< Jeremiah 49 >
1 Of the children of Ammon. Thus saith the LORD: Hath Israel no sons? Hath he no heir? Why then doth Malcam take possession of Gad, and his people dwell in the cities thereof?
Juu ya watu wa Amoni, Yahwe asema hivi, “Je Israeli hana watoto? Je hakuna mtu wa kurithi chochote katika Israeli? Kwa nini Moleki aikalie Gadi, na watu wake kukaa katika miji yake?
2 Therefore, behold, the days come, saith the LORD, that I will cause an alarm of war to be heard against Rabbah of the children of Ammon; and it shall become a desolate mound, and her daughters shall be burned with fire; then shall Israel dispossess them that did dispossess him, saith the LORD.
Hivyo angalia, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapo sikizisha ishara ya vita juu ya Raba miongoni mwa watu wa Amoni, hivyo itakuwa rundo lililoachwa na binti zake watawasha moto. Maana Israeli atawamiliki wanaommiliki,” asema Yahwe.
3 Wail, O Heshbon, for Ai is undone; cry, ye daughters of Rabbah, gird you with sackcloth; lament, and run to and fro among the folds; for Malcam shall go into captivity, his priests and his princes together.
Piga kelele kwa maombolezo, Heshboni, maana Ai utaangamizwa! Piga kelele, Binti za Raba! Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na kukimbia kwa kuchanganyikiwa, maana Moleki anakwenda matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
4 Wherefore gloriest thou in the valleys, thy flowing valley, O backsliding daughter? that didst trust in thy treasures: 'Who shall come unto me?'
Kwa nini mnajivunia nguvu zenu? Nguvu zenu zitakwisha, binti wasioamini, ninyi mnaotumaini utajiri wenu. Mwasema, “Nani atakayekuja kinyume changu?'
5 Behold, I will bring a terror upon thee, saith the Lord GOD of hosts, from all that are round about thee; and ye shall be driven out every man right forth, and there shall be none to gather up him that wandereth.
Tazama, nitaleta kitisho juu yenu - hili ni tamko la Yahwe, Bwana wa majeshi - kitisho hiki kitatoka kwao wote wanaowazunguka. Kila mmoja wenu atatawanyika mbele yake. Hakutakuwa na wa kuwakusanya wanaotawanyika.
6 But afterward I will bring back the captivity of the children of Ammon, saith the LORD.
Lakini baada ya haya nitarejesha mema ya watu wa Amoni - hili ni tamko la Yahwe.”
7 Of Edom. Thus saith the LORD of hosts: Is wisdom no more in Teman? Is counsel perished from the prudent? Is their wisdom vanished?
Juu ya Edomu, Yahwe wa majeshi asema hivi, Je hakuna tena hekima katika Temani? Je ushauri mwema umepotea kutoka kwa wenye ufahamu? Je hekima yao imeharibika?
8 Flee ye, turn back, dwell deep, O inhabitants of Dedan; For I do bring the calamity of Esau upon him, the time that I shall punish him.
Kimbieni! Rudini nyuma! Bakini katika mashimo katika ardhi, wenyeji wa Dedani. Maana naleta maafa ya Esau juu yake wakati ninaomwadhibu.
9 If grape-gatherers came to thee, would they not leave some gleaning grapes? if thieves by night, would they not destroy till they had enough?
Ikiwa wavunaji wa zabibu walikuja kwako, je wasinge acha kidogo? Ikiwa wezi walikuja usiku, je wasingeiba kiasi walichotaka?
10 But I have made Esau bare, I have uncovered his secret places, and he shall not be able to hide himself; his seed is spoiled, and his brethren, and his neighbours, and he is not.
Lakini nimempiga Esau kwa ukiwa. Nimefunua maficho yao. Hivyo hataweza kujificha mwenyewe. Watoto wake, ndugu zake, na jirani zake wameharibiwa, wamepotea.
11 Leave thy fatherless children, I will rear them, and let thy widows trust in Me.
Acha nyuma yatima wako. Nitachukua uhai wao, na wajane wako wanaweza kuniamini.”
12 For thus saith the LORD: Behold, they to whom it pertained not to drink of the cup shall assuredly drink; and art thou he that shall altogether go unpunished? thou shalt not go unpunished, but thou shalt surely drink.
Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, wasiostahili ni lazima wanywe sehemu ya kikombe. Je mnadhani mtaachwa bila kuhadhibiwa? Hapana, maana hakika mtakunywa.
13 For I have sworn by Myself, saith the LORD, that Bozrah shall become an astonishment, a reproach, a waste, and a curse; and all the cities thereof shall be perpetual wastes.
Maana nimekwisha apa kwangu mimi mwenyewe - asema Yahwe - Hiyo Bozra itakuwa hofu, aibu, magofu, na kitu cha laana. Miji yake yote itakuwa magofu daima.
14 I have heard a message from the LORD, and an ambassador is sent among the nations: 'Gather yourselves together, and come against her, and rise up to the battle.'
Nimesikia habari kutoka kwa Yahwe, na mjumbe ametumwa katika mataifa, 'Kusanyikeni na kumpiga. Jiandaeni kwa vita.'
15 For, behold, I make thee small among the nations, and despised among men.
“Maana tazama, nimekufanya kuwa mdogo kulinganisha na mataifa mengine, yenye kudharauliwa na watu.
16 Thy terribleness hath deceived thee, even the pride of thy heart, O thou that dwellest in the clefts of the rock, that holdest the height of the hill; though thou shouldest make thy nest as high as the eagle, I will bring thee down from thence, saith the LORD.
Na kwa hofu yenu, kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wakaaji wa maeneo ya mwinuko, ninyi mliomiliki vilele vya vilima ili mfanye viota vyenu kama tai. Nitawashusha kutoka huko - asema Yahwe.
17 And Edom shall become an astonishment; every one that passeth by it shall be astonished and shall hiss at all the plagues thereof.
Edomu atakuwa kitisho kwa kila aipitaye. Kila mtu atatetemeka na kutoa sauti kwa sababu ya maafa yake.
18 As in the overthrow of Sodom and Gomorrah and the neighbour cities thereof, saith the LORD, no man shall abide there, neither shall any son of man dwell therein.
Kama maangamizi ya Sodoma na Gomora na jirani zake,” asema Yahwe, “hakuna atakayeishi pale; hakuna mtu atakayekaa huko.
19 Behold, he shall come up like a lion from the thickets of the Jordan against the strong habitation; for I will suddenly make him run away from it, and whoso is chosen, him will I appoint over it; for who is like Me? and who will appoint Me a time? and who is that shepherd that will stand before Me?
Tazama, nitapanda kama simba kutoka katika misitu ya Yordani hata eneo la malisho mabichi. Maana nitaharakisha kumfanya Edomu kumkimbia, nami nitamweka mwingine atakayekuwa amechaguliwa kwa usimamizi huo. Maana ni nani aliyekama mimi, ni nani atakayeniagiza kuja? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
20 Therefore hear ye the counsel of the LORD, that He hath taken against Edom; and His purposes, that He hath purposed against the inhabitants of Teman: Surely the least of the flock shall drag them away, surely their habitation shall be appalled at them.
Hivyo sikiliza mipango ambayo Yahwe ameamua dhidi ya Edom, mipango aliyoifanya kinyume cha wakaao Temani. Bila shaka wataondolewa, hata kundi dogo kuliko yote. Nchi yao yenye malisho yao mabichi itageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
21 The earth quaketh at the noise of their fall; there is a cry, the noise whereof is heard in the Red Sea.
Kwa kishindo cha kuanguka kwao nchi hutikisika. Sauti ya milio ya kukata tamaa inasikika katika Bahari ya Shamu.
22 Behold, he shall come up and swoop down as the vulture, and spread out his wings against Bozrah; and the heart of the mighty men of Edom at that day shall be as the heart of a woman in her pangs.
Tazama, mtu fulani atapiga kama tai, na kushuka chini kwa kasi na kueneza mabawa yake juu ya Bozra. Kisha katika siku hiyo, mioyo ya askari wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika kuzaa.”
23 Of Damascus. Hamath is ashamed, and Arpad; for they have heard evil tidings, they are melted away; there is trouble in the sea; it cannot be quiet.
Juu ya Dameski: “Hamathi na Arpadi zitaaibika, maana wamesikia habari ya madhara. Wanayeyuka! Wamesumbuka kama bahari, isiyotulia.
24 Damascus is waxed feeble, she turneth herself to flee, and trembling hath seized on her; anguish and pangs have taken hold of her, as of a woman in travail.
Dameski umekuwa dhaifu sana. Unageuka kukimbia; hofu imeushika, Maangaiko na maumivu yameupata, kama uchungu wa mwanamke ajifunguaye.
25 'How is the city of praise left unrepaired, the city of my joy?'
Watu wake wanasema, “Umekuwaje mji maarufu, mji ambao nimeufurahia, kabla haujaachwa?
26 Therefore her young men shall fall in her broad places, and all the men of war shall be brought to silence in that day, saith the LORD of hosts.
Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika mitaa yake na askari wake wote watateketea siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.”
27 And I will kindle a fire in the wall of Damascus, and it shall devour the palaces of Ben-hadad.
“Maana nitawasha moto katika kuta za Dameski, nami nitazivunja ngome za Beni Hadadi.”
28 Of Kedar, and of the kingdoms of Hazor, which Nebuchadrezzar king of Babylon smote. Thus saith the LORD: Arise ye, go up against Kedar, and spoil the children of the east.
Juu ya Kedari na falme za Hazori, Yahwe amwambia hivi Nebukadneza (Basi Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa akienda kuyashambulia maeneo haya): “Inuka na uipige Kedari na kuwaharibu wale watu wa mashariki.
29 Their tents and their flocks shall they take, they shall carry away for themselves their curtains, and all their vessels, and their camels; and they shall proclaim against them a terror on every side.
Jeshi lake litachukua hema zao na makundi yao, nguzo za hema yao, na vitu vyao vyote. Watachukua ngamia wao kutoka kwa watu wa Kedari na kuwambia, 'Hofu ipo pande zote!”
30 Flee ye, flit far off, dwell deep, O ye inhabitants of Hazor, saith the LORD; for Nebuchadrezzar king of Babylon hath taken counsel against you, and hath conceived a purpose against you.
Kimbia, Tangatanga mbali! Kaa katika maandaki ardhini, mkaao Hazori - asema Yahwe - maana Nebukadneza mfalme wa Babeli amepanga mpango kinyume chenu. Kimbieni! Geukeni!
31 Arise, get you up against a nation that is at ease, that dwelleth without care, saith the LORD; that have neither gates nor bars, that dwell alone.
Simama! lishambulie taifa lililokatika amani, waishio salama,” asema Yahwe. Hawana malango wala nguzo ndani yao, na watu wake wanakaa wenyewe.
32 And their camels shall be a booty, and the multitude of their cattle a spoil; and I will scatter unto all winds them that have the corners polled; and I will bring their calamity from every side of them, saith the LORD.
Maana farasi wao watakuwa mateka, na wingi wa mali zao utakuwa mateka wa vita. Kisha nitawatawanya katika kila upepo wanaonyoa pembe za nywele zao, nami nitaleta madhara juu yao kutoka kila upande - hili ni tamko ya Yahwe.
33 And Hazor shall be a dwelling-place of jackals, a desolation for ever; no man shall abide there, neither shall any son of man dwell therein.
Hazori utakuwa makao ya mbwea, nchi isiyofaa daima. Hakuna atakayeishi huko; hakuna mwanadamu atakayekaa huko.”
34 The word of the LORD that came to Jeremiah the prophet concerning Elam in the beginning of the reign of Zedekiah king of Judah, saying:
Hili ni neno la Yahwe lililomwijia Yeremia nabii kuhusu Elamu. Ilikuwa wakati wa mwanzo wa kutawala kwake Sedekia mfalme wa Yuda, naye akasema,
35 Thus saith the LORD of hosts: Behold, I will break the bow of Elam, the chief of their might.
“Yahwe wa majeshi asema hivi: Tazama, ninakaribia kumvunja mpiga upinde wa Elamu, sehemu kuu ya nguvu zao.
36 And I will bring against Elam the four winds from the four quarters of heaven, and will scatter them toward all those winds; and there shall be no nation whither the dispersed of Elam shall not come.
Maana nitaleta pepo nne kutoka katika pande nne za mbingu, nami nitawatawanya watu wa Elamu katika pepo hizo zote. Hakuta kuwa na taifa ambalo kwalo waliotawanywa kutoka Elamu hawatakwenda.
37 And I will cause Elam to be dismayed before their enemies, and before them that seek their life; and I will bring evil upon them, even My fierce anger, saith the LORD; and I will send the sword after them, till I have consumed them;
Hivyo nitawavunjavunja Elamu mbele ya adui zao na mbele ya watafutao uhai wao. Maana nitaleta maangamizo dhidi yao, hasira ya gadhabu yangu - hili ni tamko la Yahwe - nami nitapeleka upanga nyuma yao hata nitakapowafuta wote.
38 And I will set My throne in Elam, and will destroy from thence king and princes, saith the LORD.
Kisha nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme na viongozi wao kutoka huko - asema Yahwe -
39 But it shall come to pass in the end of days, that I will bring back the captivity of Elam, saith the LORD.
na itakuwa siku zijazo kwamba nitarejesha mema ya Elamu - asema Yahwe.”