< Genesis 19 >

1 And the two angels came to Sodom at even; and Lot sat in the gate of Sodom; and Lot saw them, and rose up to meet them; and he fell down on his face to the earth;
Malaika wale wawili wakafika Sodoma wakati wa jioni, naye Loti alikuwa ameketi kwenye lango la mji. Wakati alipowaona, aliondoka kwenda kuwalaki na kuwasujudia hadi chini.
2 and he said: 'Behold now, my lords, turn aside, I pray you, into your servant's house, and tarry all night, and wash your feet, and ye shall rise up early, and go on your way.' And they said: 'Nay; but we will abide in the broad place all night.'
Akasema, “Bwana zangu, tafadhali karibuni kwenye nyumba ya mtumishi wenu. Mnaweza kunawa miguu na kulala hapa kisha asubuhi na mapema mwendelee na safari yenu.” Wakamjibu, “La hasha, tutalala hapa nje uwanjani.”
3 And he urged them greatly; and they turned in unto him, and entered into his house; and he made them a feast, and did bake unleavened bread, and they did eat.
Lakini akasisitiza kwa nguvu kwamba waingie pamoja naye nyumbani kwake. Akawaandalia chakula, mikate isiyotiwa chachu, nao wakala.
4 But before they lay down, the men of the city, even the men of Sodom, compassed the house round, both young and old, all the people from every quarter.
Kabla hawajaenda kulala, watu wote kutoka kila sehemu ya mji wa Sodoma, vijana kwa wazee, waliizunguka nyumba.
5 And they called unto Lot, and said unto him: 'Where are the men that came in to thee this night? bring them out unto us, that we may know them.'
Wakamwita Loti wakisema, “Wako wapi wale watu ambao walikuja kwako jioni hii? Watoe nje kwetu ili tuweze kuwalawiti.”
6 And Lot went out unto them to the door, and shut the door after him.
Loti akatoka nje kuonana nao, akaufunga mlango nyuma yake,
7 And he said: 'I pray you, my brethren, do not so wickedly.
akasema, “La hasha, rafiki zangu. Msifanye jambo hili ovu.
8 Behold now, I have two daughters that have not known man; let me, I pray you, bring them out unto you, and do ye to them as is good in your eyes; only unto these men do nothing; forasmuch as they are come under the shadow of my roof.'
Tazama, ninao binti wawili ambao kamwe hawajakutana kimwili na mwanaume. Acha niwatoe nje kwenu, nanyi mnaweza kuwafanyia lolote mnalotaka. Lakini msiwafanyie chochote watu hawa, kwa sababu wako kwenye ulinzi chini ya dari langu.”
9 And they said: 'Stand back.' And they said: 'This one fellow came in to sojourn, and he will needs play the judge; now will we deal worse with thee, than with them.' And they pressed sore upon the man, even Lot, and drew near to break the door.
Wakamjibu, “Tuondokee mbali.” Wakaendelea kusema, “Huyu mtu alikuja hapa kama mgeni na sasa anataka kuwa mwamuzi wetu! Tutakutenda vibaya kuliko wao.” Waliendelea kumlazimisha Loti na kusonga mbele ili kuvunja mlango.
10 But the men put forth their hand, and brought Lot into the house to them, and the door they shut.
Lakini watu wale waliokuwa ndani wakanyoosha mkono wakamvuta Loti ndani ya nyumba na kufunga mlango.
11 And they smote the men that were at the door of the house with blindness, both small and great; so that they wearied themselves to find the door.
Kisha wakawapiga kwa upofu wale watu waliokuwa mlangoni mwa ile nyumba, vijana kwa wazee, hivyo hawakuweza kuupata mlango.
12 And the men said unto Lot: 'Hast thou here any besides? son-in-law, and thy sons, and thy daughters, and whomsoever thou hast in the city; bring them out of the place;
Wale watu wawili wakamwambia Loti, “Una mtu mwingine yeyote hapa, wakwe zako, wana au binti, ama yeyote mwingine aliye wako katika mji huu? Waondoe hapa,
13 for we will destroy this place, because the cry of them is waxed great before the LORD; and the LORD hath sent us to destroy it.'
kwa sababu tunapaangamiza mahali hapa. Kilio kwa Bwana dhidi ya watu wa hapa ni kikubwa kiasi kwamba ametutuma kupaangamiza.”
14 And Lot went out, and spoke unto his sons-in-law, who married his daughters, and said: 'Up, get you out of this place; for the LORD will destroy the city.' But he seemed unto his sons-in-law as one that jested.
Kwa hiyo Loti alitoka ili kuzungumza na wakwe zake, waliokuwa wamewaposa binti zake. Akawaambia, “Fanyeni haraka kuondoka mahali hapa, kwa kuwa Bwana yu karibu kuangamiza mji huu!” Lakini wakwe zake walifikiri kwamba alikuwa akitania.
15 And when the morning arose, then the angels hastened Lot, saying: 'Arise, take thy wife, and thy two daughters that are here; lest thou be swept away in the iniquity of the city.'
Kunako mapambazuko, malaika wakamhimiza Loti, wakamwambia, “Fanya haraka! Mchukue mke wako na binti zako wawili walioko hapa, la sivyo utaangamizwa wakati mji utakapoadhibiwa.”
16 But he lingered; and the men laid hold upon his hand, and upon the hand of his wife, and upon the hand of his two daughters; the LORD being merciful unto him. And they brought him forth, and set him without the city.
Alipositasita, wale watu wakamshika mkono wake na mikono ya mke wake na binti zake wawili na kuwaongoza salama nje ya mji, kwa kuwa Bwana alikuwa na huruma kwao.
17 And it came to pass, when they had brought them forth abroad, that he said: 'Escape for thy life; look not behind thee, neither stay thou in all the Plain; escape to the mountain, lest thou be swept away.'
Mara walipokwisha kuwatoa nje, mmoja wao akawaambia, “Mkimbie kwa usalama wenu! Msitazame nyuma, wala msisimame popote katika nchi tambarare! Kimbilieni milimani, ama sivyo mtaangamizwa!”
18 And Lot said unto them: 'Oh, not so, my lord;
Lakini Loti akawajibu, “La hasha, bwana zangu, tafadhalini!
19 behold now, thy servant hath found grace in thy sight, and thou hast magnified thy mercy, which thou hast shown unto me in saving my life; and I cannot escape to the mountain, lest the evil overtake me, and I die.
Mtumishi wenu amepata kibali mbele ya macho yenu, nanyi mmeonyesha wema mkubwa kwangu kwa kuokoa maisha yangu. Lakini siwezi kukimbilia milimani, janga hili litanikumba, nami nitakufa.
20 Behold now, this city is near to flee unto, and it is a little one; oh, let me escape thither — is it not a little one? — and my soul shall live.'
Tazama, hapa kuna mji karibu wa kukimbilia, nao ni mdogo. Niruhusuni nikimbilie humo, ni mdogo sana, ama sivyo? Ndipo maisha yangu yatasalimika.”
21 And he said unto him: 'See, I have accepted thee concerning this thing also, that I will not overthrow the city of which thou hast spoken.
Akamwambia, “Vema sana, nitalikubali hili ombi pia, sitauangamiza mji ulioutaja.
22 Hasten thou, escape thither; for I cannot do any thing till thou be come thither.' — Therefore the name of the city was called Zoar. —
Lakini ukimbilie huko haraka, kwa sababu sitaweza kufanya lolote mpaka ufike huko.” (Ndiyo maana mji huo ukaitwa Soari.)
23 The sun was risen upon the earth when Lot came unto Zoar.
Wakati Loti alipofika Soari, jua lilikuwa limechomoza katika nchi.
24 Then the LORD caused to rain upon Sodom and upon Gomorrah brimstone and fire from the LORD out of heaven;
Ndipo Bwana akanyesha moto wa kiberiti uliotoka mbinguni kwa Bwana juu ya Sodoma na Gomora.
25 and He overthrow those cities, and all the Plain, and all the inhabitants of the cities, and that which grew upon the ground.
Hivyo akaiteketeza miji ile na eneo lote la tambarare, pamoja na wote waliokuwa wanaishi katika miji, hata pia mimea yote katika nchi.
26 But his wife looked back from behind him, and she became a pillar of salt.
Lakini mke wa Loti akatazama nyuma, hivyo akawa nguzo ya chumvi.
27 And Abraham got up early in the morning to the place where he had stood before the LORD.
Asubuhi na mapema siku iliyofuata, Abrahamu akaamka na kurudi mahali pale aliposimama mbele za Bwana.
28 And he looked out toward Sodom and Gomorrah, and toward all the land of the Plain, and beheld, and, lo, the smoke of the land went up as the smoke of a furnace.
Akatazama upande wa Sodoma na Gomora, kuelekea nchi yote ya tambarare, akaona moshi mzito ukipanda kutoka kwenye nchi, kama moshi utokao kwenye tanuru.
29 And it came to pass, when God destroyed the cities of the Plain, that God remembered Abraham, and sent Lot out of the midst of the overthrow, when He overthrew the cities in which Lot dwelt.
Kwa hiyo Mungu alipoiangamiza miji ya tambarare alimkumbuka Abrahamu, akamtoa Loti kutoka kwenye lile janga lililoharibu miji ile ambamo Loti alikuwa ameishi.
30 And Lot went up out of Zoar, and dwelt in the mountain, and his two daughters with him; for he feared to dwell in Zoar; and he dwelt in a cave, he and his two daughters.
Loti na binti zake wawili waliondoka Soari na kufanya makao yao kule milimani, kwa maana aliogopa kukaa Soari. Yeye na binti zake wawili waliishi katika pango.
31 And the first-born said unto the younger: 'Our father is old, and there is not a man in the earth to come in unto us after the manner of all the earth.
Siku moja binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee na hakuna mwanaume mahali hapa atakayekutana na sisi kimwili, kama ilivyo desturi ya mahali pote duniani.
32 Come, let us make our father drink wine, and we will lie with him, that we may preserve seed of our father.'
Tumnyweshe baba yetu mvinyo kisha tukutane naye kimwili ili tuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
33 And they made their father drink wine that night. And the first-born went in, and lay with her father; and he knew not when she lay down, nor when she arose.
Usiku ule walimnywesha baba yao mvinyo, alipolewa binti yake mkubwa akaingia na kukutana naye kimwili. Baba yao hakujua wakati binti yake alipoingia kulala naye wala alipotoka.
34 And it came to pass on the morrow, that the first-born said unto the younger: 'Behold, I lay yesternight with my father. Let us make him drink wine this night also; and go thou in, and lie with him, that we may preserve seed of our father.'
Siku iliyofuata binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Usiku uliopita mimi nilikutana kimwili na baba yangu. Tumnyweshe divai tena, usiku huu nawe ukutane naye kimwili ili tuweze kuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
35 And they made their father drink wine that night also. And the younger arose, and lay with him; and he knew not when she lay down, nor when she arose.
Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo tena usiku ule, naye binti yake mdogo akaingia, akakutana naye kimwili. Kwa mara nyingine baba yao hakujua binti yake alipolala naye wala alipoondoka.
36 Thus were both the daughters of Lot with child by their father.
Hivyo binti wawili wa Loti wakapata mimba kwa baba yao.
37 And the first-born bore a son, and called his name Moab — the same is the father of the Moabites unto this day.
Binti mkubwa akamzaa mwana, akamwita jina lake Moabu; ndio baba wa Wamoabu hata leo.
38 And the younger, she also bore a son, and called his name Ben-ammi — the same is the father of the children of Ammon unto this day.
Binti mdogo naye pia akamzaa mwana, naye akamwita Benami; ndiye baba wa Waamoni hata leo.

< Genesis 19 >