< Job 13 >

1 Lo, mine eye hath seen all this, mine ear hath heard and understood it.
“Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
2 What ye know, do I know also; I am not inferior unto you.
Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
3 Notwithstanding I would speak to the Almighty, and I desire to reason with God.
Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
4 But ye are plasterers of lies, ye are all physicians of no value.
Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
5 Oh that ye would altogether hold your peace! and it would be your wisdom.
Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
6 Hear now my reasoning, and hearken to the pleadings of my lips.
Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
7 Will ye speak unrighteously for God, and talk deceitfully for Him?
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8 Will ye show Him favour? Will ye contend for God?
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9 Would it be good that He should search you out? Or as one mocketh a man, will ye mock Him?
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10 He will surely reprove you, if ye do secretly show favour.
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11 Shall not His majesty terrify you, and His dread fall upon you?
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
12 Your memorials shall be like unto ashes, your eminences to eminences of clay.
Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
13 Hold your peace, let me alone, that I may speak, and let come on me what will.
“Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
14 Wherefore? I will take my flesh in my teeth, and put my life in my hand.
Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
15 Though He slay me, yet will I trust in Him; but I will argue my ways before Him.
Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
16 This also shall be my salvation, that a hypocrite cannot come before Him.
Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
17 Hear diligently my speech, and let my declaration be in your ears.
Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
18 Behold now, I have ordered my cause; I know that I shall be justified.
Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
19 Who is he that will contend with me? For then would I hold my peace and die.
Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
20 Only do not two things unto me, then will I not hide myself from Thee:
“Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
21 Withdraw Thy hand far from me; and let not Thy terror make me afraid.
Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
22 Then call Thou, and I will answer; or let me speak, and answer Thou me.
Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
23 How many are mine iniquities and sins? Make me to know my transgression and my sin.
Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
24 Wherefore hidest Thou Thy face, and holdest me for Thine enemy?
Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
25 Wilt Thou harass a driven leaf? And wilt Thou pursue the dry stubble?
Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
26 That Thou shouldest write bitter things against me, and make me to inherit the iniquities of my youth.
Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
27 Thou puttest my feet also in the stocks, and lookest narrowly unto all my paths; Thou drawest Thee a line about the soles of my feet;
Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
28 Though I am like a wine-skin that consumeth, like a garment that is moth-eaten.
“Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.

< Job 13 >