< Jeremiah 11 >
1 The word that came to Jeremiah from the LORD, saying:
Hili ndilo neno lililojia Yeremia kutoka kwa Bwana, akasema,
2 'Hear ye the words of this covenant, and speak unto the men of Judah, and to the inhabitants of Jerusalem;
“Sikiliza maneno ya agano hili, uwaambie kila mtu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu.
3 and say thou unto them: Thus saith the LORD, the God of Israel: Cursed be the man that heareth not the words of this covenant,
Uwaambie, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: na alaaniwe yeyote asiyesikiliza maneno ya agano hili.
4 which I commanded your fathers in the day that I brought them forth out of the land of Egypt, out of the iron furnace, saying: Hearken to My voice, and do them, according to all which I command you; so shall ye be My people, and I will be your God;
Hili ndilo agano nililowaamuru baba zenu walishike siku nilipowatoa kutoka katika nchi ya Misri, kutoka tanuru ya chuma. Nikawaambia, “Sikilizeni sauti yangu na mfanye mambo yote kama nilivyowaamuru, kwa kuwa mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.”
5 that I may establish the oath which I swore unto your fathers, to give them a land flowing with milk and honey, as at this day.' Then answered I, and said: 'Amen, O LORD.'
Nisikilizeni ili nipate kukitimiza kiapo nilichoapa kwa baba zenu, kiapo kwamba nitawapa nchi iliyojaa maziwa na asali kama ilivyo leo.'” Kisha mimi Yeremia nikajibu na kusema, “Ndio, Bwana!”
6 And the LORD said unto me: 'Proclaim all these words in the cities of Judah, and in the streets of Jerusalem, saying: Hear ye the words of this covenant, and do them.
Bwana akaniambia, “Hubiri habari hizi yote katika miji ya Yuda, na katika njia za Yerusalemu. Sema, “Sikilizeni maneno ya agano hili na mkayafanye.
7 For I earnestly forewarned your fathers in the day that I brought them up out of the land of Egypt, even unto this day, forewarning betimes and often, saying: Hearken to My voice.
Kwa maana nimewaagiza wazee wenu tangu siku ile niliyowaleta kutoka nchi ya Misri hadi wakati huu wa sasa, nimewaonya mara kwa mara na kusema, “Sikilizeni sauti yangu.'”
8 Yet they hearkened not, nor inclined their ear, but walked every one in the stubbornness of their evil heart; therefore I brought upon them all the words of this covenant, which I commanded them to do, but they did them not.'
Lakini hawakusikiliza au wala kutega masikio yao. Kila mtu amekuwa akitembea katika ukaidi wa moyo wake mbaya. Kwa hiyo nilileta laana zote katika agano hili nililoamuru kuja juu yao. Lakini watu bado hawakuitii.”
9 And the LORD said unto me: 'A conspiracy is found among the men of Judah, and among the inhabitants of Jerusalem.
Kisha Bwana akaniambia, “Njama imeonekana kati ya watu wa Yuda na wenyeji wa Yerusalemu.
10 They are turned back to the iniquities of their forefathers, who refused to hear My words; and they are gone after other gods to serve them; the house of Israel and the house of Judah have broken My covenant which I made with their fathers.
Wameugeukia uovu wa mababu zao wa mwanzo, ambao walikataa kusikiliza neno langu, ambao badala yake walifuata miungu mingine ili kuabudu. Waisraeli na nyumba ya Yuda walivunja agano langu nililoweka na baba zao.
11 Therefore thus saith the LORD: Behold, I will bring evil upon them, which they shall not be able to escape; and though they shall cry unto Me, I will not hearken unto them.
Kwa hiyo Bwana asema hivi, 'Tazameni, nitawaletea majanga juu yao, majanga ambayo hawataweza kuyaepuka. Ndipo wataniita, lakini sitawasikiliza.
12 Then shall the cities of Judah and the inhabitants of Jerusalem go and cry unto the gods unto whom they offer; but they shall not save them at all in the time of their trouble.
Miji ya Yuda na wenyeji wa Yerusalemu watakwenda na kuiita miungu ambayo walitoa sadaka, lakini hakika hawatawaokoa wakati wa majanga yao.
13 For according to the number of thy cities are thy gods, O Judah; and according to the number of the streets of Jerusalem have ye set up altars to the shameful thing, even altars to offer unto Baal.
Kwa kuwa idadi ya miungu yako ewe Yuda imeongezeka sawa na idadi ya miji yako. Na umefanya idadi ya madhabahu ya aibu huko Yerusalemu, madhabahu ya kufukiza uvumba kwa Baali, sawa na idadi ya njia zake.
14 Therefore pray not thou for this people, neither lift up cry nor prayer for them; for I will not hear them in the time that they cry unto Me for their trouble.'
Kwa hiyo wewe mwenyewe, Yeremia, usiwaombee watu hawa. Lazima usiomboleze au kuomba kwa niaba yao. Kwa maana siwezi kusikiliza wakati wananiita katika majanga yao.
15 What hath My beloved to do in My house, seeing she hath wrought lewdness with many, and the hallowed flesh is passed from thee? When thou doest evil, then thou rejoicest.
Mpendwa wangu anafanya nini nyumbani kwangu, ikiwa amekuwa na nia mbaya? Nyama za sadaka yako hazitakusaidia. Unafurahi kwa sababu ya matendo yako mabaya.
16 The LORD called thy name a leafy olive-tree, fair with goodly fruit; with the noise of a great tumult He hath kindled fire upon it, and the branches of it are broken.
Katika siku za nyuma Bwana alikuita mti wa mzeituni wenye majani, mzuri wenye matunda mazuri. Lakini atawasha moto juu yake ambayo itaonekana kama sauti ya dhoruba; matawi yake yatavunjika.
17 For the LORD of hosts, that planted thee, hath pronounced evil against thee, because of the evil of the house of Israel and of the house of Judah, which they have wrought for themselves in provoking Me by offering unto Baal.
Kwa maana Bwana wa majeshi, aliyekua amekusudia maafa juu yako, kwa sababu ya matendo mabaya ambayo nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda wamefanya-wamenikasirisha kwa kumtolea Baali sadaka.'”
18 And the LORD gave me knowledge of it, and I knew it; then Thou showedst me their doings.
Bwana alinijulisha mambo haya, kwa hiyo nakayajua. Wewe, Bwana, umenifanya nione matendo yao.
19 But I was like a docile lamb that is led to the slaughter; and I knew not that they had devised devices against me: 'Let us destroy the tree with the fruit thereof, and let us cut him off from the land of the living, that his name may be no more remembered.'
Nilikuwa kama kondoo mpole unayeongozwa na mchinjaji. Sikujua kwamba walikuwa wameunda mipango dhidi yangu, “Hebu tuangamize mti na matunda yake! Hebu tumkatilie mbali na nchi ya walio hai ili jina lake lisikumbukwe tena.
20 But, O LORD of hosts, that judgest righteously, that triest the reins and the heart, let me see Thy vengeance on them; for unto Thee have I revealed my cause.
Lakini Bwana wa majeshi ndiye mwamuzi mwenye haki ambaye huchunguza moyo na akili. Mimi nitashuhudia kisasi chako dhidi yao, kwa kuwa nimekuletea kesi yangu kwako.
21 Therefore thus saith the LORD concerning the men of Anathoth, that seek thy life, saying: 'Thou shalt not prophesy in the name of the LORD, that thou die not by our hand';
Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya watu wa Anathothi, wanaotafuta uhai wako, “wanasema, 'Usifanye unabii kwa jina la Bwana, usije utakufa kwa mkono wetu.'
22 therefore thus saith the LORD of hosts: Behold, I will punish them; the young men shall die by the sword, their sons and their daughters shall die by famine;
Kwa hiyo Bwana wa majeshi asema hivi, 'Tazameni, nitawaadhibu. Vijana wao wenye nguvu watakufa kwa upanga. Wana wao na binti zao watakufa kwa njaa.
23 And there shall be no remnant unto them; for I will bring evil upon the men of Anathoth, even the year of their visitation.
Hakuna hata mmoja atakayeachwa, kwa maana nitaleta maafa dhidi ya watu wa Anathothi, mwaka wa adhabu yao.'”