< Jeremiah 3 >
1 ...saying: If a man put away his wife, and she go from him, and become another man's, may he return unto her again? Will not that land be greatly polluted? But thou hast played the harlot with many lovers; and wouldest thou yet return to Me? saith the LORD.
“Kama mtu akimpa talaka mkewe, naye akamwacha na akaolewa na mtu mwingine, je, huyo mume aweza kumrudia tena? Je, hiyo nchi haitanajisika kabisa? Lakini umeishi kama kahaba na wapenzi wengi: je, sasa utanirudia tena?” asema Bwana.
2 Lift up thine eyes unto the high hills, and see: Where hast thou not been lain with? By the ways hast thou sat for them, as an Arabian in the wilderness; and thou hast polluted the land with thy harlotries and with thy wickedness.
“Inua macho utazame miinuko iliyo kame na uone. Je, pana mahali ambapo hawajalala nawe? Uliketi kando ya barabara ukiwasubiri wapenzi, ukakaa kama yeye ahamahamaye jangwani. Umeinajisi nchi kwa ukahaba wako na uovu wako.
3 Therefore the showers have been withheld, and there hath been no latter rain; yet thou hadst a harlot's forehead, thou refusedst to be ashamed.
Kwa hiyo mvua imezuiliwa, nazo mvua za vuli hazikunyesha. Hata hivyo, una uso usio na haya kama wa kahaba; unakataa kutahayari kwa aibu.
4 Didst thou not just now cry unto Me: 'My father, Thou art the friend of my youth.
Je, wewe hujaniita hivi punde tu: ‘Baba yangu, rafiki yangu tangu ujana wangu,
5 Will He bear grudge for ever? Will He keep it to the end?' Behold, thou hast spoken, but hast done evil things, and hast had thy way.
je, utakasirika siku zote? Je, ghadhabu yako itaendelea milele?’ Hivi ndivyo unavyozungumza, lakini unafanya maovu yote uwezayo.”
6 And the LORD said unto me in the days of Josiah the king: 'Hast thou seen that which backsliding Israel did? she went up upon every high mountain and under every leafy tree, and there played the harlot.
Wakati wa utawala wa Mfalme Yosia, Bwana aliniambia, “Umeona kile Israeli asiye mwaminifu amekifanya? Amepanda juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti uliotanda na amefanya uzinzi huko.
7 And I said: After she hath done all these things, she will return unto me; but she returned not. And her treacherous sister Judah saw it.
Mimi nilifikiri kuwa baada ya kuyafanya yote haya angelinirudia, lakini hakurudi, naye dada yake Yuda mdanganyifu aliona hili.
8 And I saw, when, forasmuch as backsliding Israel had committed adultery, I had put her away and given her a bill of divorcement, that yet treacherous Judah her sister feared not; but she also went and played the harlot;
Nilimpa Israeli asiye mwaminifu hati yake ya talaka, na kumfukuza kwa ajili ya uzinzi wake wote. Hata hivyo nikaona kuwa Yuda dada yake mdanganyifu hakuogopa. Yeye pia alitoka na kufanya uzinzi.
9 and it came to pass through the lightness of her harlotry, that the land was polluted, and she committed adultery with stones and with stocks;
Kwa sababu uasherati wa Israeli haukuwa kitu kwake, Yuda aliinajisi nchi kwa kuzini na mawe na miti.
10 and yet for all this her treacherous sister Judah hath not returned unto Me with her whole heart, but feignedly, saith the LORD —
Pamoja na hayo yote, Yuda dada yake mdanganyifu hakunirudia kwa moyo wake wote, bali kwa kujifanya tu,” asema Bwana.
11 even the LORD said unto me — backsliding Israel hath proved herself more righteous than treacherous Judah.
Bwana akaniambia, “Israeli asiye mwaminifu ana haki kuliko Yuda mdanganyifu.
12 Go, and proclaim these words toward the north, and say: Return, thou backsliding Israel, saith the LORD; I will not frown upon you; for I am merciful, saith the LORD, I will not bear grudge for ever.
Nenda, ukatangaze ujumbe huu kuelekea kaskazini: “‘Rudi, Israeli usiye mwaminifu,’ asema Bwana, ‘sitakutazama tena kwa uso uliokunjamana, kwa kuwa mimi ni mwenye huruma,’ asema Bwana, ‘Sitashika hasira yangu milele.
13 Only acknowledge thine iniquity, that thou hast transgressed against the LORD thy God, and hast scattered thy ways to the strangers under every leafy tree, and ye have not hearkened to My voice, saith the LORD.
Ungama dhambi zako tu: kwamba umemwasi Bwana Mungu wako, umetapanya wema wako kwa miungu ya kigeni chini ya kila mti unaotanda, nawe hukunitii mimi,’” asema Bwana.
14 Return, O backsliding children, saith the LORD; for I am a lord unto you, and I will take you one of a city, and two of a family, and I will bring you to Zion;
“Rudini, enyi watu msio waaminifu, kwa kuwa mimi ni mume wenu,” asema Bwana. “Nitawachagua ninyi, mmoja kutoka kwenye mji, na wawili kutoka kwenye ukoo, nami nitawaleta Sayuni.
15 and I will give you shepherds according to My heart, who shall feed you with knowledge and understanding.
Kisha nitawapeni wachungaji wanipendezao moyo wangu, ambao watawaongoza kwa maarifa na ufahamu.
16 And it shall come to pass, when ye are multiplied and increased in the land, in those days, saith the LORD, they shall say no more: The ark of the covenant of the LORD; neither shall it come to mind; neither shall they make mention of it; neither shall they miss it; neither shall it be made any more.
Katika siku hizo, idadi yenu itakapokuwa imeongezeka sana katika nchi, watu hawatasema tena, ‘Sanduku la Agano la Bwana,’” asema Bwana. “Halitaingia tena kwenye mawazo yao wala kukumbukwa, hawatalihitaji wala halitatengenezwa jingine.
17 At that time they shall call Jerusalem The throne of the LORD; and all the nations shall be gathered unto it, to the name of the LORD, to Jerusalem; neither shall they walk any more after the stubbornness of their evil heart.
Wakati huo, wataita Yerusalemu kuwa Kiti cha Enzi cha Bwana, nayo mataifa yote watakusanyika Yerusalemu kuliheshimu jina la Bwana. Hawatafuata tena ukaidi wa mioyo yao miovu.
18 In those days the house of Judah shall walk with the house of Israel, and they shall come together out of the land of the north to the land that I have given for an inheritance unto your fathers.'
Katika siku hizo, nyumba ya Yuda itaungana na nyumba ya Israeli, wao kwa pamoja watakuja kutoka nchi ya kaskazini hadi nchi niliyowapa baba zenu kama urithi.
19 But I said: 'How would I put thee among the sons, and give thee a pleasant land, the goodliest heritage of the nations!' And I said: 'Thou shalt call Me, My father; and shalt not turn away from following Me.'
“Mimi mwenyewe nilisema, “‘Tazama jinsi nitakavyowatunza kwa furaha kama wana na kuwapa nchi nzuri, urithi ulio mzuri kuliko wa taifa jingine lolote.’ Nilidhani mngeniita ‘Baba,’ na msingegeuka, mkaacha kunifuata.
20 Surely as a wife treacherously departeth from her husband, so have ye dealt treacherously with Me, O house of Israel, saith the LORD.
Lakini kama mwanamke asiye mwaminifu kwa mumewe, vivyo hivyo mmekosa uaminifu kwangu pia, ee nyumba ya Israeli,” asema Bwana.
21 Hark! upon the high hills is heard the suppliant weeping of the children of Israel; for that they have perverted their way, they have forgotten the LORD their God.
Kilio kinasikika juu ya miinuko iliyo kame, kulia na kuomboleza kwa watu wa Israeli, kwa sababu wamepotoka katika njia zao na wamemsahau Bwana Mungu wao.
22 Return, ye backsliding children, I will heal your backslidings. — 'Here we are, we are come unto Thee; for Thou art the LORD our God.
“Rudini, enyi watu msio waaminifu, nami nitawaponya ukengeufu wenu.” “Naam, tutakuja kwako, kwa maana wewe ni Bwana Mungu wetu.
23 Truly vain have proved the hills, the uproar on the mountains; truly in the LORD our God is the salvation of Israel.
Hakika zile ghasia za kuabudu sanamu kwenye vilima na milimani ni udanganyifu; hakika katika Bwana, Mungu wetu, uko wokovu wa Israeli.
24 But the shameful thing hath devoured the labour of our fathers from our youth; their flocks and their herds, their sons and their daughters.
Tangu ujana wetu miungu ya aibu imeyala matunda ya kazi za baba zetu: makundi yao ya kondoo na ngʼombe, wana wao na binti zao.
25 Let us lie down in our shame, and let our confusion cover us; for we have sinned against the LORD our God, we and our fathers, from our youth even unto this day; and we have not hearkened to the voice of the LORD our God.'
Sisi na tulale chini katika aibu yetu, na fedheha yetu itufunike. Tumetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wetu, sisi na mababa zetu; tangu ujana wetu hadi leo hatukumtii Bwana Mungu wetu.”