< Isaiah 63 >
1 'Who is this that cometh from Edom, with crimsoned garments from Bozrah? This that is glorious in his apparel, stately in the greatness of his strength?' — 'I that speak in victory, mighty to save.' —
Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
2 'Wherefore is Thine apparel red, and Thy garments like his that treadeth in the winevat?' —
Kwa nini mavazi yako ni mekundu, kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?
3 'I have trodden the winepress alone, and of the peoples there was no man with Me; yea, I trod them in Mine anger, and trampled them in My fury; and their lifeblood is dashed against My garments, and I have stained all My raiment.
“Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu; kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami. Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu; damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu, na kutia madoa nguo zangu zote.
4 For the day of vengeance that was in My heart, and My year of redemption are come.
Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu, mwaka wa ukombozi wangu umefika.
5 And I looked, and there was none to help, and I beheld in astonishment, and there was none to uphold; therefore Mine own arm brought salvation unto Me, and My fury, it upheld Me.
Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia, nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada; hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu, na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.
6 And I trod down the peoples in Mine anger, and made them drunk with My fury, and I poured out their lifeblood on the earth.'
Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu, katika ghadhabu yangu niliwalewesha, na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”
7 I will make mention of the mercies of the LORD, and the praises of the LORD, according to all that the LORD hath bestowed on us; and the great goodness toward the house of Israel, which He hath bestowed on them according to His compassions, and according to the multitude of His mercies.
Nitasimulia juu ya wema wa Bwana, kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa, sawasawa na yote ambayo Bwana ametenda kwa ajili yetu: naam, mambo mengi mema aliyoyatenda kwa ajili ya nyumba ya Israeli, sawasawa na huruma zake na wema wake mwingi.
8 For He said: 'Surely, they are My people, children that will not deal falsely'; so He was their Saviour.
Alisema, “Hakika wao ni watu wangu, wana ambao hawatanidanganya”; hivyo akawa Mwokozi wao.
9 In all their affliction He was afflicted, and the angel of His presence saved them; in His love and in His pity He redeemed them; and He bore them, and carried them all the days of old.
Katika taabu zao zote naye alitaabika, na malaika wa uso wake akawaokoa. Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa, akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.
10 But they rebelled, and grieved His holy spirit; therefore He was turned to be their enemy, Himself fought against them.
Lakini waliasi, na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake. Hivyo aligeuka na kuwa adui yao, na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.
11 Then His people remembered the days of old, the days of Moses: 'Where is He that brought them up out of the sea with the shepherds of His flock? Where is He that put His holy spirit in the midst of them?
Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita, siku za Mose na watu wake: yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari, pamoja na wachungaji wa kundi lake? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mtakatifu katikati yao,
12 That caused His glorious arm to go at the right hand of Moses? That divided the water before them, to make Himself an everlasting name?
aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu kuwa katika mkono wa kuume wa Mose, aliyegawa maji ya bahari mbele yao, ili kujipatia jina milele,
13 That led them through the deep, as a horse in the wilderness, without stumbling?
aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi? Kama farasi katika nchi iliyo wazi, wao hawakujikwaa,
14 As the cattle that go down into the valley, the spirit of the LORD caused them to rest; so didst Thou lead Thy people, to make Thyself a glorious name.'
kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho, walipewa pumziko na Roho wa Bwana. Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.
15 Look down from heaven, and see, even from Thy holy and glorious habitation; Where is Thy zeal and Thy mighty acts, the yearning of Thy heart and Thy compassions, now restrained toward me?
Tazama chini kutoka mbinguni ukaone kutoka kiti chako cha enzi kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu. Uko wapi wivu wako na uweza wako? Umetuzuilia wema wako na huruma zako.
16 For Thou art our Father; for Abraham knoweth us not, and Israel doth not acknowledge us; Thou, O LORD, art our Father, our Redeemer from everlasting is Thy name.
Lakini wewe ni Baba yetu, ingawa Abrahamu hatufahamu sisi wala Israeli hatutambui; wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu, Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.
17 O LORD, why dost Thou make us to err from Thy ways, and hardenest our heart from Thy fear? Return for Thy servants' sake, the tribes of Thine inheritance.
Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako, na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu? Rudi kwa ajili ya watumishi wako, yale makabila ambayo ni urithi wako.
18 Thy holy people they have well nigh driven out, our adversaries have trodden down Thy sanctuary.
Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu, lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.
19 We are become as they over whom Thou never borest rule, as they that were not called by Thy name.
Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.