< Ecclesiastes 7 >
1 A good name is better than precious oil; and the day of death than the day of one's birth.
Afadhali sifa nzuri kuliko manukato safi, nayo siku ya kufa kuliko ya kuzaliwa.
2 It is better to go to the house of mourning, than to go to the house of feasting; for that is the end of all men, and the living will lay it to his heart.
Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu, kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu, imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao.
3 Vexation is better than laughter; for by the sadness of the countenance the heart may be gladdened.
Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo.
4 The heart of the wise is in the house of mourning; but the heart of fools is in the house of mirth.
Moyo wa wenye hekima uko katika nyumba ya msiba, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya anasa.
5 It is better to hear the rebuke of the wise, than for a man to hear the song of fools.
Afadhali kusikia karipio la mtu mwenye hekima, kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
6 For as the crackling of thorns under a pot, so is the laughter of the fool; this also is vanity.
Kama ilivyo kuvunjika kwa miiba chini ya sufuria, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Hili nalo pia ni ubatili.
7 Surely oppression turneth a wise man into a fool; and a gift destroyeth the understanding.
Dhuluma humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, nayo rushwa huuharibu moyo.
8 Better is the end of a thing than the beginning thereof; and the patient in spirit is better than the proud in spirit.
Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake, uvumilivu ni bora kuliko kiburi.
9 Be not hasty in thy spirit to be angry; for anger resteth in the bosom of fools.
Usiwe mwepesi kukasirika rohoni mwako, kwa kuwa hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
10 Say not thou: 'How was it that the former days were better than these?' for it is not out of wisdom that thou inquirest concerning this.
Usiseme, “Kwa nini siku za kale zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa maana si hekima kuuliza maswali kama hayo.
11 Wisdom is good with an inheritance, yea, a profit to them that see the sun.
Hekima, kama ulivyo urithi, ni kitu chema na huwafaidia wale walionalo jua.
12 For wisdom is a defence, even as money is a defence; but the excellency of knowledge is, that wisdom preserveth the life of him that hath it.
Hekima ni ulinzi kama fedha ilivyo ulinzi, lakini faida ya maarifa ni hii: kwamba hekima huhifadhi maisha ya aliye nayo.
13 Consider the work of God; for who can make that straight, which He hath made crooked?
Tafakari kile Mungu alichokitenda: Nani awezaye kunyoosha kile ambacho yeye amekipinda?
14 In the day of prosperity be joyful, and in the day of adversity consider; God hath made even the one as well as the other, to the end that man should find nothing after him.
Nyakati zikiwa nzuri, ufurahi, lakini nyakati zikiwa mbaya, tafakari: Mungu amefanya hiyo moja, naam, sanjari na hiyo nyingine. Kwa hiyo, mwanadamu hawezi kugundua kitu chochote kuhusu maisha yake ya baadaye.
15 All things have I seen in the days of my vanity; there is a righteous man that perisheth in his righteousness, and there is a wicked man that prolongeth his life in his evil-doing.
Katika maisha haya yangu ya ubatili nimeshaona haya mawili: mtu mwadilifu akiangamia katika uadilifu wake, naye mtu mwovu akiishi maisha marefu katika uovu wake.
16 Be not righteous overmuch; neither make thyself overwise; why shouldest thou destroy thyself?
Usiwe mwenye haki kupita kiasi, wala usiwe na hekima kupita kiasi: kwa nini kujiangamiza mwenyewe?
17 Be not overmuch wicked, neither be thou foolish; why shouldest thou die before thy time?
Usiwe mwovu kupita kiasi, wala usiwe mpumbavu: kwa nini kufa kabla ya wakati wako?
18 It is good that thou shouldest take hold of the one; yea, also from the other withdraw not thy hand; for he that feareth God shall discharge himself of them all.
Ni vyema kushika hilo moja na wala usiache hilo jingine likupite. Mtu amchaye Mungu ataepuka huko kupita kiasi.
19 Wisdom is a stronghold to the wise man more than ten rulers that are in a city.
Hekima humfanya yeye aliye nayo kuwa na uwezo zaidi kuliko watawala kumi katika mji.
20 For there is not a righteous man upon earth, that doeth good, and sinneth not.
Hakuna mtu mwenye haki duniani ambaye hufanya mambo ya haki na kamwe asitende dhambi.
21 Also take not heed unto all words that are spoken, lest thou hear thy servant curse thee;
Usitie maanani kila neno linalosemwa na watu, la sivyo, waweza kumsikia mtumishi wako akikulaani:
22 for oftentimes also thine own heart knoweth that thou thyself likewise hast cursed others.
kwa kuwa unafahamu moyoni mwako kwamba wewe mwenyewe mara nyingi umewalaani wengine.
23 All this have I tried by wisdom; I said: 'I will get wisdom'; but it was far from me.
Yote haya niliyajaribu kwa hekima, nikasema, “Nimeamua kuwa na hekima”: lakini hii ilikuwa nje ya uwezo wangu.
24 That which is is far off, and exceeding deep; who can find it out?
Vyovyote hekima ilivyo, hekima iko mbali sana na imejificha, ni nani awezaye kuigundua?
25 I turned about, and applied my heart to know and to search out, and to seek wisdom and the reason of things, and to know wickedness to be folly, and foolishness to be madness;
Nikageuza fikira zangu ili kuelewa, kuchunguza na kuitafuta hekima na kusudi la mambo, na ili kuelewa ujinga wa uovu, na wazimu wa upumbavu.
26 and I find more bitter than death the woman, whose heart is snares and nets, and her hands as bands; whoso pleaseth God shall escape from her; but the sinner shall be taken by her.
Nimeona jambo lililo chungu kuliko mauti, mwanamke ambaye ni mtego, ambaye moyo wake ni wavu wa kutegea na mikono yake ni minyororo. Mtu ampendezaye Mungu atamkwepa, bali mwenye dhambi atanaswa naye.
27 Behold, this have I found, saith Koheleth, adding one thing to another, to find out the account;
Mhubiri anasema, “Tazama, hili ndilo nililogundua: “Nimegundua kitu kimoja baada ya kingine nilipokuwa katika kusudi la mambo:
28 which yet my soul sought, but I found not; one man among a thousand have I found; but a woman among all those have I not found.
ningali natafiti lakini sipati: nilimpata mwanaume mmoja mnyofu miongoni mwa elfu, lakini hakuna mwanamke mmoja mnyofu miongoni mwao.
29 Behold, this only have I found, that God made man upright; but they have sought out many inventions.
Hili ndilo peke yake nililolipata: Mungu amemuumba mwanadamu mnyofu, lakini mwanadamu amebuni mambo mengi.”