friend, even to him that forsaketh the fear of the Almighty.
Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
15 My brethren have dealt deceitfully as a brook, as the channel of brooks that overflow,
Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
16 Which are black by reason of the ice, and wherein the snow hideth itself;
ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
17 What time they wax warm, they vanish, when it is hot, they are consumed out of their place.
Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
18 The paths of their way do wind, they go up into the waste, and are lost.
Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
19 The caravans of Tema looked, the companies of Sheba waited for them —
Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
20 They were ashamed because they had hoped; they came thither, and were confounded.
Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
21 For now ye are become His; ye see a terror, and are afraid.
Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
22 Did I say: 'Give unto me'? or: 'Offer a present for me of your substance'?
Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
23 or: 'Deliver me from the adversary's hand'? or: 'Redeem me from the hand of the oppressors'?
Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
24 Teach me, and I will hold my peace; and cause me to understand wherein I have erred.
Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
25 How forcible are words of uprightness! But what doth your arguing argue?
Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
26 Do ye hold words to be an argument, but the speeches of one that is desperate to be wind?
Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
27 Yea, ye would cast lots upon the fatherless, and dig a pit for your friend.
Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
28 Now therefore be pleased to look upon me; for surely I shall not lie to your face.
Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
29 Return, I pray you, let there be no injustice; yea, return again, my cause is righteous.
Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
30 Is there injustice on my tongue? Cannot my taste discern crafty devices?
Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?