< Hosea 10 >
1 Israel was a luxuriant vine, which put forth fruit freely: as his fruit increased, he increased his altars; the more goodly his land was, the more goodly were his pillars.
Israeli ni mzabibu mzuri ambao huzaa matunda yake. kwa kadiri matunda yake yanavyoongezeka vivyo hivyo anajenga madhabahu nyingi. Kwa kuwa nchi yake ilizalishwa zaidi, aliboresha nguzo zake.
2 Their heart is divided; now shall they bear their guilt; He will break down their altars, He will spoil their pillars.
Moyo wao ni udanganyifu; sasa wanapaswa kubeba hatia yao. Bwana ataharibu madhabahu zao; ataharibu nguzo zao.
3 Surely now shall they say: 'We have no king; for we feared not the LORD; and the king, what can he do for us?'
Kwa maana watasema, “Hatuna mfalme, kwa maana hatukumcha Bwana. Na mfalme-angeweza kutufanyia nini?”
4 They speak words, they swear falsely, they make covenants; thus judgment springeth up as hemlock in the furrows of the field.
Wanasema maneno tupu na kufanya maagano kwa kuapa uongo. Kwa hivyo haki inakuja kama magugu yenye sumu katika mito ya shamba.
5 The inhabitants of Samaria shall be in dread for the calves of Beth-aven; for the people thereof shall mourn over it, and the priests thereof shall tremble for it, for its glory, because it is departed from it.
Wakazi wa Samaria wataogopa kwa sababu ya ndama za Beth Aveni. Watu wake waliomboleza juu yao, kama walivyofanya wale makuhani wa sanamu ambao walikuwa wamefurahi juu yao na utukufu wao, lakini hawako tena.
6 It also shall be carried unto Assyria, for a present to King Contentious; Ephraim shall receive shame, and Israel shall be ashamed of his own counsel.
Wao watachukuliwa kwenda Ashuru kama sadaka kwa mfalme mkuu. Efraimu atakuwa na aibu, na Israeli atakuwa na aibu kwa sanamu yake.
7 As for Samaria, her king is cut off, as foam upon the water.
Mfalme wa Samaria ataangamizwa, kama chipu cha kuni juu ya uso wa maji.
8 The high places also of Aven shall be destroyed, even the sin of Israel. The thorn and the thistle shall come up on their altars; and they shall say to the mountains: 'Cover us', and to the hills: 'Fall on us.'
Sehemu za juu za uovu zitaharibiwa. Hii ndiyo dhambi ya Israeli! Miti na vichaka vitakua juu ya madhabahu zao. Watu wataiambia milima, “Tufunike sisi!” na kwa vilima, “Tuangukieni!”
9 From the days of Gibeah thou hast sinned, O Israel; there they stood; no battle was to overtake them in Gibeah, nor the children of arrogancy.
Ee Israeli, umetenda dhambi tangu siku za Gibea; huko umebaki. Je, vita vitawapata wana wa uovu huko Gibea?
10 When it is My desire, I will chastise them; and the peoples shall be gathered against them, when they are yoked to their two rings.
Nitakapotaka, nitawaadhibu. Mataifa wataungana pamoja nao na kuwaweka katika vifungo kwa uovu wao mara mbili.
11 And Ephraim is a heifer well broken, that loveth to thresh, and I have passed over upon her fair neck; I will make Ephraim to ride, Judah shall plow, Jacob shall break his clods.
Efraimu ni ndama mwenye mafunzo ambayo anapenda kupura nafaka, hivyo nitaweka jozi juu ya shingo yake nzuri. Efraimu nitauweka jozi; Yuda ataimea; Yakobo atauvuta pigo kwa nafsi yake.
12 Sow to yourselves according to righteousness, reap according to mercy, break up your fallow ground; for it is time to seek the LORD, till He come and cause righteousness to rain upon you.
Jifanyieni haki, vuneni matunda ya uaminifu wa agano. Chimbueni ardhi yenu isiyopandwa, kwa maana ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuinua haki juu yenu.
13 Ye have plowed wickedness, ye have reaped iniquity, ye have eaten the fruit of lies; for thou didst trust in thy way, in the multitude of thy mighty men.
Mmelima uovu; mmevuna udhalimu. Mmekula matunda ya udanganyifu kwa sababu uliamini katika mipango yako na katika askari wako wengi.
14 Therefore shall a tumult arise among thy hosts, and all thy fortresses shall be spoiled, as Shalman spoiled Beth-arbel in the day of battle; the mother was dashed in pieces with her children.
Kwa hiyo mlipuko wa vita utafufuka kati ya watu wako, na miji yako yote yenye ngome itaharibiwa. Itakuwa kama Shalmani aliharibu Beth Arbeli siku ya vita, wakati mama alivunjika vipande vipande na watoto wake.
15 So hath Beth-el done unto you because of your great wickedness; at daybreak is the king of Israel utterly cut off.
Kwa hiyo itakuwa kwako, Betheli, kwa sababu ya uovu wako mkubwa. Wakati wa mchana mfalme wa Israeli atakatwa kabisa.