< Job 40 >

1 Moreover the LORD answered Job, and said:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Shall he that reproveth contend with the Almighty? He that argueth with God, let him answer it.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Then Job answered the LORD, and said:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Behold, I am of small account; what shall I answer Thee? I lay my hand upon my mouth.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Once have I spoken, but I will not answer again; yea, twice, but I will proceed no further.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Then the LORD answered Job out of the whirlwind, and said:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Gird up thy loins now like a man; I will demand of thee, and declare thou unto Me.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Wilt thou even make void My judgment? Wilt thou condemn Me, that thou mayest be justified?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Or hast thou an arm like God? And canst thou thunder with a voice like Him?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Deck thyself now with majesty and excellency, and array thyself with glory and beauty.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Cast abroad the rage of thy wrath; and look upon every one that is proud, and abase him.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Look on every one that is proud, and bring him low; and tread down the wicked in their place.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Hide them in the dust together; bind their faces in the hidden place.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Then will I also confess unto thee that thine own right hand can save thee.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Behold now behemoth, which I made with thee; he eateth grass as an ox.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Lo now, his strength is in his loins, and his force is in the stays of his body.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 He straineth his tail like a cedar; the sinews of his thighs are knit together.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 His bones are as pipes of brass; his gristles are like bars of iron.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 He is the beginning of the ways of God; He only that made him can make His sword to approach unto him.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Surely the mountains bring him forth food, and all the beasts of the field play there.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 He lieth under the lotus-trees, in the covert of the reed, and fens.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 The lotus-trees cover him with their shadow; the willows of the brook compass him about.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Behold, if a river overflow, he trembleth not; he is confident, though the Jordan rush forth to his mouth.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Shall any take him by his eyes, or pierce through his nose with a snare?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >