< 2 Chronicles 7 >

1 Now when Solomon had made an end of praying, the fire came down from heaven, and consumed the burnt-offering and the sacrifices; and the glory of the LORD filled the house.
Sasa Selemani alipokuwa amemaliza kuomba, moto ukaja kutoka mbinguni na kuiteketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu, na utukufu wa Yahwe ukaijaza nyumba.
2 And the priests could not enter into the house of the LORD, because the glory of the LORD filled the LORD'S house.
Makuhani hawakuweza kuingia kwenye nyumba ya Yahwe, kwa sababu utukufu wake uliijaza nyumba yake.
3 And all the children of Israel looked on, when the fire came down, and the glory of the LORD was upon the house; and they bowed themselves with their faces to the ground upon the pavement, and prostrated themselves, and gave thanks unto the LORD; 'for He is good, for His mercy endureth for ever.'
Watu wote wa Israeli wakaangalia juu moto uliposhuka chini na utukufu wa Yahwe ulikuwa juu ya nyumba. Wakalala kwa nyuso zao juu ya sakafu ya mawe, wakaabudu, na kutoa shukrani kwa Yahwe. Wakasema, “Kwa maana yeye ni mwema, kwa maana agano lake la kifame ladumu milele.”
4 And the king and all the people offered sacrifice before the LORD.
Kwa hiyo mfalme na watu wote wakamtolea Yahwe sadaka Yahwe.
5 And king Solomon offered a sacrifice of twenty and two thousand oxen, and a hundred and twenty thousand sheep. So the king and all the people dedicated the house of God.
Mfalme Selemani akatoa sadaka ya ng'ombe ishirini na mbili elfu na kondoo 120, 000 na mbuzi. Kwa hiyo mfalme na watu wote wakaiweka wakifu nyumba ya Mungu.
6 And the priests stood, according to their offices; the Levites also with instruments of music of the LORD, which David the king had made, to give thanks unto the LORD, for His mercy endureth for ever, with the praises of David by their hand; and the priests sounded trumpets over against them; and all Israel stood.
Makuhani wakasimama, kila mmoja akasimama mahali pake pa kuhudumu; Walawi pia pamoja na vyombo vya muziki vya Yahwe, ambavyo mfalme Daudi alivitengeza kwa ajili ya kumpa shukrani Yahwe katika nyimbo, “Kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.” Makuhani wote wakapiga matarumbeta mbele yao, na Israeli wote wakasimama.
7 Moreover Solomon hallowed the middle of the court that was before the house of the LORD; for there he offered the burnt-offerings, and the fat of the peace-offerings; because the brazen altar which Solomon had made was not able to receive the burnt-offering, and the meal-offering, and the fat.
Selemani akaitakasa sehemu ya katikati ya kiwanja cha mfalme mbele ya nyumba ya Yahwe. Humo akatoa sadaka za kuteketezwa na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba ambayo alikuwa ametengeza haikuweza kuzibeba sadaka, sadaka za nafaka, na za mafuta.
8 So Solomon held the feast at that time seven days, and all Israel with him, a very great congregation, from the entrance of Hamath unto the Brook of Egypt.
Kwa hiyo Selemani akaitisha sikukuu wakati huo kwa siku saba, na Israeli wote pamaoja naye, kusanyiko kubwa, kutoka Lebo Hamathi mpaka kijito cha Misiri.
9 And on the eighth day they held a solemn assembly; for they kept the dedication of the altar seven days, and the feast seven days.
Siku ya nane wakaitisha kusanyiko la makini, kwa maana kwa siku saba walishika kuwekwa wakfu kwa ile madhabahu.
10 And on the three and twentieth day of the seventh month he sent the people away unto their tents, joyful and glad of heart for the goodness that the LORD had shown unto David, and to Solomon, and to Israel His people.
Katika siku ya ishini na tatu ya mwezi wa saba, Selemani akawatanya watu kwenda kwenye nyumba zao kwa furaha na mioyo ya shangwe kwa sababu ya wema aliokuwa ameuonesha Yahwe kwa Daudi, Selemani, Israeli, na watu wake.
11 Thus Solomon finished the house of the LORD, and the king's house; and all that came into Solomon's heart to make in the house of the LORD, and in his own house, he prosperously effected.
Hivyo Selemani akaimaliza nyumba ya Yahwe na nyumba yake mwenyewe. Kila kitu kilichokuja katika moyo wa Selemani kwa ajili ya kukitengeneza katika nyumba ya mfalme na katika nyumba yake mwenyewe, alikitimiza kwa mafanikio.
12 And the LORD appeared to Solomon by night, and said unto him: 'I have heard thy prayer, and have chosen this place to Myself for a house of sacrifice.
Yahwe akamtokea Selemani usiku na kusema kwake, “Nimesikia maombi yako, na nimeichagua sehemu hii kwa ajili yangu mwenyewe kama nyumba ya dhabihu.
13 If I shut up heaven that there be no rain, or if I command the locust to devour the land, or if I send pestilence among My people;
Kama nitazifunga mbingu ili kwamba kusiwepo mvua, au kama nitaamuru nzige waimeze nchi, au kama nitatuma magonjwa kati kati ya watu wangu,
14 if My people, upon whom My name is called, shall humble themselves, and pray, and seek My face, and turn from their evil ways; then will I hear from heaven, and will forgive their sin, and will heal their land.
kisha watu wangu, ambao wameitwa kwa jina langu, watajinyenyekeza, kuomba, kuutafuta uso wangu, na kuziacha njia zao mbaya, nitasikia kutoka mbinguni, kuwasamehe dhambi zao, na kuiponya nchi yao.
15 Now Mine eyes shall be open, and Mine ears attent, unto the prayer that is made in this place.
Sasa macho yangu yatakuwa wazi na masikio yangu yatasikiliza maombi yanayofanywa katika sehemu hii.
16 For now have I chosen and hallowed this house, that My name may be there for ever; and Mine eyes and My heart shall be there perpetually.
Kwa maana sasa nimeichagua na kauitakasa nyumba hii ili kwamba jina langu lipate kuwa humo milele. Masikio yangu na moyo wangu vitakuwako kila siku.
17 And as for thee, if thou wilt walk before Me as David thy father walked, and do according to all that I have commanded thee, and wilt keep My statutes and Mine ordinances;
Kwako wewe, kama utatembe mbele zangu kama baba yako Daudi alivyotembea, ukitii yote nilyokuamuru na kuzishika sheria zangu na maagizo yangu,
18 then I will establish the throne of thy kingdom, according as I covenanted with David thy father, saying: There shall not fail thee a man to be ruler in Israel.
basi nitakithibitisha kiti cha enzi cha ufalme wako, kama nilivyosema katika agano na Daudi baba yako, niliposema, 'Mzaliwa wako hatashindwa kamwe kuwa mtawala katika Israeli.'
19 But if ye turn away, and forsake My statutes and My commandments which I have set before you, and shall go and serve other gods, and worship them;
Lakin ukigeuka, na kuzisahau sheria zangu na amri amabzo nimeweka mbele yenu, na kama utaenda kuabudu miungu wengine na kuwasujudia,
20 then will I pluck them up by the roots out of My land which I have given them; and this house, which I have hallowed for My name, will I cast out of My sight, and I will make it a proverb and a byword among all peoples.
basi nitawang'oa kutoka kwenye nchi yangu amabayo nimewapa. Nyumba hii ambayo nimeitakasa kwa ajili ya jina langu, nitaitupilia mbali kutoka mbele zangu, na nitaifanya kuwa methali na utani miongini mwa watu wote.
21 And this house, which is so high, every one that passeth by it shall be astonished, and shall say: Why hath the LORD done thus unto this land, and to this house?
Ingawa hekalu hili hili zuri sana kwa sasa, kila mtu apitaye karibu yake atashangazwa na ataguna. Watauliza, 'Kwa nini Yahwe ameifanyia hivi nchi hii na nyumba hii',
22 And they shall answer: Because they forsook the LORD, the God of their fathers, who brought them forth out of the land of Egypt, and laid hold on other gods, and worshipped them, and served them; therefore hath He brought all this evil upon them.'
wengine watajibu, 'Kwa sababu walimsahau Yahwe, Mungu wao, ambaye alikuwa amewatoa babu zao nje ya nchi ya Misiri, na wakashikamana na miungu wengine na kuwainamia chini na kuwaabudu. Hii ndiyo maana Yahwe ameleta majanga haya yote juu yao”

< 2 Chronicles 7 >