< Ezekiel 22 >

1 Moreover the word of the LORD came unto me, saying:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 'Now, thou, son of man, wilt thou judge, wilt thou judge the bloody city? then cause her to know all her abominations.
“Sasa wewe, mwanadamu, Je! Utanihukumu? Utauhukumu mji kwa damu? Mfanye ajue machukizo yake yote.
3 And thou shalt say: Thus saith the Lord GOD: O city that sheddest blood in the midst of thee, that thy time may come, and that makest idols unto thyself to defile thee;
Utasema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Huu ndiyo mji umbao umwagao damu kati yake ili kwamba mda wake ufike; mji ufanyao sanamu ili ujitie unajisi.
4 thou art become guilty in thy blood that thou hast shed, and art defiled in thine idols which thou hast made; and thou hast caused thy days to draw near, and art come even unto thy years; therefore have I made thee a reproach unto the nations, and a mocking to all the countries!
Umekuwa na hatia kwa damu uliyoimwaga, na kufanya unajisi kwa sanamu ulizozitengeneza. Kwa kuwa umezileta karibu siku zako na kuzikaribia siku zako za mwisho. Kwa hiyo nitakufanya lawama kwa mataifa na kejeli katika uso wa kila nchi.
5 Those that are near, and those that are far from thee, shall mock thee, thou defiled of name and full of tumult.
Wote walio karibu na wale walio mbali nawe watakudhihaki, wewe mji mchafu, ujulikanao kila mahali kwa sifa mbaya kama kujaa machafuko.
6 Behold, the princes of Israel, every one according to his might, have been in thee to shed blood.
Tazama! Wakuu wa Israeli, kila mmoja kwa nguvu yake, wamekuja kwako kumwaga damu.
7 In thee have they made light of father and mother; in the midst of thee have they dealt by oppression with the stranger; in thee have they wronged the fatherless and the widow.
Wamefanya udanganyifu kwa baba na mama ndani yako, na wametenda yaliyo kinyume juu ya wageni kati yako. Wamewatenda vibaya yatima na wajane ndani mwako.
8 Thou hast despised My holy things, and hast profaned My sabbaths.
Umevidharau vitu vyangu vitakatifu na kuinajisi Sabato yangu.
9 In thee have been talebearers to shed blood; and in thee they have eaten upon the mountains; in the midst of thee they have committed lewdness.
Watu wasingiziaji wamekuja kati yako ili kumwaga damu, na hula juu ya milima. Hufanya uovu kati yako.
10 In thee have they uncovered their fathers' nakedness; in thee have they humbled her that was unclean in her impurity.
Uchi wa baba umefunuliwa ndani yako. Wamemtukana mwanamke mchafu ndani yako wakati wa uchafu wake.
11 And each hath committed abomination with his neighbour's wife; and each hath lewdly defiled his daughter-in-law; and each in thee hath humbled his sister, his father's daughter.
Watu waliofanya machukizo pamoja na wake za majirani zao, na watu wafanyao uchafu wa aibu kwa mke wa mwanao mwenyewe; watu wawatukanao dada zao wenyewe-binti za baba zao wenyewe-haya yote yapo miongoni mwanu.
12 In thee have they taken gifts to shed blood; thou hast taken interest and increase, and thou hast greedily gained of thy neighbours by oppression, and hast forgotten Me, saith the Lord GOD.
Hawa watu huchukua rushwa kati yenu ili kumwaga damu. Umechukua faida na kuongeza riba nyingi sana, na umenisahau-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
13 Behold, therefore, I have smitten My hand at thy dishonest gain which thou hast made, and at thy blood which hath been in the midst of thee.
Tazama! Kwa mkono wangu nimeipiga faida ambayo uliyoitengeneza kwa njia isiyo halali, na damu iliyo kati yako.
14 Can thy heart endure, or can thy hands be strong, in the days that I shall deal with thee? I the LORD have spoken it, and will do it.
Je! Moyo wako utasimama, mikono yako itakuwa hodari katika siku wakati mimi mwenyewe nitakapo kushughulikia? Mimi, Yahwe, nasema hivi, na nitalifanya.
15 And I will scatter thee among the nations, and disperse thee through the countries; and I will consume thy filthiness out of thee.
Hivyo nitakutawanya kati ya mataifa na kukutawanya kati ya nchi mbali mbali. Katika njia hii, nitausafisha uchafu kutoka kwako.
16 And thou shalt be profaned in thyself, in the sight of the nations; and thou shalt know that I am the LORD.'
Hivyo utakuwa mchafu machoni mwa mataifa. Kisha utajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
17 And the word of the LORD came unto me, saying:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
18 'Son of man, the house of Israel is become dross unto Me; all of them are brass and tin and iron and lead, in the midst of the furnace; they are the dross of silver.
“Mwanadamu, nyumba ya Israeli imekuwa takataka kwangu. Wote wamekuwa masazo ya shaba na bati, na chuma na risasi kati yenu. Watakuwa kama takataka ya fedha katika tanuu.
19 Therefore thus saith the Lord GOD: Because ye are all become dross, therefore, behold, I will gather you into the midst of Jerusalem.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu mmekuwa kama takataka, kwa hiyo, tazama! Nataka kuwakusanya katikakati ya mji wa Yerusalemu.
20 As they gather silver and brass and iron and lead and tin into the midst of the furnace, to blow the fire upon it, to melt it; so will I gather you in Mine anger and in My fury, and I will cast you in, and melt you.
Kama kukusanya fedha na shaba, chuma, risasi na chuma kati ya tanuu ili kuvifukutia moto na kuviyeyusha juu yake, nitawayeyusha. Hivyo nitawakusanya katika hasira yangu na ghadhabu. Nitawaweka hapo na kufukutisha moto juu yake ili kuiyeyusha; hivyo nitawakusanya katika hasira yangu na ghadhabu yangu, na nitawaweka hapo na kuwayeyusha.
21 Yea, I will gather you, and blow upon you with the fire of My wrath, and ye shall be melted in the midst thereof.
Basi nitawakusanya na kuwafukutia kwa moto wa hasira yangu juu yenu hivyo basi mtamwagwa kati yake.
22 As silver is melted in the midst of the furnace, so shall ye be melted in the midst thereof; and ye shall know that I the LORD have poured out My fury upon you.'
Kama kuyeyusha fedha kati ya tanuu, mtayeyushwa chini kati yake, na mtajua yakwamba mimi, Yahwe, nimemwaga ghdhabu yangu juu yenu!”'
23 And the word of the LORD came unto me, saying:
Neno la Yahwe likanijia, kusema,
24 'Son of man, say unto her: Thou art a land that is not cleansed, nor rained upon in the day of indignation.
“Mwanadamu, mwambie, 'Wewe ni nchi ambayo haijasafishwa. Hakuna mvua siku ya hasira!
25 There is a conspiracy of her prophets in the midst thereof, like a roaring lion ravening the prey; they have devoured souls, they take treasure and precious things, they have made her widows many in the midst thereof.
Kuna njama ya manabii wake kati yake, kama simba angurumaye akirarua mawindo. Wamekula uhai na kuchukua utajiri wa thamani; wamewafanya wajane wengi ndani yake!
26 Her priests have done violence to My law, and have profaned My holy things; they have put no difference between the holy and the common, neither have they taught difference between the unclean and the clean, and have hid their eyes from My sabbaths, and I am profaned among them.
Makuhani wake hufanya kinyume na sheria yangu, na wamevinajisi vitu vyangu vitakatifu. Hawawezi kutofautisha kati ya vitu vitakatifu na vitu vya najisi. Wanaficha macho yao kutoka Sabato zangu hivyo basi nimetiwa unajisi kati yao.
27 Her princes in the midst thereof are like wolves ravening the prey: to shed blood, and to destroy souls, so as to get dishonest gain.
Wakuu wake ndani mwake wamekuwa kama mbwa mwitu wakirarua mawindo yao. Wamemwaga damu na kuharibu maisha, ili kupata faida kwa njia ya udanganyifu.
28 And her prophets have daubed for them with whited plaster, seeing falsehood, and divining lies unto them, saying: Thus saith the Lord GOD, when the LORD hath not spoken.
Manabii wake wamepakwa chokaa; wanaona maono ya uongo na kutabiri uongo kwao. Wanasema “Bwana Yahwe asema hivi”' wakati Yahwe hajanena.
29 The people of the land have used oppression, and exercised robbery, and have wronged the poor and needy, and have oppressed the stranger unlawfully.
Watu wa nchi wamewakandamiza kwa kutaka kwa nguvu na kuwanyang'anya kwa nguvu, na wamewatesa maskini na wahitaji, na kuwakandamiza wageni bila haki.
30 And I sought for a man among them, that should make up the hedge, and stand in the breach before Me for the land, that I should not destroy it; but I found none.
Hivyo nimetafuta mtu kutoka kwao ambaye ataweza kujenga ukuta na ambaye atakayeweza kusimama mbele yangu katika uvunjaji wake kwa ajili ya nchi basi sitaweza kuiharibu, lakini sikuona mtu.
31 Therefore have I poured out Mine indignation upon them; I have consumed them with the fire of My wrath; their own way have I brought upon their heads, saith the Lord GOD.'
Hivyo nitaimwaga ghadhabu yangu juu yao. Nitawamaliza kwa moto wa ghadhabu yangu na kuweka njia yao juu ya vichwa vyao wenyewe-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'

< Ezekiel 22 >